Wakati wa uchunguzi wa kwanza wa afya wa Rais George H.W. Bush mwaka 1989, alionekana na madaktari bingwa watano tu, kwa mujibu wa taarifa y...
Wakati wa uchunguzi wa kwanza wa afya wa Rais George H.W. Bush mwaka 1989, alionekana na madaktari bingwa watano tu, kwa mujibu wa taarifa ya Ikulu ya Marekani (White House) ya wakati huo. Miaka 12 baadaye, mtoto wake, George W. Bush, alifanyiwa uchunguzi na madaktari bingwa 12 katika uchunguzi wake wa kwanza akiwa rais, maafisa wa White House walisema.
Hata hivyo, Rais Donald Trump anaonekana kuweka rekodi mpya: madaktari bingwa 22 walimfanyia tathmini katika uchunguzi wake wa afya wa hivi karibuni .
Idadi hiyo ni karibu mara mbili ya idadi ya wataalamu waliomfanyia tathmini Trump katika uchunguzi wake wa afya uliopita akiwa rais, kulingana na mapitio ya taarifa zilizowekwa wazi na madaktari wa Trump.
Vilevile, takwimu hiyo inawakilisha idadi kubwa zaidi ya madaktari bingwa kuwahi kumfanyia tathmini rais katika ziara moja ya matibabu, kwa mujibu wa mapitio ya kumbukumbu na taarifa za umma.
Jambo hili limeibua maswali kutoka kwa madaktari wa nje ambao walisema tayari walikuwa na shaka na taarifa zinazotolewa na White House kuhusu afya ya Trump, ambaye anakaribia umri wa miaka 80.
“Hiyo ni idadi isiyo ya kawaida,” alisema Jonathan Reiner, daktari wa moyo wa muda mrefu wa aliyekuwa Makamu wa Rais, Dick Cheney. “Wanawakilisha fani gani za ubingwa? Kwa nini wawe wengi kiasi hicho?”
Maafisa wa White House walisema kuwa idadi hiyo iliendana na hitaji la kufanya "tathmini kamili na ya kinga" kwa rais. Sean Barbabella, daktari wa rais, alisema tathmini hiyo ilibaini kuwa Trump yuko kwenye "afya bora kabisa."
“Kuhusika kwa madaktari bingwa wengi kunaakisi tathmini ya kina na ya taaluma mbalimbali inayoendana na taratibu bora zaidi za huduma ya matibabu kwa ngazi ya viongozi wakuu,” White House ilisema kwenye taarifa yake.
Ofisa mmoja wa White House alisema kuwa madaktari wanaoshirikiana na Chuo Kikuu cha Harvard, Chuo Kikuu cha Duke na taasisi nyingine maarufu walisaidia kufanya tathmini hiyo. Afisa huyo pia alisema kuwa baadhi ya madaktari wa jumla (generalists) walijumuishwa katika hesabu hiyo ya serikali ya wataalamu 22.
“Hatuna cha kuficha,” afisa huyo alisema.
Mara nyingi White House imekuwa ikikataa kujibu maswali maalum kuhusu tathmini za matibabu za Trump, kama vile nini kilichomfanya rais kufanyiwa uchunguzi wa pili wa kimwili katika Kituo cha Kitaifa cha Matibabu cha Kijeshi cha Walter Reed mwaka jana.
Kawaida marais hufanya ziara moja tu ya kila mwaka isipokuwa kama wana dharura ya kiafya. Karibu miezi mitatu baada ya ziara hiyo, na baada ya awali kuwaambia waandishi wa habari kuwa alikuwa amefanyiwa uchunguzi wa MRI, Trump na White House walifafanua kuwa rais alikuwa amepata kipimo cha CT scan kama sehemu ya tathmini yake.
Ripoti za matibabu za Trump pia hazijumuishi tena dawa ya kawaida ya kuzuia kukatika kwa nywele ambayo madaktari wake walisema alikuwa akitumia mara kwa mara wakati wa muhula wake wa kwanza madarakani. Maafisa wa White House wamekataa kutoa maoni yao kuhusu matumizi ya zamani ya Trump ya dawa hiyo, finasteride, na iwapo ameacha kuitumia.
