BALOZI OMAR: SEKTA BINAFSI NI INJINI YA TANZANIA KUFIKIA MALENGO YA DIRA 2050

  Serikali imetoa wito kwa wadau wa sekta ya fedha, wawekezaji na sekta binafsi nchini kuunganisha nguvu katika kubadili akiba za Watanzania...

 



Serikali imetoa wito kwa wadau wa sekta ya fedha, wawekezaji na sekta binafsi nchini kuunganisha nguvu katika kubadili akiba za Watanzania kuwa mitaji ya uwekezaji yenye tija, itakayochochea uzalishaji, kuongeza ajira, mauzo ya nje na kukuza uchumi kwa mujibu wa Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2050.

Wito huo umetolewa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), wakati alipokuwa Mgeni Rasmi katika halfa ya Mjadala wa Bodi ya Wakurugenzi na Wajumbe wa Jukwaa la Wakurugenzi Wakuu wa Tanzania (CEOrt) unaofanyika kila Mwezi” Board of Directors and Members of the CEO Roundtable of Tanzania (CEOrt) Monthly Dialogue”, iliyofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam.

Mhe. Balozi Omar alisema kuwa utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, ambayo inalenga kuifanya Tanzania kuwa na uchumi wenye thamani ya takribani dola za Marekani trilioni moja, huku pato la mtu mmoja mmoja likitarajiwa kuvuka dola 7,000 ifikapo mwaka 2050, lakini pia uchumi wa viwanda, jumuishi na unaoongozwa na sekta binafsi.

“Utekelezaji wa Dira 2050 kupitia Mpango wa Muda Mrefu wa Maendeleo na Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Miaka Mitano (FYDP IV) umeweka msisitizo mkubwa kwa sekta binafsi, ambapo mfumo wa uwekezaji wa uwiano wa asilimia 70 kwa 30 unaiweka sekta binafsi kama injini kuu ya ukuaji na ufadhili wa maendeleo” alisema Mhe. Balozi Omar.

Aliongeza kuwa Utekelezaji wa FYDP IV unahitaji uwekezaji unaokadiriwa kufikia takribani Shilingi trilioni 477, ambapo sekta binafsi inatarajiwa kugharamia takribani asilimia 70, sawa na Shilingi trilioni 324.49.

Mhe. Balozi Omar, alisisitiza kuwa takwimu hizo zinaonesha wazi kuwa Tanzania haiwezi kufikia malengo yake ya maendeleo kwa kutegemea bajeti ya Serikali, mikopo ya nje au misaada ya maendeleo pekee, bali inapaswa kuongeza uwezo wa kukusanya na kutumia mitaji ya ndani na ya sekta binafsi.

Akizungumzia Mfumo wa fedha, Mhe. Balozi Omar alisema sekta ya fedha nchini imeendelea kuwa imara licha ya changamoto na misukosuko ya uchumi duniani, ikiwa imechangiwa na misingi imara ya uchumi na shughuli endelevu za kiuchumi na mageuzi mbalimbali katika sekta hiyo yameendelea kuweka mazingira wezeshi kwa ukuaji wa sekta huku mikopo kwa sekta binafsi ikikua kwa wastani wa zaidi ya asilimia 20 na mikopo chechefu ikiendelea kudhibitiwa chini ya kiwango kinachopendekezwa cha asilimia tano.

“Mchango wa sekta ya fedha katika Pato la Taifa umeongezeka hadi kufikia asilimia 4.3, huku ujumuishaji wa kifedha kwa watu wazima ukifikia asilimia 76, Maendeleo haya yanatoa msingi mzuri wa kuongeza uwezo wa mfumo wa fedha katika kukusanya akiba na kuzielekeza kwenye uwekezaji wenye tija” alisema Mhe. Balozi Omar.

Aidha, alisema Serikali inakamilisha mchakato wa kuidhinisha awamu ya pili ya Blueprint for Regulatory Reforms (MKUMBI II), ambayo inalenga kuendana na mabadiliko ya sasa ya kiuchumi, kiteknolojia na kibiashara sambamba na kuendelea kufanya mageuzi ya kisheria, kiutawala na kitaasisi yanayolenga kurahisisha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini.

Alisisitiza umuhimu wa kuongeza uwekezaji wa ndani, akieleza kuwa pamoja na uwekezaji wa moja kwa moja kutoka nje (FDI) umeongezeka kutoka dola milioni 1,656 mwaka 2024 hadi dola milioni 1,718 mwaka 2025, sawa na ongezeko la asilimia 3.7, kuwa muhimu katika kuleta mitaji, teknolojia, utaalamu na masoko ya kimataifa, Watanzania wanapaswa kuwezeshwa kushiriki zaidi katika kuwekeza ndani ya uchumi wao wenyewe.

