Mshambuliaji Thomas Ulimwengu ambaye ndiye mchezaji pekee kutoka nje aliyeitwa na Kocha Kim Poulsen kwenye U20 (Ngorongoro Heroes) a...
Mshambuliaji Thomas Ulimwengu ambaye ndiye
mchezaji pekee kutoka nje aliyeitwa na
Kocha Kim Poulsen kwenye U20 (Ngorongoro Heroes)
anatarajia kujiunga na kikosi hicho
ambacho kiko kambini kesho (Aprili 14 mwaka huu).
Ulimwengu
ambaye anachezea timu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo
(DRC) atawasili saa 1.20 usiku kwa ndege ya Kenya
Airways akitokea jijini
Lubumbashi.
Ngorongoro
Heroes ambayo iliingia kambini Aprili 20 mwaka huu inajiandaa kwa mechi
ya mashindano ya Afrika kwa vijana wenye umri
chini ya miaka 20 dhidi ya Sudan.
Mechi hiyo itachezwa Aprili 21 mwaka huu kwenye
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam
kuanzia saa 10 kamili jioni.
Kwa mujibu
wa Kocha Poulsen, kikosi chake kesho (Aprili 14 mwaka huu) kitakuwa na
awamu (sessions) mbili za mazoezi kwenye Uwanja wa
Karume. Awali ya kwanza itakuwa
asubuhi nay a pili itafanyika jioni.
Wachezaji
wengine walioko kwenye kikosi hicho cha Ngorongoro Heroes ni Saleh
Malande, Aishi Manula, Hassan Kessy, Said Ruhava,
Carlos Kilenge, Dizzana Issa,
Amani Kyata, Issa Rashid, Emily Mgeta na Khamis
Mroki.
Wengine ni
Ramadhan Singano, Frank Sekule, Frank Domayo, Omega Seme, Abdallah
Hussein, Ibrahim Rajab, Hassan Dilunga, Alhaje
Zege, Jerome Lambele, Atupele Green
na Simon Msuvan. Mechi ya marudiano dhidi ya Sudan
itachezwa jijini Khartoum kati ya
Mei 4, 5 na 6 mwaka huu.
Fainali za Afrika kwa vijana zitafanyika Machi
mwakani nchini Algeria. Timu nne za
juu kwenye fainali hizo zitacheza Fainali za Dunia
zitakazofanyika nchini Uturuki
kuanzia Juni hadi Julai mwakani.
LIGI KUU YAINGIA RAUNDI YA 23
Raundi ya 23 ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) inaingia
raundi ya 23 kesho (Aprili 14
mwaka huu) kwa mechi nne. Polisi Dodoma
wataikaribisha Azam kwenye Uwanja wa
Jamhuri, mjini Dodoma wakati JKT Ruvu watakuwa
wageni wa Mtibwa Sugar mjini Turiani.
Mechi
nyingine za raundi hiyo zitakuwa kati ya Kagera Sugar na African Lyon
zitakazooneshana kazi kwenye Uwanja wa Kaitaba
mjini Bukoba. Nayo Moro United
inaikaribisha Oljoro JKT katika mechi
itakayofanyika Uwanja wa Chamazi, Dar es
Salaam.
Raundi ya
23 itakamilika Jumapili (Aprili 15 mwaka huu) kwa mechi kati ya Ruvu
Shooting na Simba itakayochezwa Uwanja wa Taifa,
Dar es Salaam wakati Yanga itakuwa
mgeni wa Toto Africans kwenye Uwanja wa CCM
Kirumba, jijini Mwanza. Villa Squad
itapambana na Coastal Union kwenye Uwanja wa
Chamazi, Dar es Salaam.
Ligi hiyo
itaendelea tena Aprili 18 mwaka huu kwa mechi tano. Kagera Sugar vs Yanga
mjini Bukoba, Toto Africans vs African Lyon jijini
Mwanza, JKT Ruvu vs Simba- Uwanja
wa Taifa, Dar es Salaam, Ruvu Shooting vs Moro
United mjini Mlandizi na Polisi
Dodoma vs Coastal Union mjini Dodoma.
BONGO MOVIE KUICHANGIA TWIGA STARS
Timu ya Taifa ya mpira wa miguu kwa wanawake
(Twiga Stars) itacheza mechi ya
kirafiki na timu ya wasanii wa filamu ya Bongo
Movie itakayofanyika Jumamosi (Aprili
14 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Lengo la mechi hiyo ya maonesho (exhibition) ni
kuichangia Twiga Stars ambayo hivi
sasa iko kwenye mashindano ya mchujo ya Kombe la
Afrika kwa Wanawake (AWC) ambayo
fainali zake zitafanyika Novemba mwaka huu nchini
Equatorial Guinea.
Pia
asilimia mbili ya mapato yatakayopatikana kwenye mechi ya Twiga Stars na Bongo
Movie yatakwenda kwenye familia ya mwigizaji nguli
wa filamu Tanzania, Stephen
Kanumba aliyefariki dunia Aprili 7 mwaka huu.
Kiingilio
katika mechi hiyo kitakuwa sh. 10,000 kwa VIP A, sh. 5,000 kwa VIP C na B
na sh. 2,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, kijani
na bluu. Mechi itaanza saa 10
kamili jioni.
Machi 10
mwaka huu, Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk.
Fenella Mukangara alizindua akaunti ya Twiga Stars
kupitia Tigo Pesa kuichangia timu
hiyo ambayo inashiriki michuano ya AWC.
Wachangiaji wanatakiwa kutuma mchango wao
kwenda namba 13389.
RUFANI YA YANGA KWA TIBAIGANA
Kikao cha Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira
wa Miguu Tanzania (TFF)
kilichokuwa kifanyike kesho (Aprili 14 mwaka huu)
kujadili rufani ya Yanga kupinga
kunyang’anywa pointi tatu kwa kumchezesha Nadir
Haroub katika mechi dhidi ya Coastal
Union kimeahirishwa.
Kamati hiyo
chini ya uenyekiti wa Kamishna mstaafu wa Polisi, Alfred Tibaigana sasa
kitafanyika Jumanne (Aprili 17 mwaka huu) saa 9
alasiri kwenye ofisi za TFF.
MIKOA 13 YAWASILISHA MABINGWA WAKE
Vyama vya mpira wa miguu vya mikoa 17 ya Tanzania
Bara vimewasilisha majina ya
mabingwa wake kwa ajili ya Ligi ya Taifa iliyopangwa
kuanza Aprili 22 mwaka huu
katika vituo vitatu.
Mikoa hiyo
na mabingwa wake katika mabano ni Kigoma (Kanembwa FC ya Kibondo),
Kilimanjaro (Forest FC ya Siha), Ruvuma (Mighty
Elephant ya Songea), Dodoma (CDA),
Rukwa, (Mpanda Star ya Mpanda), Iringa (Kurugenzi
FC ya Mufindi) na Lindi (Lindi
SC).
Mingine ni
Mtwara (Ndanda FC), Shinyanga (Mwadui FC), Mara (Polisi Mara), Singida
(Aston Villa), Arusha (Flamingo SC) na Tabora
(Majimaji FC). Mikoa ambayo
haijawasilisha mabingwa wake ni Manyara, Dar es
Salaam, Mwanza, Tanga, Morogoro na
Kagera.
Source:Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
COMMENTS