TAARIFA YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI MHE.HAMAD RASHID MOHAMED (MB) KUHUSU UTATA WA MAHESABU KATIKA KITABU CHA KWANZA CHA MAPATO YAAN...
TAARIFA YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI
MHE.HAMAD RASHID MOHAMED (MB) KUHUSU UTATA WA MAHESABU KATIKA KITABU CHA KWANZA CHA MAPATO YAANI “VOLUME 1 FINANCIAL STATEMENT AND REVENUE ESTIMATES” KWA MWAKA WA FEDHA WA FEDHA 2008/2009:
_____________________
UTANGULIZI
Mheshimiwa Spika,
Leo Asubuhi ulitoa mwongozo ulioombwa na Kambi ya Upinzani kuhusiana na kukiukwa kwa Kanuni ya 96(1) kuhusiana na matakwa ya kanuni hiyo kwamba “Waziri atapeleka kwa Katibu Makadirio ya Matumizi ya kawaida na ya maendeleo ya Serikali ya mwaka wa fedha unaohusika na nakala ya makadirio hayo itapelekwa na kumfikia kila mbunge angalau siku ishirini na moja kabla ya Mkutano ambao utashughulikia makadirio hayo” ulitoa mwongozo kuwa kuna utata katika kipengele hicho na kuagiza Kamati ya Fedha kupitia Kanuni hiyo na kupendekeza marekebisho stahiki.
Mheshimiwa Spika,
Kutokana na hoja zilizotolewa na Kambi ya Upinzani wakati wa majadala kuwa kuna mapungufu katika Takwimu za Kitabu cha Mapato, Serikali imewasilisha marekebisho ya Takwimu hizo.
Na kwa kuwa Takwimu za ziada zilizowasilishwa na Waziri leo asubuhi kwa njia ya “Addendum to Volume 1” kuonekana bado hazioani na Takwimu zilizoko kwenye Kitabu cha Hotuba ya Waziri uliagiza Kitabu hicho pamoja na Addendum kipitiwe na Kamati ya Fedha na Uchumi na baadaye Mwenyekiti wa Kamati husika na Kambi ya Upinzani tuitolee Taarifa ndani ya Bunge lako Tukufu.
Ninaomba kuchukua nafasi hii kutoa Taarifa kwa niaba ya Kambi ya Upinzani Bungeni.
Mheshimiwa Spika,
Moja, Kambi ya Upinzani imefarijika na unyofu wa Serikali wa kukubali kuwa kulikuwa na mapungufu na makosa ya Kitakwimu katika Kitabu cha kwanza cha Makadirio ya Mapato (Volume 1 cha Financial Statement and Revenue Estimates), na hivyo kuwasilisha Bungeni Nyongeza ya Marekebisho hayo,(Addendum to Volume l ).
Mbili, Mheshimiwa Waziri ameieleza Kamati ya Fedha kuwa mapungufu hayo yametokana na serikali kupata makisio ya awali ambayo miongoni mwake hayakuwa yamethibitishwa na vyombo vinavyochangia mapato ya serikali (Kwa mfano, katika Benki Kuu Serikali ilikisia sh 11 Bilioni lakini baade ikathibitika kuwa ni sh 6 Bilioni). Kambi ya Upinzani imeridhika na maelezo hayo isipokuwa kwamba kwa miaka ijayo kazi hiyo iwe imekamilika kabla ya Makadirio ya Mapato na Matumizi kuwasilishwa Bungeni, ili Bunge kwa niaba ya Wananchi liweze kupitisha jambo lililo na uhakika nalo.
Tatu, Baada ya maelezo ya Waziri wa Fedha na Uchumi, Kambi ya Upinzani imebaini kwamba utegemezi wa Bajeti ya Maendeleo kwa Wahisani bado ni mkubwa mno kwa kiwango cha asilimia 97.5. Hii maana yake ni kwamba tunafanya uchumi wa kuchumia Tumbo (Stomach economy). Kambi ya Upinzani inasisitiza kwamba vyanzo vya Mapato ilivyovibainisha katika Bajeti mbadala vifuatiliwe kikamilifu ili kupunguza utegemezi huu.
Nne, Kambi ya Upinzani bado inasikitishwa na kitendo cha Serikali ya Muungano kutogawa gawio sahihi kutokana na faida ya Benki Kuu kwenda Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa mujibu wa Kumbukumbu za IMF, ilikuwa inamiliki asilimia 11.5 ya Hisa za Benki Kuu (BOT). Hivyo kugawa gawio kwa asilimia 4.5 ni kuipunja Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kupata gawio sahihi kutokana na mtaji wake wakati Benki Kuu inaanza mwaka 1965 baada ya kuvunjwa kwa Bodi ya Sarafu ya Afrika ya Mashariki (East African Currency Board). Kambi ya Upinzani inaitaka Benki Kuu ya Tanzania igawe gawio kwa SMZ kwa mujibu wa hisa zake.
Mheshimiwa Spika,
Tano, Kambi ya Upinzani inasisitiza kuwa katika miaka ijayo Bunge lizingatie Ibara ya 138 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano inayotaja kuwa hakuna Kodi au tozo yeyote inayoweza kutozwa bila idhini ya Bunge au kwa mujibu wa Sheria ya iliyotungwa na Bunge.
Sita, Kambi ya Upinzani inaona upo muhimu pia kufanya marekebisho ya kifungu cha 96 cha Kanuni ya Bunge Toleo la 2007 ili kulifanya Bunge kujadili na kupitisha mapendekezo ya Mapato na Matumizi kama yanavyowasilishwa na Vitabu vyote vinne vya Bajeti badala ya kupitisha matumizi tu kama ilivyozoeleka.
Saba, Kutokana na kasoro zilizoonekana hivi sasa ambapo Bunge limekuwa likijadili na kupitisha vitabu vya matumizi pekee na hata Kamati ya Fedha na Uchumi kutojadili Vitabu vya Mapato, na kutokana na uzoefu wa Mabunge mengine, Kambi ya Upinzani inapendekeza Bunge kuwa na Kamati ya Bajeti (Budget Committee) ambayo wajumbe wake watakuwa ni wenyeviti wa Kamati zote za kudumu za Bunge. Kamati ya Bajeti ndio itakuwa na jukumu la kupitia makadirio yote ya Mapato na Matumizi ya Serikali.
Nane, Kutokana na uzoefu tuliopata kutoka katika Mabunge mengine, Kambi ya Upinzani inapendekeza kuwa kwa vile Mheshimiwa Spika anatoa Maamuzi mengi ndani ya Bunge wakati umefika sasa wa Maamuzi hayo kuchapishwa rasmi katika umbo la Kitabu kurahisisha rejea ya Wabunge kuhusu mambo yaliyokwisha kuamuliwa ndani ya Bunge na wewe Mheshimiwa Spika, Naibu wako na Wenyeviti.
Mheshimiwa Spika,
Tisa, Kambi ya Upinzani Bungeni imefuatilia kwa karibu michango mbalimbali ya wabunge wakati wa wiki hii ya mjadala wa Bajeti.
Kambi imesikitishwa sana na mchango wa Mbunge mmoja jana aliposema kwamba Watendaji wa Serikali hawana nia njema na CCM na hivyo kumkwamisha Waziri wa Fedha.
Tabia ya sisi wanasiasa kupeleka lawama kwa watendaji kwa makosa ambayo sote twahusika ni tabia mbaya.
Kambi ya Upinzani ina imani kubwa na watendaji wa Serikali na tunawataka wafanye kazi zao bila upendeleo wa kiitikadi. Watendaji wote Serikalini, watanzania wazalendo endeleeni kuchapa kazi na mchukulie mchango wa Mheshimiwa Mbunge kama Waheshimiwa binafsi, Poleni sana.
Kumi, hatimaye naomba kuchukua nafasi hii kuwapongeza Wabunge wote wa Kambi ya Upinzani waliosimamia kidete
kurekebishwa kwa mapungufu haya na kuonyesha umuhimu wa Bunge kujadili Kitabu cha kwanza ili kutimiza matakwa ya Katiba, ibara ya 138.
Mheshimiwa Spika,
Kambi ya Upinzani ina imani na watendaji wote wa Serikali hasa tukielewa mazingira wanayofanyia kazi hiyo, natumaini kabisa kwamba mapungufu yaliyotokea, yalifanywa kwa nia ya kumuanguasha Waziri, ila ni hali halisi ya matatizo ya kuwa na vianzio vya uhakika na vya kutosha matumizi yetu. Tunaomba waendelee kujenga uadilifu wao kwa Taifa.
Aidha, namshukuru Mhe. Waziri wa Fedha na Uchumi, Mhe. Mustapha Mkullo, na Manaibu wake wote wawili na watendaji wao kwa jitihada kubwa waliyafanya kwanza kuuthamini mchango wa Kambi ya Upinzani na kukubali kuufanyia kazi ushauri wetu. Hii ndiyo roho inayotakiwa ya Wabunge kuthamini mchango mzuri upande wowote unakotoka.
Mwisho, kutokana na ushirikiano na unyofu alioonyesha Mheshimiwa Waziri na Manaibu wake, Kambi ya Upinzani, kwa kuzingatia maslahi ya Taifa, inampa nafasi na hivyo kufikiria kupitisha au kutokupitisha Bajeti hii itategemea maelezo ya kuridhisha kuhusiana na maeneo yote tuliyohoji katika hotuba zetu mbalimbali.
Mheshimiwa Spika baada ya kusema hayo naomba kuwasilisha.
...............................................................
Mhe. Hamad Rashid Mohamed (Mb)
KIONGOZI WA UPINZANI BUNGENI NA MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI WIZARA YA FEDHA NA UCHUMI
0.06.2008
MHE.HAMAD RASHID MOHAMED (MB) KUHUSU UTATA WA MAHESABU KATIKA KITABU CHA KWANZA CHA MAPATO YAANI “VOLUME 1 FINANCIAL STATEMENT AND REVENUE ESTIMATES” KWA MWAKA WA FEDHA WA FEDHA 2008/2009:
_____________________
UTANGULIZI
Mheshimiwa Spika,
Leo Asubuhi ulitoa mwongozo ulioombwa na Kambi ya Upinzani kuhusiana na kukiukwa kwa Kanuni ya 96(1) kuhusiana na matakwa ya kanuni hiyo kwamba “Waziri atapeleka kwa Katibu Makadirio ya Matumizi ya kawaida na ya maendeleo ya Serikali ya mwaka wa fedha unaohusika na nakala ya makadirio hayo itapelekwa na kumfikia kila mbunge angalau siku ishirini na moja kabla ya Mkutano ambao utashughulikia makadirio hayo” ulitoa mwongozo kuwa kuna utata katika kipengele hicho na kuagiza Kamati ya Fedha kupitia Kanuni hiyo na kupendekeza marekebisho stahiki.
Mheshimiwa Spika,
Kutokana na hoja zilizotolewa na Kambi ya Upinzani wakati wa majadala kuwa kuna mapungufu katika Takwimu za Kitabu cha Mapato, Serikali imewasilisha marekebisho ya Takwimu hizo.
Na kwa kuwa Takwimu za ziada zilizowasilishwa na Waziri leo asubuhi kwa njia ya “Addendum to Volume 1” kuonekana bado hazioani na Takwimu zilizoko kwenye Kitabu cha Hotuba ya Waziri uliagiza Kitabu hicho pamoja na Addendum kipitiwe na Kamati ya Fedha na Uchumi na baadaye Mwenyekiti wa Kamati husika na Kambi ya Upinzani tuitolee Taarifa ndani ya Bunge lako Tukufu.
Ninaomba kuchukua nafasi hii kutoa Taarifa kwa niaba ya Kambi ya Upinzani Bungeni.
Mheshimiwa Spika,
Moja, Kambi ya Upinzani imefarijika na unyofu wa Serikali wa kukubali kuwa kulikuwa na mapungufu na makosa ya Kitakwimu katika Kitabu cha kwanza cha Makadirio ya Mapato (Volume 1 cha Financial Statement and Revenue Estimates), na hivyo kuwasilisha Bungeni Nyongeza ya Marekebisho hayo,(Addendum to Volume l ).
Mbili, Mheshimiwa Waziri ameieleza Kamati ya Fedha kuwa mapungufu hayo yametokana na serikali kupata makisio ya awali ambayo miongoni mwake hayakuwa yamethibitishwa na vyombo vinavyochangia mapato ya serikali (Kwa mfano, katika Benki Kuu Serikali ilikisia sh 11 Bilioni lakini baade ikathibitika kuwa ni sh 6 Bilioni). Kambi ya Upinzani imeridhika na maelezo hayo isipokuwa kwamba kwa miaka ijayo kazi hiyo iwe imekamilika kabla ya Makadirio ya Mapato na Matumizi kuwasilishwa Bungeni, ili Bunge kwa niaba ya Wananchi liweze kupitisha jambo lililo na uhakika nalo.
Tatu, Baada ya maelezo ya Waziri wa Fedha na Uchumi, Kambi ya Upinzani imebaini kwamba utegemezi wa Bajeti ya Maendeleo kwa Wahisani bado ni mkubwa mno kwa kiwango cha asilimia 97.5. Hii maana yake ni kwamba tunafanya uchumi wa kuchumia Tumbo (Stomach economy). Kambi ya Upinzani inasisitiza kwamba vyanzo vya Mapato ilivyovibainisha katika Bajeti mbadala vifuatiliwe kikamilifu ili kupunguza utegemezi huu.
Nne, Kambi ya Upinzani bado inasikitishwa na kitendo cha Serikali ya Muungano kutogawa gawio sahihi kutokana na faida ya Benki Kuu kwenda Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa mujibu wa Kumbukumbu za IMF, ilikuwa inamiliki asilimia 11.5 ya Hisa za Benki Kuu (BOT). Hivyo kugawa gawio kwa asilimia 4.5 ni kuipunja Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kupata gawio sahihi kutokana na mtaji wake wakati Benki Kuu inaanza mwaka 1965 baada ya kuvunjwa kwa Bodi ya Sarafu ya Afrika ya Mashariki (East African Currency Board). Kambi ya Upinzani inaitaka Benki Kuu ya Tanzania igawe gawio kwa SMZ kwa mujibu wa hisa zake.
Mheshimiwa Spika,
Tano, Kambi ya Upinzani inasisitiza kuwa katika miaka ijayo Bunge lizingatie Ibara ya 138 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano inayotaja kuwa hakuna Kodi au tozo yeyote inayoweza kutozwa bila idhini ya Bunge au kwa mujibu wa Sheria ya iliyotungwa na Bunge.
Sita, Kambi ya Upinzani inaona upo muhimu pia kufanya marekebisho ya kifungu cha 96 cha Kanuni ya Bunge Toleo la 2007 ili kulifanya Bunge kujadili na kupitisha mapendekezo ya Mapato na Matumizi kama yanavyowasilishwa na Vitabu vyote vinne vya Bajeti badala ya kupitisha matumizi tu kama ilivyozoeleka.
Saba, Kutokana na kasoro zilizoonekana hivi sasa ambapo Bunge limekuwa likijadili na kupitisha vitabu vya matumizi pekee na hata Kamati ya Fedha na Uchumi kutojadili Vitabu vya Mapato, na kutokana na uzoefu wa Mabunge mengine, Kambi ya Upinzani inapendekeza Bunge kuwa na Kamati ya Bajeti (Budget Committee) ambayo wajumbe wake watakuwa ni wenyeviti wa Kamati zote za kudumu za Bunge. Kamati ya Bajeti ndio itakuwa na jukumu la kupitia makadirio yote ya Mapato na Matumizi ya Serikali.
Nane, Kutokana na uzoefu tuliopata kutoka katika Mabunge mengine, Kambi ya Upinzani inapendekeza kuwa kwa vile Mheshimiwa Spika anatoa Maamuzi mengi ndani ya Bunge wakati umefika sasa wa Maamuzi hayo kuchapishwa rasmi katika umbo la Kitabu kurahisisha rejea ya Wabunge kuhusu mambo yaliyokwisha kuamuliwa ndani ya Bunge na wewe Mheshimiwa Spika, Naibu wako na Wenyeviti.
Mheshimiwa Spika,
Tisa, Kambi ya Upinzani Bungeni imefuatilia kwa karibu michango mbalimbali ya wabunge wakati wa wiki hii ya mjadala wa Bajeti.
Kambi imesikitishwa sana na mchango wa Mbunge mmoja jana aliposema kwamba Watendaji wa Serikali hawana nia njema na CCM na hivyo kumkwamisha Waziri wa Fedha.
Tabia ya sisi wanasiasa kupeleka lawama kwa watendaji kwa makosa ambayo sote twahusika ni tabia mbaya.
Kambi ya Upinzani ina imani kubwa na watendaji wa Serikali na tunawataka wafanye kazi zao bila upendeleo wa kiitikadi. Watendaji wote Serikalini, watanzania wazalendo endeleeni kuchapa kazi na mchukulie mchango wa Mheshimiwa Mbunge kama Waheshimiwa binafsi, Poleni sana.
Kumi, hatimaye naomba kuchukua nafasi hii kuwapongeza Wabunge wote wa Kambi ya Upinzani waliosimamia kidete
kurekebishwa kwa mapungufu haya na kuonyesha umuhimu wa Bunge kujadili Kitabu cha kwanza ili kutimiza matakwa ya Katiba, ibara ya 138.
Mheshimiwa Spika,
Kambi ya Upinzani ina imani na watendaji wote wa Serikali hasa tukielewa mazingira wanayofanyia kazi hiyo, natumaini kabisa kwamba mapungufu yaliyotokea, yalifanywa kwa nia ya kumuanguasha Waziri, ila ni hali halisi ya matatizo ya kuwa na vianzio vya uhakika na vya kutosha matumizi yetu. Tunaomba waendelee kujenga uadilifu wao kwa Taifa.
Aidha, namshukuru Mhe. Waziri wa Fedha na Uchumi, Mhe. Mustapha Mkullo, na Manaibu wake wote wawili na watendaji wao kwa jitihada kubwa waliyafanya kwanza kuuthamini mchango wa Kambi ya Upinzani na kukubali kuufanyia kazi ushauri wetu. Hii ndiyo roho inayotakiwa ya Wabunge kuthamini mchango mzuri upande wowote unakotoka.
Mwisho, kutokana na ushirikiano na unyofu alioonyesha Mheshimiwa Waziri na Manaibu wake, Kambi ya Upinzani, kwa kuzingatia maslahi ya Taifa, inampa nafasi na hivyo kufikiria kupitisha au kutokupitisha Bajeti hii itategemea maelezo ya kuridhisha kuhusiana na maeneo yote tuliyohoji katika hotuba zetu mbalimbali.
Mheshimiwa Spika baada ya kusema hayo naomba kuwasilisha.
...............................................................
Mhe. Hamad Rashid Mohamed (Mb)
KIONGOZI WA UPINZANI BUNGENI NA MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI WIZARA YA FEDHA NA UCHUMI
0.06.2008
COMMENTS