Kutoka Lukwangule Katika pitapita yangu nilipata ujumbe huu katika mtandao wa http://daruislam.blog.com . Mimi ni mtu tu katika maisha...
Kutoka Lukwangule
Katika pitapita yangu
nilipata ujumbe huu katika mtandao wa http://daruislam.blog.com.
Mimi ni mtu tu katika maisha ya dunia lakini wenye akili na wasio na akili wana haki ya kusoma
maandiko na kuyatafakari kwa kina nini maana yake. Mungu amewapa nafasi hizo.Nayaweka
katika chapisho ndani ya bango hili bila kuhariri naamini walionazo na wasionazo wanaweza kuangalia
nini na kama wao mni wasomaji wa falsafa za plato,Aristotle na Yesu watajua
kwanini nimeweka chapisho hili.
Lukwangule
MKONO NYUMA YA VURUGU LA
ZANZIBAR NA MALENGO YAKE
Vurugu zilizotokea
karibuni na kuchukuwa siku kadhaa ndani ya Zanzibar
zilizopelekea kuchomwa
baadhi ya makanisa, kufungwa barabara, kuchomwa kwa
baadhi ya maduka ya ulevi
(baa) na kusitisha kwa kiasi fulani shughuli za
kiuchumi na kijamii kiasi
cha kulifanya Jeshi la Polisi kutawanya watu kwa
mabomu ya machozi na
kufanya doria sehemu kubwa ya mji zilipangwa na
kuratibiwa kwa malengo
maalum na kuna mkono mrefu nyuma yake.
Kabla ya kuelezea malengo
na mkono nyuma ya vurugu hili, amma mkono wa
ndani au mkono wa nje.
Kwanza, tuangalie baadhi ya viashiria
vinavyodhihirisha kwamba
vurugu hizi ni mchezo wa kuigiza:
Kwanza, Jumuiya ya Uamsho
ni rafiki mkubwa wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa
Zanzibar na Raisi wa
Zanzibar, kiasi cha Jumuiya hiyo kuandaa dua maalumu
kuiombea dua serikali
hiyo na Raisi wake.
Pili, licha ya Uamsho
kufanya mihadhara yake viwanjani, lakini pia imekuwa
ikitumia misikiti kwa
harakati zake mbali mbali katika vugu vugu hili. Kama
vile dua na itikafu.
Mmoja katika msikiti mkubwa unaotumika kwa harakati
zake ni Msikiti Munawwara
Kidongo chekundu. Msikiti ambao uko katika mikono
ya serikali.
Tatu, mihadhara ya
Jumuiya ya Uamsho inayotoa kauli kali dhidi ya muungano
na kuhamasisha watu wawe
tayari hata kufa kutetea nchi yao imekuwa
ikiendelea kwa muda mrefu
kwa baraka zote za Serikali ya Umoja wa Kitaifa
Zanzibar. Na Serikali
iliwapatia kibali cha miezi sita kufanya mahubiri
hayo. Kwa jina la kutoa
elimu ya uraia.
Nne, idara ya serikali ya
Waqfu ambayo ndio yenye dhamana ya kuratibu
masuala ya dini ya
Kiislamu yakiwemo mahubiri ya Kiislamu hususan viwanjani
ililamika kuhusu
mihadhara hiyo na kutaka kuisitisha lakini inaonekana
ilishindikana.
Tano, Waziri dhamana
katika Ofisi ya Makamo wa Pili wa Raisi Zanzibar,
bwana Mohammed Aboud
awali alitoa taarifa ya kujikosha serikali na
kutangaza kusitisha
mihadhara hiyo. Hali iliyopelekea baadhi ya wakuu wa
mikoa hususan Pemba
kutangaza kuzuia mihadhara hiyo katika maeneo yao,
lakini mihadhara
iliendelea kama kawaida, kana kwamba inaonekana waliagizwa
na serikali kuu waachie
mihadhara hiyo iendelee.
Sita, Umoja wa Vijana wa
CCM Zanzibar pamoja na wakereketwa muhafidhina wa
CCM walionekana kukerwa
na mihadhara hiyo pamoja na matamko makali dhidi ya
muungano yanayotolewa
katika mihadhara hiyo, na walianzisha kampeni maalumu
kwa kushirikiana na
wakereketwa wenye nguvu kama Borafya Silima na Mbaraka
Shamte kwa lengo la
kujibu na kukabiliana na wimbi la mihadhara hiyo, huku
wakijigamba kwamba
watakwenda sambamba na Jumuiya ya Uamsho, kwa kuwafuata
kila mahali inapofanyika
mihadhara yao kuvunja na kubomoa athari yao. Cha
kushangaza! si muda mrefu
Jumuiya hiyo ya CCM na wakereketwa wake pia
waliacha kampeni yao,
kana kwamba walitakiwa wasitishe.
Saba, siku ya Jumamosi
Mei 26 yalipofanywa maandamano na Uamsho yalifanywa
bila ya kibali na
yalipewa ulinzi kamili na jeshi la Polisi bila ya
kudhuriwa wala kukamatwa
viongozi wala waandamanaji na hawakupata pingamizi
yoyote.
Nane, kitendo na
mazingira ya kumkamata kwa kumnyakuwa Ustadh Mussa Juma
ambae hakuwa mstari wa
mbele sana kama wengine katika mihadhara wala katika
maandamano kilifanywa
akiwa msikitini ili kiguse hisia za Waumini.
Ikikusudiwa kuchochea
fujo na kupatikana uhalali wa vurugu, na ili
ipatikane fursa ya
kuongeza vitendo vya vurugu zaidi, kama kuchoma makanisa
ili kukuza ukubwa wa
vurugu na kuonekana kuna mgogoro na tatizo kubwa ndani
ya Zanzibar. Kazi ya
kuchoma makanisa yumkin kwa kiasi kikubwa walipewa
wakereketwa wa kundi la
vijana muhafidhina wa CCM wa maskani. Wakioneshwa
kwamba lengo la mkakati
huo ni kuimaliza Uamsho. Vijana hawa wa CCM kama
walivyo Uamsho ni wenye
jazba wasiokuwa na upeo wa mambo wala uchambuzi wa
kisiasa, kwa hivyo
wakalibeba jukumu hilo bila ya kurudi nyuma. Ilhali
lengo kuu la mkakati huo
wa kuchoma makanisa ni kukuza ukubwa wa vurugu na
kuonekana kuweko kiwango
kikubwa cha mgogoro.
Tisa, namna Polisi
walivyokabiliana na tukio lenyewe pia ni usanii wa wazi.
Kwanza, Kamishna wa
Polisi Zanzibar alitamka wazi kwamba viongozi
waliochochea vurugu
watakamatwa kwa gharama yoyote. Cha kushangaza!
Hakukuwa na kiongozi
yoyote wa mstari wa mbele aliyekamatwa au kufanywa
msako mkali kama
tulivyozoea. Pia namna Polisi walivyokuwa kwenye vurugu
hili, hakuna kiudhati
aliyejeruhiwa au kuuwawa kama tulivyozoea namna
Polisi wa hapa
wanapokabiliana kwa ukali wa kuruka mipaka na vurugu hususan
zenye kufungamana na
siasa.
Hivi ni baadhi ya
viashiria kwamba Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar
inaelewa fika kila
kinachotendeka na kukibariki kuanzia vugu vugu la
mihadhara ya Uamsho hadi
kuripuka vurugu.
*Nani nyuma ya vurugu
hili, na nini malengo yake?*
Hapa kuna misukumo miwili
mikubwa. Msukumo wa ndani na msukumo wa nje. Kwa
upande wa ndani, vurugu
hizi ni shinikizo la baadhi ya wanasiasa wakubwa wa
CCM Zanzibar wakiungwa
mkono na baadhi ya wanasiasa wa CUF Zanzibar
wanaofangamana kwa
uzalendo wao wa ‘uzanzibari’. Japo kwamba CUF nyuma ya
pazia inaonekana kupinga
vuguvugu hili, kwa kuwa ajenda ya vuguvugu la
Uamsho ni kuvunja
kabisaa.. Muungano, ilhali sera ya CUF ni kuwepo serikali
tatu. Lakini kimsingi CUF
imeshakufa na imebaki kuwa tawi la CCM. Na zaidi
hakuna matumaini kisiasa
kwa CUF kupata serikali ya Muungano kuweza
kutekeleza sera yake
hiyo. Kwa hivyo, sera yake juu ya Muungano na sera
nyenginezo zinabakia kuwa
nadharia tu. Hivyo si ajabu CUF Zanzibar kwa
hisia zao za kizalendo
wakadandia mkondo wa vugu vugu hili. Lakini kutokana
na nafasi za wanasiasa
hao katika serikali na katika vyama vyao na kulinda
maslahi yao binafsi
wanakosa ujasiri wa kuonekana wazi wazi. Aidha, wale
waliomo ndani ya CCM nao
hawana ushujaa katika vikao vyao halali vya chama
kutoa duku duku lao
kiudhati kuhusu Muungano, zaidi ya kusema ‘ndio
nakubaliana’ na kuahidi
‘kulinda Muungano’. Kwa hivyo, kundi hili wamehisi
watumie fursa ya
kuyadandia majukwaa ya dini ya Kiislamu. Kwa kuwa wakaazi
wa Zanzibar kiasili wana
hisia ya dini yao ya kiislamu, ili kuweza kuvutia
watu na wafuasi wengi
zaidi katika vugu vugu hili bila ya kuzingatia chama
chochote. Pia kauli mbiu
inayotumika na Uamsho ya kutaka kura ya maoni juu
ya mustakbali wa Muungano
imetumika ili ionekane kuwa kinyume kabisa na
vyama vyote vya kisiasa
vilivyopo. Lengo ni kuonesha na kupeleka ujumbe kwa
CCM taifa na serikali
yake ya Muungano kwamba hali si shwari tena kutoka
kwa raia wenyewe wa
Zanzibar. Ili kwa haraka matatizo mbali mbali
yanaotokamana na Muungano
yakiwemo suala la uchimbaji na umiliki wa mafuta
yatatuliwe kabla hali
haijawa ya kutisha zaidi!. Kimsingi Raisi wa sasa wa
Zanzibar si mtu shupavu
kama alivyokuwa Dk. Salmin Amour kuweza kuwa na
misimamao mikali ya
kizalendo. Lakini yumkin waliomzunguuka wameweza
kufanikiwa kumchochea
kuhusu maslahi ya Zanzibar hususan katika suala la
uchimbaji wa mafuta ambao
ni mtaji mwanana kisiasa. Ikumbukwe kwamba suala
la uchimbaji wa mafuta ya
Zanzibar limekuwa na mjadala mkali miongoni mwa
wanasiasa na wananchi
jumla, kiasi cha kuweza kuwaunganisha wanasiasa wa
Zanzibar na raia jumla
kuunga mkono vugu vugu la Uamsho, kwa lengo la
kuzidisha shinikizo kwa
Serikali ya Muungano kulitazama upya. Inawezekana
pia kwa kiasi kikubwa
katika vugu vugu hili kumuhusisha raisi mstaafu
aliemaliza muhula wake.
Katika zama zake, aliyekuwa Waziri wake wa Nishati
(Mansour) alikuwa
akitamka waziwazi kwa maneno makali kuhusu uchimbaji wa
mafuta na gesi ya
Zanzibar kwamba utabakia kuwa milki ya Zanzibar. Kitu
ambacho ni kinyume na
mawafikiano ya Muungano. Waziri Mansour alidiriki
kutoa kauli hizo kali
ilhali Raisi Amani si kwa nafasi yake ya uraisi, wala
Unaibu Mwenyekiti wa CCM
hakuthubutu kumchukulia hatua za kumzuia wala
kumuadhibu. Pamoja na
hayo Raisi huyu mstaafu ana shauku kubwa ya kumtakasa
baba yake kwamba alikuwa
na nia safi juu ya suala la Muungano.Kampeni
ambayo inapata nguvu vya
kutosha kila uchao. Kinyume na alivyokuwa
akichukuliwa huko awali
kwamba ni msaliti aliyeuza Zanzibar kwa Tanganyika.
Pamoja na sababu hiyo pia
wimbi hili ni ujanja wa kujificha kufeli kwa
Serikali ya Umoja wa
Kitaifa Zanzibar kinyume na matarajio ya raia.
*Msukumo wa nje. *
Kwa upande mwengine wa
msukumo wa nje. Vuguvugu hili linatokamana na
Marekani. Ukizingatia kwa
makini kauli ya balozi wa Marekani ndani ya
Tanzania Alfonso E.
Lenhardt, baada ya vurugu hili alitamka: *“Tunatambua
umuhimu wa kuwepo mjadala
wenye nguvu ndani ya umma, na tunahamasisha wadau
wote kuuendeleza kwa
utaratibu wa amani na kidemokrasia”*.
*
*
Akikusudia wahusika na
wadau wa qadhia hii waketi na walimalize jambo hili
kidemokrasia na kwa
maridhiano. Katika kauli hii kunadhihirika kiashiria
cha mkono wa dola hiyo.
Marekani inaelewa fika sera ya Muungano ya CCM
kwamba ni serikali mbili
kuelekea serikali moja, sasa iweje waketi kujadili
qadhia hii na wahusika
wengine? Marekani ndio msimamizi kwa kiasi kikubwa
wa Afrika Mashariki baada
ya kumnyan’ganya bwana wa asili wa ngome hii
yaani Uingereza. Licha ya
Marekani kufanikiwa kujenga himaya na ushawishi
mkubwa Afrika ya
Mashariki, bado inakabiliwa na upinzani mkubwa na
changamoto kadhaa kutoka
bwana huyo wa asili wa eneo hili (Uingereza). Hili
hudhihirika katika
upinzani mkubwa wa vyama vyao ndani ya nchi hizi. Kwa
mfano, Chama cha ODM
nchini Kenya chini ya Odinga ni chama cha Marekani,
ilhali chama cha PNU cha
Kibaki kiko chini ya Uingereza. Marekani
ilikabiliwa na hali ngumu
sana katika uchaguzi uliopita ndani ya Kenya
kutokana na ujanja wa
kisiasa wa Uingereza. Hadi ikalazimika kugawana
ngawira na keki ya Kenya
na mwenzake Uingereza. Hali hiyo mpaka sasa ni
tofauti na Tanzania.
Licha ya Uingereza kwa kupitia Chadema kuota mizizi,
bado chama cha CCM
ambacho ni chama cha Marekani kinaendelea kushikilia
hatamu ndani ya Serikali
ya Muungano. Na Marekani imefanikiwa kufanya
mkakati kabambe wa
kumakinisha athari yake ndani ya Zanzibar na kumkatisha
tamaa kabisa Uingereza
kwa kuunganisha chama chake kilichokuwa uwanjani CCM
na chama chake cha
akiba/reserve (CUF). Hata hivyo, Marekani imejifunza
kutoka siasa za Kenya,
lau haikuwa makini zaidi ndani ya Tanzania, amma
itafika mahala ipoteze
kabisa ushawishi wake na maslahi yake au italazimika
kugawana ngawira na
Uingereza. Hali itakayomugharimu kupungua athari yake
au kupoteza kabisa nguvu,
maslahi na ushawishi wake katika nchi hii. Kwa
hivyo, hali inavyoendelea
Tanzania kwa Chama cha Muingereza (Chadema)
kinachoungwa mkono pia na
Jumuiya ya Ulaya hususan Ujerumani, kinaonekana
kila siku kumakinika na
kupata watu wengi ndani ya Tanzania hususan Bara,
kiasi cha hata baadhi ya
vigogo wa chama cha CCM, ambao bila ya shaka
wanaounga mkono Uingereza
kutishia kutoka CCM na kuingia ndani ya Chadema.
Hali hiyo inaifanya
Marekani kutokuwa na raha juu ya mwenendo wa siasa za
Tanzania ikiwemo
Zanzibar. Kwa hivyo, vuguvugu hili la Uamsho Zanzibar ni
mchezo wa Marekani
kupitia CCM kiujanja, kwa kutumia baadhi ya vikundi vya
Kiislamu ndani ya
Zanzibar, amma kwa kujijua au kwa kutojijuwa kutokana na
kukosa kwao uweledi mpana
wa kisiasa na fikra thabiti ya Kiislamu. Marekani
imejifunza kwamba baadhi
ya vikundi vya Kiislamu ndani ya Tanzania hufanya
kazi nzuri ya kufikia
malengo yake ikiwemo kukiokoa chama chake cha CCM
kinapokuwa katika shimo
la maangamizi kwa kubanwa koo na Chadema. Kama
ilivyodhihirika katika
uchaguzi mdogo wa jimbo la Igunga. Wakati huo
takriban vikundi vingi
vya Kiislamu vililitumia tukio la kuvuliwa mtandio
Mkuu wa Wilaya Fatma
Kimario na wakereketwa wa Chadema kama ni ushahidi wa
chama hicho kuwa ni adui
wa Waislamu. Huku vikundi hivyo hivyo vya Kiislamu
vilijitia upofu wa tukio
kubwa ovu lililofanywa na CCM wakati huo huo,
kufanya dua ya pamoja
baina ya Waislamu na Wakiristo kuwaombea waathirika
wa ajali ya Mv. Spice
Zanzibar. Unapoyapima matukio mawili haya yaliyotokea
wakati mmoja kwa mujibu
wa ‘hukmu za Kiislamu’ licha ya kuwa yote ni maovu,
lakini la CCM ni ovu
zaidi. Sasa iweje vikundi hivi kwa hili la CCM vibakie
kimya cha mfu? Na kwa
upande wa baadhi ya vikundi vilivyopo Zanzibar
vilifanya kazi nzuri kwa
gharama ndogo wakati wa kupiga kampeni ya Marekani
ya kuundwa Serikali ya Umoja
wa Kitaifa ya Zanzibar.
Katika vugu vugu hili
linaloendelea la Uamsho Marekani hailengi tu, kuunda
serikali tatu katika
Muungano, bali ikiwezekana, lakini kwa njia za busara
kuiondoa kabisa Zanzibar
katika Muungano. Japo kwamba si jambo jepesi,
litakalogharimu Zanzibar
gharama za mambo ya ubalozi na mengineyo pia
kugharimu Tanganyika
kulitangaza upya kimataifa dola lao jipya. Na lau
haitowezekana Marekani
inadhamiria walau kuweka serikali tatu kwa lengo la
kuumega muungano kidogo
kidogo mpaka kuuhitimisha kabisa. Kwa sababu,
kuitoa Zanzibar katika
Muungano ni jambo la usalama na utulivu zaidi kwa
maslahi ya Marekani ya
uchimbaji wa mafuta ya Zanzibar hata kuliko kuwapo
serikali tatu. Na pia
salama kwake amma ikiwa Bara kinatawala chama chake
cha CCM au kikishinda
chama cha Uingereza (Chadema). Utaona, japo kwamba
sera ya Uingereza
(Chadema) kidhahiri katika suala la Muungano ni serikali
tatu, lakini inawezekana
huo ni mtego tu wa Uingereza ambao Marekani
inaonekana kuung’amua.
Yumkin, lau Chadema kinapata ushindi Tanganyika,
Uingereza inaweza
ikaigeuza ghafla sera hiyo kiasi cha kuirejesha tena
Zanzibar katika mikono ya
Uingereza kutokana na kuwepo rasilmali ya mafuta.
Karibuni Mbunge mwenye
nguvu wa Chadema Zitto Kabwe alikaririwa akisema
kwamba masuala ya mafuta
na gesi hayakupaswa kuwa katika mambo ya Muungano.
Kauli hiyo ya kijanja ni
dhihirisho ya kukita siasa za Muingereza ndani ya
Chadema. Siasa ‘za
unachosema kinyume na unachoamini na kukitendea kazi’.
Marekani na maafisa wa
juu wa CCM wanajua kinachoendelea katika vuguvugu la
Uamsho na vurugu
zilizojiri, wanajaribu kuonesha kwa ufundi sana kwamba
hili ni suala
linalotokamana na wazanzibari wenyewe bila ya mkono wa nje,
kama lilivyoonyeshwa
suala la muwafaka baina ya ‘Karume na Seif’
lililopelekea kuzaliwa
Serikali ya Umoja wa Kitaifa. Dhamira ya kuonesha
hivyo ni kuwafanya
muhafidhina ndani ya CCM waweze kuikubali hali hiyo
kidogo kidogo na kuanza
kulainika kidogo kidogo tayari kwa mabadiliko.
Kwa ufupi, Marekani
inalenga kwa mkakati wa vuguvugu la Uamsho kama mbinu
ya kufikia kujihifadhi na
kujilinda dhidi ya Uingereza, pia ipate kuikomba
kwa raha, salama na
utulivu rasilmali ya mafuta ndani ya Zanzibar. Huku
Marekani akijifanya
kijanja kuwaridhisha wazanzibari kwamba wanajitawalia
mambo yao wenyewe
kikamilifu nje ya Muungano, dhana iliyojaa ndani ya vifua
vyao.
*Matarajio*
Baada ya vurugu hili
Serikali ya Umoja wa Kitaifa kuwa mkali mdomoni,
lakini laini kivitendo
kwa Uamsho, viongozi wake na vurugu lililotokea.
Tayari ZBC (Shirika la
Utangazaji Zanzibar) katika Tv wanaonesha picha za
matokeo ya vurugu hili,
na hitimisho la kipindi hicho humalizia: *‘iliyopita
si ndwele tugange ijayo’*
Pia mihadhara itabanwa kidogo, na hatimae
kuruhusiwa kama kawaida.
Baadhi ya kesi zilizofunguliwa dhidi ya walioleta
vurugu zitafutwa na kufa
kifo cha kawaida, serikali italipa gharama za
uharibifu wa makanisa na
mali nyenginezo, na Marekani kiufundi kidogo
kidogo itahamasisha
mabadiliko ili kuandaa mazingira ya kufikia lengo lake.
Na viongozi wa juu wa CCM
wataonekana kukemea qadhia hii kijanja kwa ukali,
kana kwamba hawana habari
ya kinachoendelea.
*Hitimisho*
Kwa hakika,
kuchanganyikiwa kwa ndugu zetu katika umma kunatupa moyo wa
fedheha na masikitiko
makubwa. Lau ingekuwa aibu ya kifamilia tu
tungeinyamazia mambo
yakesha! Lakini kwa kuwa tunabeba qadhia ya umma,
hulazimika tuuonye na
kuuonesha njia. Katika mwezi kama huu wa Rajab mwaka
1342 Hijri sawa na
mwanzoni mwa mwezi wa Machi mwaka 1924 miladi, ndio
wakati waliodiriki makafiri
kwa uadui mkubwa kuimaliza dola ya mwisho ya
Kiislamu (Khilafah
Uthmania). Miongoni mwa silaha ya hatari waliyoitumia
makafiri hao kufikia
lengo hilo ni fikra hii wanayoishadidia leo Uamsho,
fikra ya ubaguzi/
aswabia. Fikra ya watu kujifunga, kujilabu na kujitukuza
kwa mujibu wa maeneo yao
wanayoishi au walipozaliwa, badala ya kujinasibu
kama sehemu ya umma
mtukufu wa Kiislamu ulioenea duniani kote. Hatimae,
Waarabu wakaona wana
mambo yao kama Waarabu, na Waturuki kama Waturuki.
Haikumalizia hapo, katika
Waturuki wakajitukuza wengine kundi la Wakurdi,
na Waarabu nao ardhi zao
zikakatwa vijinchi telee…. hadi nyengine ni aibu
hata kuziita nchi kamwe!
Lau Umma wetu ungejifunga vilivyo na hukmu za
Kiislamu na manhaj sahihi
ya Kiislamu usingeweza kamwe kuingia ndani ya
mtego kama hii ya
makafiri.
Tunamuomba Allah *Ta’ala
*katika mwezi huu mtukufu wa Rajab ainue ufahamu
wa umma wetu ujifunge
kidhati na manhaj ya Mtume wetu (SAAW) katika kuleta
mageuzi ya kweli ili
tuweze kurejesha tena izza/nguvu yetu kwa kurejesha
tena dola yetu ya
Kiislamu ya *Khilafah Rashidah* kama alivyobashiri
kipenzi chetu SAAW.
18 Rajab 1433 Hijri
04/06/2012 Miladi
*
Tembelea mtandao wetu
www.daruislam.blog.com*
*Shukran*
COMMENTS