MAKALA ya Uhuru
Desemba 9, 1961, Tanzania ilipata Uhuru chini
ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere. Je, Uhuru huu unamaanisha
nini kwetu? Leo hii tunaweza kusimama kidete na kusema ni Uhuru wa kweli
unaotuondoa kwenye utegemezi wa wakoloni tulioachana nao, unaotufanya
tuamue mambo yetu wenyewe kama taifa, unaotuondoa kubughudhiwa na
kuingiliwa na mambo kama magonjwa, njaa, upungufu wa umeme, umasikini na
ujinga? Tupo huru kweli, hebu msikilize Beda Msimbe anavyochambua Uhuru
wa Tanganyika na sasa Tanzania, ikiwa imepita kwenye awamu tatu, na
sasa ya nne inaingia ngwe ya pili. Anaaangalia yote hayo na kushauri
nini kifanyike zaidi ili Uhuru uwe wa kweli au kuuimarisha, furahia makala hii...
![]() |
| Gavana wa mwisho akisindikizwa melini na Julius Nyerere |
Tanzanzania ya
miaka ya sasa inazungumza ufisadi zaidi kuliko hatga kuangalia historia
yao na kuangalia wapi walipojikwaa na badakla yake wanaangalia wapi
walipoangukia.Wakati mwalimu Nyerere anahutibia Bunge kwa mara ya kwanza
baada ta Tanganyika kupata Uhuru alionesha wazi njia ya kufuata, sehemu
kubwa ya njia hiyo ni kupata maendeleo ya kweli kibinadamu kama nchi
kwa kupigana na maadui watatu ambao ni umaskini, ujinga na maradhi.
Kwa
kauli yake hiyo alidhamiria kuonesha njia ya kuondokana na utegemezi na
katika kipindi hicho kauli yake haikuwa Uhuru kazi ya Tanu bali ni
Uhuru na Kazi.
Hata
wakati wa kuangalia miaka mitano ya mwanzo ya uhuru mwaka 1965 historia
iliandika mengi lakini mtu ambaye aliandika kauli tata zilizojadiliwa
kwa kina ni Henry Bienen. Mwandishi huyu katika kitabu chake cha
Tanzania: Party Transformation and Economic Development ilichotolewa na Princeton Unmiversity Press mwaka 1967 alizungumzia kwa kina siasa za Tanzania na maendeleo yake.
Huenda
maneno aliyoyasema wakati huo ingawa wachambuzi wenzake wa enzi hizo
walisema maandishi yake yamepitwa na wakati kutokana na kutokea kwa
Azimio la Arusha, ukiyatazama hutaweza kuyakana kwa leo wakati kilio cha
Tanzania ni ufisadi na mipango ya maendeleo isiyotekelezeka au
isiyokuwa endelevu.
Mwandishi
huyo wa zamani alikuwa anazungumzia haja ya mipangilio ya kisiasa ya
wazi ambayo juu yake ndipo mipango ya maendeleo inaweza kusukwa kwa
ajili ya kusukuma mbele gudrudumu la maendeleo. Kwake yeye aliona wazi
kwamba Tanzania haijapambanua mfumo wa kufuata katika kujenga uchumi
wake na haiwezi kuwa rahisi kuendelea kutegemea mihimili ya kikoloni
kupata maendeleo ya kweli. Mwandishi huyo alisema wazi kwamba pamoja na
Tanu kuwa na uwezo wa kushawishi watu lakini shauri la kiuchumi lilikuwa
ni dogo na kama vile halina mwelekeo wa kweli kama taifa lilififishwa na uwezo mdogo wa kati ndani ya chama wa kubuni mipango na kuiweka katika utekelezaji wa kweli.
Shida kubwa ya hali hiyo kwa mujibu wa mwandishi huyo ilitokana na uongozi
sehemu kubwa kuanza mchakato wa kujineemesha na kuchukua vivazi vya
wazungu waliondoka na kuachana na falsafa nzima ya kuutafuta uhuru.
