Burundi yamtunukia Tuzo Mwalimu Nyerere

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Taifa la Burundi limemtunukia Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere Tuzo la juu kabisa ambalo Burundi hut...

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Taifa la Burundi limemtunukia Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere Tuzo la juu kabisa ambalo Burundi hutoa kwa watu mbali mbali kutokana na mchango wake katika kuleta uhuru na baadaye kwa jitihada zake kubwa za kuleta amani katika nchi hiyo.
Mwalimu Nyerere alitunukiwa Tuzo hilo – Tuzo la Taifa la Burundi (Order of the National Republic of Burundi) -  kwenye Kilele cha Sherehe za Kuadhimisha Miaka 50 ya Uhuru wa Burundi zilifanyika jana, Independence Road, pembeni mwa Uwanja wa Michezo wa Louis Rwagasore mjini Bujumbura na kutangazwa hadharani kwa maelfu kwa maelfu ya watu waliohudhuria sherehe hizo.
Tuzo hiyo ya Mwalimu imepokelewa kwa niaba yake na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ambaye alikuwa mmoja wa viongozi sita wa nchi za nje waliohudhuria sherehe hizo.
Akitangaza Tuzo hilo, Rais wa Burundi, Mheshimiwa Pierre Nkurunzinza alisema kuwa Burundi imeamua kumtunuku Mwalimu Nyerere sababu mbili – moja ni ushauri wake muhimu sana katika kuleta uhuru wa Burundi kutoka kwa wakoloni wa Kibelgiji.
“Kwanza Mwalimu alikuwa mshauri muhimu sana wa Mwanzilishi wa Taifa letu, Mheshimiwa Louis Rwagasore na baadaye zilikuwa ni jitihada zake ambazo hatimaye zimeleta amani na utulivu ambao tunaufurahia katika Burundi kwa sasa,”
Pamoja na Hayati Mwalimu, aliyekuwa Rais wa Afrika Kusini Mzee Nelson Mandela pia amepata tuzo hiyo. Mzee Mandela alichukua nafasi ya Mwalimu kama mpatanishi wa mgogoro wa Burundi kufuatia kifo cha Mwalimu mwaka 1999.
Katika sherehe hizo, zilizoendelea mfululizo kwa saa saba unusu tokea saa nne asubuhi hadi saa 11 jioni, Rais Kikwete aliungana na viongozi wenzake wa nchi sita na wawakilishi wa nchi nyingine nyingi duniani kuhudhuria kilele cha sherehe za kufana kuadhimisha Miaka 50 ya Uhuru wa Burundi.
Burundi ilipata uhuru kutoka kwa wakoloni wa Kibelgiji Julai 2, mwaka 1962 na Rais Kikwete aliwasili Bujumbura asubuhi ya jana, akitokea Kigali, Rwanda, ambako pia alihudhuria sherehe kama hizo Kuadhimisha Sherehe za Miaka 50 ya Uhuru wa Rwanda iliyopata uhuru Julai Mosi, 1962, kutoka kwa wakoloni hao hao wa Kibelgiji.
Tofauti na Rwanda ambako Rais Kikwete alikuwa rais pekee aliyehudhuria sherehe za uhuru wa nchi hiyo na mgeni rasmi, katika sherehe za Burundi, Mheshimiwa Rais na Mama Salma Kikwete wameungana na Rais mwenyeji Pierre Nkurunzinza, Rais Mwai Kibaki wa Kenya, Rais Theodore Obing Nguema wa Equatorial Guinea, Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Rais Francois Bozize wa Jamhuri ya Afrika ya Kati na Rais Shariff Sheikh Ahmed Shariff katika kusherehekea uhuru wa Burundi.