Uchunguzi huu wa kina wa afya ya Trump unakuja huku kukiwa na maswali mapana zaidi kuhusu utimamu wa rais wa sasa na mtangulizi wake, Joe Biden, kuhudumu kama amiri jeshi mkuu. Biden, ambaye alikuwa na umri wa miaka 82 alipoondoka madarakani, na Trump, ambaye anafikisha umri wa miaka 80 mnamo Juni 14, ndio wanaume wawili wenye umri mkubwa zaidi kuwahi kuhudumu kama rais.
Karine Jean-Pierre, ambaye alihudumu kama katibu wa vyombo vya habari wa Biden, alisema katika mkutano na waandishi wa habari mnamo Februari 2024 kwamba timu ya "madaktari 20" walishiriki katika tathmini ya matibabu ya Biden huko Walter Reed mwaka huo.
Serikali zilizopita mara nyingi zimeamua kutofichua idadi maalum ya madaktari bingwa wanaoshauri katika tathmini za matibabu za marais, ambazo kijadi hufanyika Walter Reed.
Marais hawatakiwi kisheria kufichua kumbukumbu zao za afya, ingawa wabunge wa vyama vyote viwili wametoa wito wa uwepo wa ukaguzi zaidi kwa wakuu wa nchi, kama vile kuundwa kwa tume huru inayoweza kutathmini afya ya rais.
Lakini kumbukumbu na taarifa zilizopo wazi kwa umma zinaonyesha kuwa idadi ya wataalamu wanaokagua afya ya rais inaonekana kuongezeka kwa kasi sana.
Madaktari bingwa watano waliohusika katika uchunguzi wa Rais George H.W. Bush mnamo Mei 1989 walijumuisha daktari wa macho, daktari wa mfumo wa mkojo, daktari wa ngozi na madaktari wawili wa mzio (allergists) — maafisa wa White House walisema wakati huo. Bush mwenye umri wa miaka 65 kisha aliononana na madaktari bingwa wanane mwaka uliofuata, ikiwa ni pamoja na daktari wa eksirei (radiologist), daktari wa moyo na daktari wa viungo (rheumatologist), White House ilisema.
Mtoto wake, Rais George W. Bush, aliononana na madaktari bingwa 12 katika uchunguzi wake wa afya wa mwaka 2001, maafisa wa White House walisema wakati huo.
Wakati maswali yakiwazunguka watu wengi kuhusu utimamu wa Trump katika mwaka wake wa kwanza madarakani, Ronny Jackson, ambaye alihudumu kama daktari wa Trump katika muhula wake wa kwanza na sasa ni mbunge wa chama cha Republican kutoka Texas, aliandaa madaktari bingwa 13 ili wamwone rais, aliandika katika kitabu chake cha kumbukumbu.
“Sikufanya uchunguzi huu wa kimwili peke yangu; nilisaidiwa na kamati nzima ya madaktari bingwa wa kiwango cha juu huko Walter Reed, ikijumuisha wale waliobobea katika magonjwa ya ngozi, mifupa, mfumo wa chakula, macho, mfumo wa mkojo, magonjwa ya mapafu, masikio, pua na koo (otolaryngology), na magonjwa ya moyo,” Jackson aliandika katika kitabu chake, “Holding the Line.”
“Daktari wa moyo alifanya uchunguzi wake wa moyo. Daktari wa mapafu alifanya uchunguzi wake wa mapafu na vipimo vya utendaji wa mapafu, daktari wa ngozi alifanya uchunguzi wake wa ngozi, na kadhalika.”
Trump aliononana na madaktari bingwa 11 katika uchunguzi wake wa afya wa 2019 na madaktari bingwa 14 katika uchunguzi wake wa mwaka jana, kwa mujibu wa ripoti za matibabu zilizopita zilizotolewa na White House.
SOURCE: Washington Post

COMMENTS