Kuwepo kwa mwelekeo usioeleweka wa kijamaa kwa mfumo wa Mao na Marx haukutoa
nafasi kubwa ya mabadiko ya kasi kutokana na tofauti za matabaka. Hali
ambayo ilijionesha na kusababisha kuzaliwa kwa Azimio la Arusha kasha
kuwapo kwa Elimu ya kujitegemea na badaye ujamaa na maendeleo vijijini.
Huenda
Bienen kutokana na Uamaerika wake alikosea kuzungumza jinsi mkanganyiko
wa siasa na mchuano wa matabaka unavyomaliza nchi kwa kukosa msingi
imara wa kisiasa wa kujenga miundo mbinu ya maendeleo kipindi hicho
lakini upo ukweli wa leo kwamba taifa la Tanzania limerejea katika
mchakato wa miaka hiyo ya mwanzo ya uhuru kutokana na kuchipuka kw
amsuguano mwingine wa kitabaka ambapo wanajiotokeza watu ambao
wanajijazia mali wanafanya hivyo kwa kuitafuna nchi kwa njia mbalimbali.
Pengine ni Nyerere ambaye alikuwa na mabadiiko
ya kifikira pale ambapo alianza kulidhibiti tabaka hili la watu wenye
nacho na wenye uwezo wa kujilimbikizia mali kuacha kufanya hivyo kwa
kufikiria shauri la Ujamaa na Azimio la Arusha.
Tukiwa katika mwaka 50 bado
tunaweza kujiuliza kama kweli tuko huru, Kimsingi katika dunia hii ya
mtandao Tanzania bado haijawa huru katika mambo yote ambayo Julius
Nyerere Rais wa kwanza wa Tanzania aliyapigania; na katika msingi mbaya
wa mawazo tunaweza kusema kwamba sehemu kubwa ya maendeeo ambayo
yalipatikana miaka kumi baada ya Uhuru hayapo .
Tunachofanya
sasa kama ukimtazama mtunzi mwingine wa mustkabali wa Tanzania Ibrahim
Werrema John katika kitabu chake cha Tanzanians to the Promised Land ni
kutibia sehemu ya juu ya jeraha wakati kidonda kwa ndani bado kibichi na
huenda kikawa kinavunda.
Ukimsoma
Werrema sehemu kubwa ya maandishi yake utagundua kuwa anasisitiza
Watanzania kuliangalia taifa lao kwa namna nyingine kutokana na umaskini
mkubwa kuendelea kuwapo, tofauti kubwa ya kipato, kudidimia kwa elimu na
tatizo la uadilifu na uongozi ambao ndio nyenzo muhimu katika
kufanikisha njia isiyo ya kubahatisha au kudanganya ya uchumi ambao ndio
unaweza kuleta maisha bora kwa wananchi.
Kitabu hiki ambacho kimehaririwa na Jenerali
Ulimwengu na Lisa Smith Holtz kimechambuo uongozi kuanzia enzi za
Mwalimu Nyerere,Mzee Mwinyi, Benjamim Mkapa na kidogo Jakaya
Kiwete.Mtunzi ana maswala ya msingi ambayo anataka watanzania kuyajadili
nap engine katika upofu aliulizia ule ukali wa kijiwe cha mlimani cha kushawishi mawazo makali ya maendeleo imeishia wapi.
Kimsingi
elimu ni mkombozi wa kwanza, lakini kwa taifa ambalo linategemea
utaalamu wa sayansi katika kuchimba madini kutoka nje, elimu yetu ikiwa
ni bora elimu badala ya elimu bora ambayo inaweza kumfanya mtu
kujitambua na kutambua haki yake katika maisha haya bila kujali
uchakachuaji unaofanywa na wanasiasa uchwara.
Ni
wazi mapungufu makubwa ya ushindani na kutaka watu kuwajibika kunafanya
hata kujipanga kuwa na viwanda mama kuwa ni tatizo, taifa likibaki la
wachuuzi zaid kama vile hatuna raslimali za kutufanya kuwa na sauti kubw
aya kicuhumi duniani; lakini hiyo kama si mbaya watanzania wanakosa ule
utashi wa kuangalia hilo kwa undani na kulipatia ufumbuzi
wa utamaduni unaokubalika wa kistaarabu duniani kwa kukomaa kwa
demokrasia na kutambua haki ya mtanzania kwa taifa lake . Kila mtu
anadhani si wajibu wake kuangalia mustakabali wa nchi, tunabaki si tu
wachuuzi bali walalamikaji wakubwa!
Ukiangalia
historia ya nchi hii unaona kwamba miaka ya awali ilikuwa na shida
nkubwa lakini miaka sita baadaye kukawa na nia ya dhati ya kuangalia
maendeleo ya wananchi hasa kwa kuleta nidhamu ya matumizi ya madaraka na
pia kuweka wazi maendeleo ya nchi yanayozingatia watu na si vitu.
Lakini
kwa nchi yenye uchumi mzuri , wakati ule katani ikiwa na heshima kubwa
duniani na akiba nzuri ya fedha za kigeni, Tanzania ilishindwa kuwa na
sera ambayo ingeliweza kusimama kidete katika vurugu za dunia na kuibuka
na misingi imara na si kwa sababu ya ubaya wa sera baada ya Azimio la
Arusha, bali kutokana na uongozi wenyewe kushindwa kutafsiri vyema
kanuni walizojipangia za maendeleo kwa kuzingatia falsafa mpya yenye
kujali maslahi ya watu na kuona aibu ya kujilimbikizia mali.
Lakini ni wazi kuwapo kwa umoja wa kitaifa ambao unatishiwa leo na masuala mapya yanayoambatana
na matabaka ya kijamii,pia ulisabaisha misingi nya uchumi kudharaulika
na kubwa la kuzingatia ni amani na utulivu.
Ingawa
Tanzania ni miongoni mwa nchi chache duniani zenye sifa za kuwa shwari
kijamii na kisiasa, uchumi wake ni mtego mkubwa ambnao nunaweza baadaye
kuleta maporomoko makubwa ya utamaduni wa uvumilivu uliopo kwa miaka 50
sasa.
Ukiangalia kimsingi Nchi hii inapoingia katika miaka 50 bado juhudi
za kuipeleka katika nchi ya maziwa haijapata mwelekeo hasa baada ya
kufumuliwa kwa azimio la Arusha ambalo lina msingi mkubwa katika
uadilifu na utumishi kwa umma; ni katika hili kizazi cha uhuru
kilishuhudia utulivu wa kisiasa na kijamii uliotokana na kipato kuwa
karibu sawa.
Tatizo
kubwa la umaskini linalotokana na msingi duni wa uchumi wa taifa na
kubaki kuwa taifa la kuagiza hata sindano na vijiti vya kusafishia meno
kutoka nje,ndilo hasa linazaa hata myumbisho wa maadili ambapo rushwa
zimetapakaa mpaka katika ngazi ya chini kabisa ya maisha, wajumbe wa
nyumba kumi wakitaka elfu moja kukuandikia karatasi ya kwenda kupeleka
shauri lako Polisi.
Tatizo
la Tanzania kwa sasa ni shida katika uchumi wake ambao kuparaganyika
kwake kunatokana na kukosekana kwa mipango inayofuatiliwa ya kutengeneza
uchumi mdogo kwa lengo la kuuboresha uchumi mkubwa.
Kukosekana
kwa uchumi imara kunaleta pia adha ya kuibuka kw a matatizo mengine kwa
kuwa uchumi imara husaidia sana kuimarisha utendaji wa serikali. Kwa
sasa japo tunasema tumep;iga hatua mbele ya kuangamiza ujinga, lakini
shida kubwa ipo katika maradhi na umaskini na ndipo hapo unapojiuliza
kama kweli ujinga umetoweka katika mazingira kama haya ya sasa.