Walikuwepo wawakilishi wa nchi nyingine nyingi duniani akiwamo Makamu wa Rais wa Uganda na Makamu wa Rais wa Nigeria, Mheshimiwa Prince Philip ambaye ni mtoto wa Malkia wa Belgium, Waziri Mkuu wa Swaziland na Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU) anayemaliza muda wake, Mheshimiwa Jean Ping.
Wananchi wa Burundi wamejitokeza kwa wingi sana kuhudhuria sherehe za uhuru wa nchi yao ambayo tokea mwaka 1965 yalipotokea mapinduzi ya kijeshi ya kwanza haijapata kuwa na raha ya kuwa na amani kwa miaka 10 mfululizo ukiondoa sasa.
Moja ya mambo ambayo yamechukuwa muda mrefu kiasi cha saa tatu ni maandamano ya wananchi wa Burundi ambayo yameshirikisha vikundi vya wananchi kutoka taasisi mbali mbali zikiwamo Idara za Serikali, Makampuni Binafsi na Taasisi Zisizokuwa za Kiserikali.
Askari wa miavuli wakiwa wamebeba bendera za Taifa la Burundi pia wamekuwa kivutio kikubwa katika sherehe hizo kama yalivyokuwa maonyesho ya makomando wa Jeshi la Anga la Burundi (BAF)  kutoka kwenye helikopta iliyosimama angani hadi chini kiasi cha urefu wa mita 150.
Aidha, ngoma aina ya Rukinzo ilivutia sana wananchi kama lilivyokuwa gwaride la nchi tano Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambako kila kundi la askari wakiongozwa na kundi la askari wa Burundi lakini kila kundi likiwa chini ya kamanda wake lilipita mbele ya viongozi na maelfu kwa maelfu ya wananchi waliohudhuria sherehe hizo.
Mbali na ngoma za vikundi vya ngoma za asili na utamaduni wa Burundi zimevutia sana hisia za wananchi,  pia wananchi kwenye sherehe hizo wameshuhudia gwaride la kuvutia la Jeshi la Burundi likiwa na vikosi mbali mbali kikiwemo Kikosi cha Kulinda Amani katika nchi mbali mbali duniani. Aidha, gwaride hilo limeshirikisha Jeshi la Polisi ambalo lilionyesha vifaa vya huduma mbali mbali ambazo hutolewa na Jeshi hilo  kulinda usalama wa raia zikiwamo za usalama barabarani, huduma za zima moto na huduma za magari ya kubeba wagonjwa.
Jeshi la Burundi pia limetumia nafasi ya sherehe hizo kuonyesha vifaa vinavyotumiwa na vikosi vya Jeshi hilo ambavyo ni Jeshi la Ardhini, Jeshi la Maji na Jeshi la Anga ikiwa ni pamoja na helikopta mbili za kijeshi –helicopter Gun Ships.
Rais Nkurunziza, mwenyeji wa sherehe hizo, ambaye alianza kuhutubia Taifa la Burundi kiasi cha saa 10 mchana, alitumia muda wa kutosha kuisifia Tanzania na uongozi wake wa awamu mbali mbali kwa mchango wake mkubwa katika uhuru wa Burundi na baadaye katika mazungumzo ya kuleta amani katika Burundi.
Alimsifia Rais Kikwete kama Rais wa nchi rafiki na jirani na kama “kaka yangu” katika hotuba hiyo ambako alitangaza kumtunukia medali ya juu kabisa katika Taifa la Burundi Mwalimu Nyerere kwa mchango wake katika Uhuru wa Burundi na baadaye katika kuleta amani ya nchi hiyo.
Rais Kikwete anatarajiwa kuondoka mjini Bujumbura baadaye leo, Jumanne, Julai 3, 2012, kurejea nyumbani.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
3 Julai, 2012



COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4816,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: Burundi yamtunukia Tuzo Mwalimu Nyerere
Burundi yamtunukia Tuzo Mwalimu Nyerere
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2012/07/burundi-yamtunukia-tuzo-mwalimu-nyerere.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2012/07/burundi-yamtunukia-tuzo-mwalimu-nyerere.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy