WAKATI Waziri Mkuu anaandaa waraka kwa halmashauri zote kumaliza tatizo la madawati katika shule za msingi mwaka huu, serikali imesema seh...
WAKATI Waziri Mkuu anaandaa waraka kwa halmashauri zote kumaliza tatizo la madawati katika shule za msingi mwaka huu, serikali imesema sehemu kubwa ya fedha sh bilioni 18 za rada zitatumika kwa ajili kusaidia kuondoa tatizo hilo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Wazirik Mkuu, tawala za mikoa na serikali za mitaa,(Tamisemi) George Mkuchika alisema hayo wakati akijibu swali la nyongeza la mbunge wa Kibakwe George Simbachawene ( CCM ) mbaye alisema halmashauri ndizo zinazoendesha shule hizo na hali inaonekana kuwa mbaya.
Mkuchika alisema Waraka huo utakaosambazwa utaelekeza moja kwa moja nini kinatakiwa kufanywa na Halmashauri kumalzia tatizo la madfawati moja kwa moja.
Mkuchika pia alisema kwamba shughuli hiyo itamalziwa kwa fedha kutoka serikalini, Hazina (fedha za Rada) na kwa wananchi wenyewe ambao amesema ndio wenye shule.
Alisema shule za msingi ni mali ya vijiji na shule za kata (sekondari ) ni mali za kata kwa hiyo zinahitaji nguvu za pamojna na serikali kuliondoa tatizo hilo mara moja.
Alishauri wananchi kuongez anguvu kuchangia nafasi yao kuhakikisha kwamba tatizo hilo linamalizika kw amanufaa ya taifa zima.
Wakati akimalizia kuzungumzia suala hilo spika wa Bunge Anne Makinda alichombeza kwamba shughuli hasa za kujenga choo ni za wananchi na wala si serikali kuu au ya mitaa.
Katika maswalim mengine ya nyongeza kuhusu tatizo madawati wapo wabunge waliotaka kuwepo na kibali cha kuvuna miti ili kutengeneza madawati ambapo walijibiwa kwamba inaruhusiwa kwa kutumia taratibu zilizowekwa za uvunaji wa misitu.
Awali Martha Mlata alizungumzia haja ya fedha za rada kuingizwa kuondoa tatizo hilo kwa kuzipa zabuni taasisi za umma kama magereza na JKT kutengeneza samani hizo muhimu kwa shule zetu.
Awali Naibu waziri, Ofisi ya waziri Mkuu tawala za mikoa, Kassim Majaliwa akijibu swali la msingi la tatizo la madawati nchini lililoulizwa na mbunge wa Musoma Vijijini ,Vicent Nyerere (chadema) kuwa serikali imejipanga vipi kumaliza tatizo hilo, alisema kwamba dawati kama kifaa muhimu kuongeza ufanisi wa kujifunza lifanyiwa kazi.
Alisema kwamba kwa mwaka wa fedha wa 2009/2010 serikali ilitoa sh bilioni 1 kwa ajili ya ununuzi wa madawati kwa shule za sekondari na mwaka 2010/2011 ilitoa sh bilioni 3 kwa ajili ya ununuzi wa madawati shule za msingi.
Hata hivyo alisisitiza kwamba serikali kupitia Halmashauri nchini imekuwa ikielekeza utaratibu wa kuhakikisha kuwa kunakuwepo na mikakati ya kupunguza tatizo la madawati kwa wanafunzi kwa kuhusisha wadau mbalimbali.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Wazirik Mkuu, tawala za mikoa na serikali za mitaa,(Tamisemi) George Mkuchika alisema hayo wakati akijibu swali la nyongeza la mbunge wa Kibakwe George Simbachawene ( CCM ) mbaye alisema halmashauri ndizo zinazoendesha shule hizo na hali inaonekana kuwa mbaya.
Mkuchika alisema Waraka huo utakaosambazwa utaelekeza moja kwa moja nini kinatakiwa kufanywa na Halmashauri kumalzia tatizo la madfawati moja kwa moja.
Mkuchika pia alisema kwamba shughuli hiyo itamalziwa kwa fedha kutoka serikalini, Hazina (fedha za Rada) na kwa wananchi wenyewe ambao amesema ndio wenye shule.
Alisema shule za msingi ni mali ya vijiji na shule za kata (sekondari ) ni mali za kata kwa hiyo zinahitaji nguvu za pamojna na serikali kuliondoa tatizo hilo mara moja.
Alishauri wananchi kuongez anguvu kuchangia nafasi yao kuhakikisha kwamba tatizo hilo linamalizika kw amanufaa ya taifa zima.
Wakati akimalizia kuzungumzia suala hilo spika wa Bunge Anne Makinda alichombeza kwamba shughuli hasa za kujenga choo ni za wananchi na wala si serikali kuu au ya mitaa.
Katika maswalim mengine ya nyongeza kuhusu tatizo madawati wapo wabunge waliotaka kuwepo na kibali cha kuvuna miti ili kutengeneza madawati ambapo walijibiwa kwamba inaruhusiwa kwa kutumia taratibu zilizowekwa za uvunaji wa misitu.
Awali Martha Mlata alizungumzia haja ya fedha za rada kuingizwa kuondoa tatizo hilo kwa kuzipa zabuni taasisi za umma kama magereza na JKT kutengeneza samani hizo muhimu kwa shule zetu.
Awali Naibu waziri, Ofisi ya waziri Mkuu tawala za mikoa, Kassim Majaliwa akijibu swali la msingi la tatizo la madawati nchini lililoulizwa na mbunge wa Musoma Vijijini ,Vicent Nyerere (chadema) kuwa serikali imejipanga vipi kumaliza tatizo hilo, alisema kwamba dawati kama kifaa muhimu kuongeza ufanisi wa kujifunza lifanyiwa kazi.
Alisema kwamba kwa mwaka wa fedha wa 2009/2010 serikali ilitoa sh bilioni 1 kwa ajili ya ununuzi wa madawati kwa shule za sekondari na mwaka 2010/2011 ilitoa sh bilioni 3 kwa ajili ya ununuzi wa madawati shule za msingi.
Hata hivyo alisisitiza kwamba serikali kupitia Halmashauri nchini imekuwa ikielekeza utaratibu wa kuhakikisha kuwa kunakuwepo na mikakati ya kupunguza tatizo la madawati kwa wanafunzi kwa kuhusisha wadau mbalimbali.
COMMENTS