Tatizo
la maradhi linazidi kukua, malaria ukimwi vikiongoza na hata maradhik
yanayozuilika yanatibuka na kutishia kama kweli fedha nyingi za serikali
hazitayujmima katika kukabiliana na vitu ambavyo vingeliweza kuzuilika.
Swali
la msingi la kujiuliza ni katika mazingira haya ya miaka 50 na mawazo
yale yale na matatizo yale yale tuliyokuwa nayo wakati tunapata uhuru,
kweli tunaweza kusogea mbele? Tukiw abado tunatawaliwa na kupokea
misaada ya maendeleo, kweli hatuhatarishi uwezo wetu wa uhuru na kufuata
wanayotaka wao hao wanatupa ruzuku yao?Si ajabu hata kuharibika kwa
utamaduni wao wanatuvushia na sisi wakitutaka tuheshimu haki za binadamu
pamoja na mashoga, na kuondokana na kanuni zinazozuia watu kuwa
mashoga.
Nyerere
alizungumzia kujilimbikizia mali akafikiria azimio la Arusha, lilileta
jeuri kubwa,leo tunazungumzia mafisadi kama bidhaa iliyoletwa na Azimio
la Zanzibar na tumevikwa na aibu kubwa katika kuwabana hawa walioibukia
katika Azimio la Zanzibar.
Huduma
za jamii bado . Ingawa zipo dalili za kuendeleo kupiga hatua kwa
kukubali tulichokosea katika elimu na kujaribu kuiweka sawa kwa kuwa na
jamii iliyoelimika kwa kuzingatia mpango wa maendeleo (vision 2025).
Hatuwezi
kuwa makini katika mali asili zetu iwe madini au mbuga kama hatuna
elimu ya kutosha ya kuendesha mambo hayo sisi wenyewe au hata kama
tukiwapa watu basi tujue nani anatuibia na nani anastahili kuwapo pale
na tunamwangalia namna gani.
Kwa
umri wa mtu miaka 50 hasa Afrika ni mzee mwenye busara lakini kwa taifa
bado pengine linajivuta na kwa Tanzania mafanikio yaliyopatikana katika jamii yanaonekana kutishiwa na mwenendo usiovumilika wa ufisadi na kutapanya mali za umma kwa kuendekeza rushwa.
Pengine
tunaweza kujidai kuwa tuko huru kama tutakuwa na uhakika wa sekta ya
uchumi zaidi na kuhakikisha kwamba serikali inaendeshwa kwa kanuni na
wafanyakazi wa serikali hawatumii vibaya madaraka yao na kusababisha
matatizo kwa wananchi ambao waliwaweka pale ili kuwasaidia kuwaondolea
matatizo yao.
Katika miaka 50 kuna
kinachoonekana hasa kupunguza umbali na muda wa usafiri kati ya mikoa
inayofanya Tanzania kutoka mji wa biashara wa Dare s salaam, Mwanza na
Arusha. Barabara zimejengwa japo zinaharibika kutokana na kukosekana kwa
busara zinazohitaji hasa fikira za matumizi ya reliu katika kubeba
mizigo mizito.
Pengine
jaribio la kufungua mikoa ya Tanzania inaweza kurekebisha hali ya
uchumi, lakini kama tatizo la nishati litaendelea kutesa nchi hii
kutokana na mipango isiyozingatia hali halisi ya mazingira, Tanzania ya
sasa haitakuwa na tofauti na ile ambayo Mwalimu Nyerere aliichukua
kutoka kwa wakoloni.
Nishati
ni msingi wa uchumi wa kisasa, lakini kama hakuna maana yake hata
viwanda mama haviwezi kuwapo na uimbaji wa sera usiotelekezekana ni sawa
na kuwa na jeraha kubwa lilishonwa juu na ndani likaachwa bila dawa.
mwisho

COMMENTS