HOTUBA YA KATIBU MKUU WA WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII, BIBI BLANDINA NYONI KATIKA UFUNGAJI WA KONGAMANO LASABA LA WAANDISHI NA WAANDISH...
HOTUBA YA KATIBU MKUU WA WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII, BIBI BLANDINA NYONI KATIKA UFUNGAJI WA KONGAMANO LASABA LA WAANDISHI NA WAANDISHI WAANDAMIZI LILIOFANYIKA TAREHE 28 HADI 29, 2011, MOROGORO.
• Mwenyekiti wa Kongamano Bw. Lauden Mwambona
• Makamu wa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHFI), Bw. Kiwenge Ally Kiwenge,
• Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Bw. Emanuel Humba,
• Wajumbe wa Bodi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya,
• Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Bw. Hamis Mdee,
• Wakurugenzi, Mameneja na Watumishi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya,
• Wawakilishi wa Taasisi dada zilizo chini ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii,
• Waratibu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya na Mfuko wa Afya ya Jamii wa Mkoawa Morogoro,
• Ndugu wana habari,
• Wageni Waalikwa,
• Mabibi na Mabwana
Asalam Aleikum, Bwana Yesu Asifiwe.
Shukrani:
Ndugu Mwenyekiti wa Kongamano, Wajumbe wa Bodi ya Mfuko, Viongozi, Wahariri na Waandishi. Nianze kwa kutoa shukrani za dhati kwa kunialika kufunga Kongamano hili muhimu la Wahahari na Waandishi wa Habari ambalo lililenga kupata mrejesho kuhusu Hali halisi ya huduma za matibabu zinatotolew kupitia NHIF na CHF huko vijijini.
Utaratibu mliotumia wa kuwapa nafasi wanahabari kwenda vijijini ni mzuri na ningefurahi kuona unaendelezwa na kuigwa na taasisi nyingine pia. Kwa kuzingatia umuhimu wa kongamano hili, Wizara iliwaleta maafisa wake waandamizi ambao mmekuwa nao tangu jana na pia iliwasisitiza kuwepo na uwakilishi wa Taasisi zilizo chini ya Wizara. Nashukuru kwamba wote wamehudhuria kama tulivyoelekeza.
Taarifa za Utafiti na Majadiliano:
Ndugu Mwenyekiti na ndugu Wanahabari, nimetaarifiwa pia mmekuwa na kikao kizuri na mmejadili kwa kina masuala muhimu yanayogusa maeneo mbalimbali muhimu ikiwa ni pamoja na suala zima la upatikanaji wa dawa, hali ya vituo vya matibabu, matumizi ya fedha zinazotokana na mifuko ya uchangiaji, maadili ya watoa huduma, miundombinu na kadhalika.
Napenda niwashukuru nyote. mliofanya utafiti na nyote milioshiriki kikao hiki kwa kuchangia mada mbalimbali. Michango yenu imesaidia kuibua masuala na maeneo yanayokwamisha maendeleo ya sekta ya afya hasa utekelezaji wa Sera ya Mabadiliko katika Sekta ya Afya.
Ni dhahiri kuwa sekta ya afya inakabiliwa na jukumu kubwa la kutoa huduma bora za matibabu kwa wananchi hasa maeneo ya vijijini. Nina imani na matumaini makubwa kuwa kwa ushirikiano ambao mmekuwa mkiutoa kwa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, tunaweza kabisa kuzipunguza (kama si kuzimaliza) baadhi ya changamoto zilizo ndani ya uwezo wetu. mfano suala la matumizi ya fedha zinazotokana na uchangiaji huduma za matibabu ngazi ya Halmashauri ambalo
Suala la upatikanaji wa dawa:
Ndugu Mwenyekiti na ndugu wanahabari, bila shaka kila mmoja wetu ameshuhudia mwenyewe jinsi gani suala la usimamizi na upatikanaji wa huduma ya dawa katika baadhi ya vituo vya matibabu linavyokatisha tamaa siyo tu wanachama wa NHIF na CHF, lakini Watanzania kwa ujumla. Hili ni suala ambalo sisi kama Serikali kwa upande wetu tunalitambua na tunalifanyia kazi katika maeneo yafuatayo:-
• Tunaendelea kuiimarisha Bohari Kuu ya Dawa (MSD) ambayo ni chombo cha kimkakati cha Serikali.
• Tunaihimiza Sekta Binafsi washiriki katika kuagiza dawa na kufungua maduka ya dawa za Moto na Dawa Muhimu hasa vijijini, maeneo ambayo huduma hiyo inahitajika sana na kuna wanachama wengi wa Bima ya Afya;
• Tumeongeza kasi ya kusambaza kwa Maduka ya Dawa Muhimu (DLDM) kupitia Mamlaka ya Chakula na Dawa nchini (TFDA) na kuuagiza Mfuko wa Bima ya Afya kuyasajili maduka hayo kila mara TFDA watakapokuwa wamemaliza kuyaidhinisha;
• Tulikwisha toa tamko Bungeni (wakati wa Bunge la Bajeti) kuwa fedha kiasi cha theluthi mbili (2/3) ya fedha zote zinazotokana na mifuko ya uchangiaji ya NHIF, CHF na Papo kwa Papo zitumike kununulia dawa. Kazi yetu sisi na nyingi iwe ni kuona azma hiyo inatekelezwa kwa vitendo ili wananchi wengi wanufaike na huduma hii.
• Kupitia MSD tumeanza utaratibu wa usambazaji wa Dawa hadi vituoni kule Tanga. Matarajio yetu ni kuona ni kwa namna gani utaratibu huu unaweza kuendelezwa kwa ufanisi katika mikoa mingine. Tuliamua katika mwaka huu wa fedha tuchukue mkoa mmoja kwa kila kanda.
Tunaamini kuwa hatua hiyo itasogeza karibu zaidi hudma za usambazaji wa dawa na hivyo kupunguza kero ya ukosefu wa dawa katika vituo vya matibabu. Tunawaomba wananchi na ninyi wanahabari kuwa macho na kuwa walinzi wa dawa hasa za Serikali ili zisivuje vituoni na kuangukia mikononi mwa watu wasio tutakia mema. Sisi kama Wizara tuko tayari kushirikiana na mwananchi yoyote katika suala hili. Kamati za Afya ziimarishwe ili wawe wasimamizi wa huduma za dawa maeneo yao.
Ubovu wa Miundo mbinu:
Ndugu Mwenyekiti, nimetaarifiwa pia Katika baadhi ya makala tulizozionanjana na leo zinaonyesha wazi kuwa hali ya vituo vya kutolea huduma ni mbaya, na kwa kweli kwa namna moja au nyingine hali hiyo inasababuisha hata wananchi wachache wanaokatwa mishahara yao kwa ajili ya NHIF na wale wanaochangia katika Mfuko wa Afya ya Jamii wakate tamaa ya kuendelea kuchangia. Hili nalo tutalifanyia kazi kupitia utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo wa Afya ya Msingi (MMAM) ili kuhakikisha kuwa kila kituo kinakuwa na hadhi inayostahili.
Katibu Mkuu akiongea leo jioni morogoro
Maadili ya Watumishi wa Sekta ya Afya:
Suala la maadili ya watendaji wa vituo vya matibabu mmelitaja katika taarifa zenu kama eneo lenye changamoto. Wito wangu kwenu na kwa wananchi wote ni kuwa watumishi wachache wasiofuata maadili wabainishwe ili hatua za kinidhamu zichukuliwe. Inawezekana kabisa watumishi hao wachache wanaweza kuathiri vibaya juhudi za Serikali za kutoa huduma bora kwa wananchi. Ni vyema pia pale watumishi wengine wanapofanya vizuri pia tutambue mchango wao. Si vizuri pia wananchi au wanachama wa Mfuko wa NHIF au wa CHF kuwa chanzo cha malumbano katika vituo vya matibabu. Hivyo wakati tunahimiza suala la maadili kwa Watumishi wa Sekta ya Afya ni vyema vilevile wananchi kwa upande mwingine wakazingatia maadili na ushauri wa kitaalamu kutoka kwa watumishi wa sekta hii.
Suala la Elimu kwa Umma
Ndugu Mwenyekiti, tatizo kubwa linalochangia utekelezaji mdogo wa Sera na Miongozo ya Serikali ni elimu kwa walengwa. Kama mmesikiliza kwa umakini hoja zilizowasilishwa katika Kongamano hili nyingi zinabainsha uhaba wa elimu kuhusu Sera au huduma za NHIF au CHF kwa walengwa. Kukwama au kufanikiwa kwa utekelezaji wa mipango ya NHIF na CHF kunategemeana sana na uelewa wa wananchi kuhusu shughuli hizo. Naomba kwa kushurikiana na Idara nyingine zilizo chini ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii wekeni mikakati ya pamoja ya kuelimisha umma kuhusu haki na wajibu wa mdau ili linaptokea tatizo wananchi wajue ni nani wa kumwelekeea kidole.
Utafiti wa pamoja:
Napenda kumaliza kwa kusema kuwa baada ya kusikiliza taarifa hizi za utafiti, mimi nafikiri kuwa kuna haja ya kuwa na mkakati wa pamoja wa kufanya tafiti za mara kwa mara kwa kuwatumia wana habari ili tufikie mahali ambapo tunaweza kusema kwa uhakika kuwa changamoto za sekta ya afya zinafahaika na zinawekewa mikakati na nguvu za pamoja za kuzitatua.
Hitimisho:
Baada ya kusema hayo naomba sasa nitamke kuwa Kongamano letu la siku mbili limefungwa rasmi.
Asanteni kwa kunisikiliza.
• Mwenyekiti wa Kongamano Bw. Lauden Mwambona
• Makamu wa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHFI), Bw. Kiwenge Ally Kiwenge,
• Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Bw. Emanuel Humba,
• Wajumbe wa Bodi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya,
• Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Bw. Hamis Mdee,
• Wakurugenzi, Mameneja na Watumishi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya,
• Wawakilishi wa Taasisi dada zilizo chini ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii,
• Waratibu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya na Mfuko wa Afya ya Jamii wa Mkoawa Morogoro,
• Ndugu wana habari,
• Wageni Waalikwa,
• Mabibi na Mabwana
Asalam Aleikum, Bwana Yesu Asifiwe.
Shukrani:
Ndugu Mwenyekiti wa Kongamano, Wajumbe wa Bodi ya Mfuko, Viongozi, Wahariri na Waandishi. Nianze kwa kutoa shukrani za dhati kwa kunialika kufunga Kongamano hili muhimu la Wahahari na Waandishi wa Habari ambalo lililenga kupata mrejesho kuhusu Hali halisi ya huduma za matibabu zinatotolew kupitia NHIF na CHF huko vijijini.
Utaratibu mliotumia wa kuwapa nafasi wanahabari kwenda vijijini ni mzuri na ningefurahi kuona unaendelezwa na kuigwa na taasisi nyingine pia. Kwa kuzingatia umuhimu wa kongamano hili, Wizara iliwaleta maafisa wake waandamizi ambao mmekuwa nao tangu jana na pia iliwasisitiza kuwepo na uwakilishi wa Taasisi zilizo chini ya Wizara. Nashukuru kwamba wote wamehudhuria kama tulivyoelekeza.
Taarifa za Utafiti na Majadiliano:
Ndugu Mwenyekiti na ndugu Wanahabari, nimetaarifiwa pia mmekuwa na kikao kizuri na mmejadili kwa kina masuala muhimu yanayogusa maeneo mbalimbali muhimu ikiwa ni pamoja na suala zima la upatikanaji wa dawa, hali ya vituo vya matibabu, matumizi ya fedha zinazotokana na mifuko ya uchangiaji, maadili ya watoa huduma, miundombinu na kadhalika.
Napenda niwashukuru nyote. mliofanya utafiti na nyote milioshiriki kikao hiki kwa kuchangia mada mbalimbali. Michango yenu imesaidia kuibua masuala na maeneo yanayokwamisha maendeleo ya sekta ya afya hasa utekelezaji wa Sera ya Mabadiliko katika Sekta ya Afya.
Ni dhahiri kuwa sekta ya afya inakabiliwa na jukumu kubwa la kutoa huduma bora za matibabu kwa wananchi hasa maeneo ya vijijini. Nina imani na matumaini makubwa kuwa kwa ushirikiano ambao mmekuwa mkiutoa kwa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, tunaweza kabisa kuzipunguza (kama si kuzimaliza) baadhi ya changamoto zilizo ndani ya uwezo wetu. mfano suala la matumizi ya fedha zinazotokana na uchangiaji huduma za matibabu ngazi ya Halmashauri ambalo
Suala la upatikanaji wa dawa:
Ndugu Mwenyekiti na ndugu wanahabari, bila shaka kila mmoja wetu ameshuhudia mwenyewe jinsi gani suala la usimamizi na upatikanaji wa huduma ya dawa katika baadhi ya vituo vya matibabu linavyokatisha tamaa siyo tu wanachama wa NHIF na CHF, lakini Watanzania kwa ujumla. Hili ni suala ambalo sisi kama Serikali kwa upande wetu tunalitambua na tunalifanyia kazi katika maeneo yafuatayo:-
• Tunaendelea kuiimarisha Bohari Kuu ya Dawa (MSD) ambayo ni chombo cha kimkakati cha Serikali.
• Tunaihimiza Sekta Binafsi washiriki katika kuagiza dawa na kufungua maduka ya dawa za Moto na Dawa Muhimu hasa vijijini, maeneo ambayo huduma hiyo inahitajika sana na kuna wanachama wengi wa Bima ya Afya;
• Tumeongeza kasi ya kusambaza kwa Maduka ya Dawa Muhimu (DLDM) kupitia Mamlaka ya Chakula na Dawa nchini (TFDA) na kuuagiza Mfuko wa Bima ya Afya kuyasajili maduka hayo kila mara TFDA watakapokuwa wamemaliza kuyaidhinisha;
• Tulikwisha toa tamko Bungeni (wakati wa Bunge la Bajeti) kuwa fedha kiasi cha theluthi mbili (2/3) ya fedha zote zinazotokana na mifuko ya uchangiaji ya NHIF, CHF na Papo kwa Papo zitumike kununulia dawa. Kazi yetu sisi na nyingi iwe ni kuona azma hiyo inatekelezwa kwa vitendo ili wananchi wengi wanufaike na huduma hii.
• Kupitia MSD tumeanza utaratibu wa usambazaji wa Dawa hadi vituoni kule Tanga. Matarajio yetu ni kuona ni kwa namna gani utaratibu huu unaweza kuendelezwa kwa ufanisi katika mikoa mingine. Tuliamua katika mwaka huu wa fedha tuchukue mkoa mmoja kwa kila kanda.
Tunaamini kuwa hatua hiyo itasogeza karibu zaidi hudma za usambazaji wa dawa na hivyo kupunguza kero ya ukosefu wa dawa katika vituo vya matibabu. Tunawaomba wananchi na ninyi wanahabari kuwa macho na kuwa walinzi wa dawa hasa za Serikali ili zisivuje vituoni na kuangukia mikononi mwa watu wasio tutakia mema. Sisi kama Wizara tuko tayari kushirikiana na mwananchi yoyote katika suala hili. Kamati za Afya ziimarishwe ili wawe wasimamizi wa huduma za dawa maeneo yao.
Ubovu wa Miundo mbinu:
Ndugu Mwenyekiti, nimetaarifiwa pia Katika baadhi ya makala tulizozionanjana na leo zinaonyesha wazi kuwa hali ya vituo vya kutolea huduma ni mbaya, na kwa kweli kwa namna moja au nyingine hali hiyo inasababuisha hata wananchi wachache wanaokatwa mishahara yao kwa ajili ya NHIF na wale wanaochangia katika Mfuko wa Afya ya Jamii wakate tamaa ya kuendelea kuchangia. Hili nalo tutalifanyia kazi kupitia utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo wa Afya ya Msingi (MMAM) ili kuhakikisha kuwa kila kituo kinakuwa na hadhi inayostahili.
Katibu Mkuu akiongea leo jioni morogoro
Maadili ya Watumishi wa Sekta ya Afya:
Suala la maadili ya watendaji wa vituo vya matibabu mmelitaja katika taarifa zenu kama eneo lenye changamoto. Wito wangu kwenu na kwa wananchi wote ni kuwa watumishi wachache wasiofuata maadili wabainishwe ili hatua za kinidhamu zichukuliwe. Inawezekana kabisa watumishi hao wachache wanaweza kuathiri vibaya juhudi za Serikali za kutoa huduma bora kwa wananchi. Ni vyema pia pale watumishi wengine wanapofanya vizuri pia tutambue mchango wao. Si vizuri pia wananchi au wanachama wa Mfuko wa NHIF au wa CHF kuwa chanzo cha malumbano katika vituo vya matibabu. Hivyo wakati tunahimiza suala la maadili kwa Watumishi wa Sekta ya Afya ni vyema vilevile wananchi kwa upande mwingine wakazingatia maadili na ushauri wa kitaalamu kutoka kwa watumishi wa sekta hii.
Suala la Elimu kwa Umma
Ndugu Mwenyekiti, tatizo kubwa linalochangia utekelezaji mdogo wa Sera na Miongozo ya Serikali ni elimu kwa walengwa. Kama mmesikiliza kwa umakini hoja zilizowasilishwa katika Kongamano hili nyingi zinabainsha uhaba wa elimu kuhusu Sera au huduma za NHIF au CHF kwa walengwa. Kukwama au kufanikiwa kwa utekelezaji wa mipango ya NHIF na CHF kunategemeana sana na uelewa wa wananchi kuhusu shughuli hizo. Naomba kwa kushurikiana na Idara nyingine zilizo chini ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii wekeni mikakati ya pamoja ya kuelimisha umma kuhusu haki na wajibu wa mdau ili linaptokea tatizo wananchi wajue ni nani wa kumwelekeea kidole.
Utafiti wa pamoja:
Napenda kumaliza kwa kusema kuwa baada ya kusikiliza taarifa hizi za utafiti, mimi nafikiri kuwa kuna haja ya kuwa na mkakati wa pamoja wa kufanya tafiti za mara kwa mara kwa kuwatumia wana habari ili tufikie mahali ambapo tunaweza kusema kwa uhakika kuwa changamoto za sekta ya afya zinafahaika na zinawekewa mikakati na nguvu za pamoja za kuzitatua.
Hitimisho:
Baada ya kusema hayo naomba sasa nitamke kuwa Kongamano letu la siku mbili limefungwa rasmi.
Asanteni kwa kunisikiliza.
COMMENTS