JK atoa maagizo saba ya kuzingatiwa mazingira Tanzania

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS Telephone: 255-22-2114512, 2116898 E-mail:...


THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
              press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425



 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ametoa maagizo thabiti saba ya kuhifadhi mazingira nchini akisema “tusipokuwa makini na kuchukua hatua thabiti za kuhifadhi mazingira, uhai na ustawi wetu utakuwa mashakani. Tusipofanya hivyo, huko mbele ya safari kuna giza nene la maangamizi.”
Aidha, Rais Kikwete ametoa mifano saba ya kuthibitisha uharibifu wa mazingira duniani na kueleza njia nne ambazo kwa kiasi kikubwa zinachangia katika uharibifu wa mazingira nchini.
Amesisitiza kuwa jukumu la kutunza na la kuhifadhi mazingira ni la Watanzania wote, linalohitaji juhudi za pamoja na ushirikiano wa karibu wa wadau wote katika ngazi zote nchini.
Rais Kikwete ameeleza athari hizo za mazingira na hatua za kuchukuliwa kupambana na hali hiyo wakati alipohutubia mamia ya wananchi kwenye Uwanja wa Mashujaa mjini Moshi kwenye Kilele cha Maadhiminisho ya Siku ya Mazingira Duniani ambako pia amezindua Kampeni ya Kitaifa ya Usafi na Ujenzi wa Vyoo Bora.
Baada ya kueleza kwa ufasaha kuhusu athari za uharibifu wa mazingira nchini, Rais Kikwete ametoa maagizo thabiti saba ya jinsi ya kupambana na hali hiyo nchini ikiwa ni pamoja na kuzingatia umuhimu wa kuhifadhi ardhi na misitu kwa kupanda miti; kuhifadhi vyanzo vya maji, milima na misitu ya asili; na kudhibiti kilimo, ufugaji na uchimbaji wa madini usiokuwa endelevu.
Maagizo mengine ya Rais Kikwete ni kudhibiti matumizi mabaya ya dawa za mifugo na kilimo; kudhibiti uchafuzi wa mazingira katika maeneo ya makazi na viwandani; kusimamia uzalishaji bora usiochafua mazingira kwenye viwanda nchini; na kulinda mazingira ya pwani, mito, maziwa na bahari.
Rais Kikwete pia amewaeleza wananchi mifano saba ya kuthibitisha jinsi hali ya mazingira ilivyoharibika duniani ikiwa ni pamoja na ukweli kuwa majira ya mvua yamebadilika, mvua siyo ya uhakika na vipindi vya ukame vimeongezeka; theluji inapungua kwa kasi kwenye ncha za Kaskazini na Kusini mwa dunia na kwenye vilele ya milima ukiwamo Mlima Kilimanjaro; na kuongezeka kwa maji baharini na hivyo kuzidi kula nchi kavu na kuyaweka maeneo mengine katika hatari ya kumezwa na maji.
Mifano mingine ni magonjwa kama malaria kuzidi kusambaa katika maeneo ambayo zamani yalikuwa hayana mbu kwa sababu yalikuwa baridi na sasa yamekuwa joto; kuzidi kupungua kwa maji safi kwenye mito, chemichemi, vijito, maziwa na mabwawa; kuzidi kuendelea kupungua kwa eneo la misitu na kusambaa zaidi kwa jangwa; na kupungua kwa ubora wa ardhi na hivyo kupungua kwa mazao na malisho ya mifugo.
Kuhusu uharibifu wa mazigira nchini, Rais Kikwete amesema kuwa umekuwa unachangiwa pamoja na mambo mengine ukataji miti kwa wingi kwa ajili ya shughuli za kilimo; uvunaji miti kwa kasi zaidi kuliko ile inayopangwa; kuwepo kwa mifugo mingi kupita uwezo wa ardhi; na shughuli za viwanda na hasa mahitaji ya nishati na malighafi kusababisha uharibifu wa mazingira.
Kuhusu umuhimu wa kushirikiana kupambana na janga la uharibifu wa mazingira, Rais Kikwete amewaambia wananchi: “ Jukumu la kutunza na kuhifadhi mazingira ni letu sote, linahitaji juhudi za pamoja na ushirikiano wa karibu wa wadau husika katika ngazi zote. Sisi peke yetu Serikalini hatuwezi kwani wahenga wamesema: ‘kidole kimoja hakivunji chawa.’ Tunataka wote tuhusike – Serikali Kuu, Serikali za Mitaa, wananchi, NGO’s na kadhalika.”
Ameongeza Rais Kikwete: “Napenda kutumia nafasi hii kuzipongeza baadhi ya Serikali za Mitaa ambazo zimeunda Kamati za Mazingira ili kuratibu shughuli za kuhifadhi mazingira katika maeneo yao. Napenda kutoa mwito kwa Serikali za Mitaa ambazo bado hazijaunda Kamati hizo, wafanye hivyo mapema iwezekanavyo. Tayari nimewaagiza Wakuu wa Mikoa na Wilaya zote nchini kusimamia kwa makini Sheria na Kanuni za Hifadhi ya Mazingira katika maeneo yao. Natumaini hili litafanyika.”
Wakati wa sherehe hizo, Rais Kikwete pia amewakabidhi washindi wa mwaka huu wa mashindano ya usafi nchini na washindi wa mashindano ya kuhifadhi mazingira nchini ambako Shule ya Sekondari ya Kameyu ya Mkoa wa Manyara imechukua ushindi wa jumla wa ubora wa kuhifadhi na kutunza mazingira nchini.
Aidha, wakati wa sherehe hizo, Rais Kikwete amezindua Kampeni ya Taifa ya Usafi na Ujenzi wa Vyoo Bora ambao unaendeshwa kwa ushirikiano baina ya Serikali, Wananchi na Washirika wa Maendeleo wa Tanzania ikiwemo Benki ya Dunia na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mfuko wa Watoto (UNICEF).
Mapema leo asubuhi, Rais Kikwete amezindua Mpango wa Upandaji Miti wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini ambako maelfu kwa maelfu ya miti itapandwa katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha na Manyara. Rais amezindua Mpango huo kwa kupand mti aina ya Mzeituni kwenye eneo la Hosteli ya Uhuru mjini Moshi.

……..Mwisho…..

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
5 Juni, 2012

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4816,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: JK atoa maagizo saba ya kuzingatiwa mazingira Tanzania
JK atoa maagizo saba ya kuzingatiwa mazingira Tanzania
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2012/06/jk-atoa-maagizo-saba-ya-kuzingatiwa.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2012/06/jk-atoa-maagizo-saba-ya-kuzingatiwa.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy