TUKIO JINGINE KUBWA LA NDOVU SPECIAL MALT KWA WANATAALUMA Bia yadhamini mkutano wa wafanyabiashara na wanataaluma kwa Sh. milioni 5 Ndovu Sp...
TUKIO JINGINE KUBWA LA NDOVU SPECIAL MALT KWA WANATAALUMA
Bia yadhamini mkutano wa wafanyabiashara na wanataaluma kwa Sh. milioni 5
Ndovu Special Malt yaendelea kuunga mkono wafanyabiashara
Udhamini ni katika mfululizo wa kuhusika kwa bia hiyo na matukio ya wanataaluma
Dar es Salaam: Ndovu Special Malt, moja ya bia maarufu nchini kwa mara nyingine tena inaendeleza ushirikiano wake na jumuiya ya wafanyabiashara nchini kwa kudhamini mkutano wa pili wa wafanyabiashara ujulikanao kama The 2nd Grand Networking After Dinner Talk 2008 ambao umeandaliwa kwa pamoja na Shirikisho la Wenye Viwanda Tanzania (CTI) na Baraza la Wahutubu la Afrika Mashariki (ESB).
Katika udhamini wake kwa mkutano wa mwaka huu, Ndovu Special Malt imetoa jumla ya Sh. milioni 5, fedha ambazo zitatumika katika maandalizi na uendeshaji wa mkutano huo pamoja na mipango mingine ya kuuendeleza.
Akizungumza wakati wa kukabidhi hundi ya udhamini huo kwa CTI, Meneja wa Bia ya Ndovu Special Malt Mpeli Nsekela alisema, “Sisi Ndovu Special Malt tunajivunia sana kuhusika na jumuiya ya wafanyabiashara hapa nchini. Tunafahamu fika mchango wa jumuiya hii kwa uchumi wetu na nchi nzima kwa ujumla ndiyo maana tumeamua kushirikiana na CTI na ESB katika tukio hili kubwa. Udhamini huu unasimika rekodi ya Ndovu Special Malt ya kushiriki katika matukio ya kibiashara ambapo wanataaluma mbalimbali wanakutana kubadilishana mawazo na kujenga mikakati.”
Ndovu Special Malt, ambayo kwa kawaida inapendelewa na watu wenye mtazamo wa kitaaluma, tayari imefanikisha matukio kadhaa yaliyowakutanisha wafanyabiashara na wanataaluma wengine yakiwemo udhamini wa miezi 9 wa Mkutano wa British Council wa Wakurugenzi, Warsha ya CTI ya Wanawake na Ujasiriamali, Chakula cha Jioni cha Taasisi ya Wahandisi, mikutano ya Mtandao wa Wanataaluma wa Tanzania na Usiku wa Wanamasoko ambao hufanyika mara nne kwa mwaka.
Mkutano huo utakaofanyika kwenye hoteli ya Movenpick Royal Palm jijini Dar es Salaam Ijumaa Novemba 21 utawakutanisha pamoja wafanyabiashara wakubwa, wakurugenzi watendaji, maofisa wa Serikali, wanadiplomasia, mameneja, wajasiriamali, wanataaluma mbalimbali na wadau wengineo. Mkutano huo utahutubiwa na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Mhe. Balozi Juma Mwapachu na Mwenyekiti wa Kampuni ya Uwekezaji ya Taifa (NICOL) Felix G. N. Mosha.
Ndovu Special Malt inatengenezwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL).
Bia yadhamini mkutano wa wafanyabiashara na wanataaluma kwa Sh. milioni 5
Ndovu Special Malt yaendelea kuunga mkono wafanyabiashara
Udhamini ni katika mfululizo wa kuhusika kwa bia hiyo na matukio ya wanataaluma
Dar es Salaam: Ndovu Special Malt, moja ya bia maarufu nchini kwa mara nyingine tena inaendeleza ushirikiano wake na jumuiya ya wafanyabiashara nchini kwa kudhamini mkutano wa pili wa wafanyabiashara ujulikanao kama The 2nd Grand Networking After Dinner Talk 2008 ambao umeandaliwa kwa pamoja na Shirikisho la Wenye Viwanda Tanzania (CTI) na Baraza la Wahutubu la Afrika Mashariki (ESB).
Katika udhamini wake kwa mkutano wa mwaka huu, Ndovu Special Malt imetoa jumla ya Sh. milioni 5, fedha ambazo zitatumika katika maandalizi na uendeshaji wa mkutano huo pamoja na mipango mingine ya kuuendeleza.
Akizungumza wakati wa kukabidhi hundi ya udhamini huo kwa CTI, Meneja wa Bia ya Ndovu Special Malt Mpeli Nsekela alisema, “Sisi Ndovu Special Malt tunajivunia sana kuhusika na jumuiya ya wafanyabiashara hapa nchini. Tunafahamu fika mchango wa jumuiya hii kwa uchumi wetu na nchi nzima kwa ujumla ndiyo maana tumeamua kushirikiana na CTI na ESB katika tukio hili kubwa. Udhamini huu unasimika rekodi ya Ndovu Special Malt ya kushiriki katika matukio ya kibiashara ambapo wanataaluma mbalimbali wanakutana kubadilishana mawazo na kujenga mikakati.”
Ndovu Special Malt, ambayo kwa kawaida inapendelewa na watu wenye mtazamo wa kitaaluma, tayari imefanikisha matukio kadhaa yaliyowakutanisha wafanyabiashara na wanataaluma wengine yakiwemo udhamini wa miezi 9 wa Mkutano wa British Council wa Wakurugenzi, Warsha ya CTI ya Wanawake na Ujasiriamali, Chakula cha Jioni cha Taasisi ya Wahandisi, mikutano ya Mtandao wa Wanataaluma wa Tanzania na Usiku wa Wanamasoko ambao hufanyika mara nne kwa mwaka.
Mkutano huo utakaofanyika kwenye hoteli ya Movenpick Royal Palm jijini Dar es Salaam Ijumaa Novemba 21 utawakutanisha pamoja wafanyabiashara wakubwa, wakurugenzi watendaji, maofisa wa Serikali, wanadiplomasia, mameneja, wajasiriamali, wanataaluma mbalimbali na wadau wengineo. Mkutano huo utahutubiwa na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Mhe. Balozi Juma Mwapachu na Mwenyekiti wa Kampuni ya Uwekezaji ya Taifa (NICOL) Felix G. N. Mosha.
Ndovu Special Malt inatengenezwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL).
Pichani:CTI Business Development Services Dir. Cecilia Chambaka (r) speaks to the media during Ndovu Special Malt's presentation of the sponsorship cheque to CTI. Left is Ndovu Special Malt Brand Manager Mpeli Nsekela
COMMENTS