“Nawasisitiza umuhimu wa kuimarisha na kuongeza ushiriki katika masoko ya mitaji nchini, akieleza kuwa masoko yenye kina na ukwasi yanaweza kuwa chanzo muhimu cha mitaji ya muda mrefu kwa ajili ya uwekezaji na Serikali itaendelea kuweka mazingira wezeshi ya kisheria na udhibiti yatakayowezesha kuibuka kwa bidhaa mbalimbali za masoko ya mitaji, huku ushiriki wa wananchi katika hati fungani za Serikali, mifuko ya uwekezaji na soko la hisa ukiendelea kuhamasishwa” alisema Mhe. Balozi Omar.

Aliongeza kuwa Tanzania tayari ina msingi mzuri wa kifedha unaojumuisha mfumo wa benki unaokua, mifuko ya pensheni na taasisi za fedha zenye mali zinazoongezeka, ushiriki mkubwa wa wananchi katika bidhaa rasmi za uwekezaji, masoko ya mitaji yanayopanuka pamoja na sekta binafsi yenye nguvu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Jukwaa la Wakurugenzi Wakuu wa Tanzania (CEOrt), Bw. David Tarimo, alisema mjadala huo umejikita katika namna ya kubadilisha akiba zilizopo nchini kuwa mtaji wa kukuza uchumi na kuongeza upatikanaji wa mtaji wa ndani.

Alisema mjadala huo pia umeangazia malengo makubwa yaliyowekwa kupitia Dira ya Maendeleo ya Taifa ya Miaka 50, ambayo kwa kiasi kikubwa yanategemea ushiriki na uwekezaji wa sekta binafsi, na Mpango wa Tano wa Maendeleo wa Miaka Mitano umeweka msisitizo mkubwa zaidi katika uwekezaji wa sekta binafsi ikilinganishwa na mipango ya miaka iliyopita.

Bw. Tarimo amesema kikao hicho kimewapa wadau fursa ya kubadilishana mawazo kuhusu hatua zinazopaswa kuchukuliwa ili kuimarisha mazingira ya uwekezaji na kuongeza uwezo wa sekta binafsi kushiriki kikamilifu katika kufikia malengo ya maendeleo ya Taifa.

“Jukwaa hili lmepata fursa ya kusikiliza mipango ya Serikali kuhusu utekelezaji wa Dira hiyo, huku wajumbe nao wakitoa mawazo na mapendekezo yanayolenga kusaidia kufanikisha malengo hayo” alisema Bw. Tarimo.

Aliongeza kuwa CEOrt itaendelea kushirikiana na Serikali kubaini maeneo yanayohitaji maboresho na kuunga mkono mageuzi katika kanuni na taratibu, ili kujenga mazingira ya biashara yaliyo rafiki, rahisi na yenye gharama nafuu, hususan kwa wafanyabiashara wadogo.

COMMENTS

Name

Anga,12,Arusha,27,batiki,1,Burudani,469,burundani,2,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,78,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,316,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,haba,1,habar,3,Habari,7504,habari dodoma,41,habari. dodoma,32,habaria,1,hadithi,27,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,52,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,7,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,771,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,miochezo,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,376,muziki na fasheni,21,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,10,SAYANSI ANGA,14,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,17,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,urembo,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTALII,1,UTAMADUNI,4,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: BALOZI OMAR: SEKTA BINAFSI NI INJINI YA TANZANIA KUFIKIA MALENGO YA DIRA 2050
BALOZI OMAR: SEKTA BINAFSI NI INJINI YA TANZANIA KUFIKIA MALENGO YA DIRA 2050
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgPxZkAFxSNP7TQFv7K8CDLnGjhzy6yllTSCQrlO0ctLrtRtIGptmUjdMj8N3__RRnafPU82o64GnjUiMIaEamPA_BJv7hWhoXcpR1_88IvzVSvO1QNZ4TdKbBDOOH9pTXehYCx5NFNhFCh-xhl5gel4NcxMDRrl9tbEspEyC7BEsEK-cMJ-fsXeuq68X6H/s320/omar2.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgPxZkAFxSNP7TQFv7K8CDLnGjhzy6yllTSCQrlO0ctLrtRtIGptmUjdMj8N3__RRnafPU82o64GnjUiMIaEamPA_BJv7hWhoXcpR1_88IvzVSvO1QNZ4TdKbBDOOH9pTXehYCx5NFNhFCh-xhl5gel4NcxMDRrl9tbEspEyC7BEsEK-cMJ-fsXeuq68X6H/s72-c/omar2.jpg
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2026/09/balozi-omar-sekta-binafsi-ni-injini-ya.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2026/09/balozi-omar-sekta-binafsi-ni-injini-ya.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy