BAADHI ya wanahabari nchini wamekuwa wabunifu na hivyo kuanzisha vipindi katika vituo vya televisheni na redio, ambavyo si tu vinavutia, l...
BAADHI ya
wanahabari nchini wamekuwa wabunifu na hivyo kuanzisha vipindi katika vituo vya
televisheni na redio, ambavyo si tu vinavutia, lakini pia vinaburudisha na
kuelimisha jamii kwa jumla.
Binafsi nawapongeza wanahabari wa aina hiyo, ambao kila kukicha hufikiria na kuja na ubunifu wa hali ya juu katika kutimiza dhima yao kwa jamii, lakini pia wakishawishi usikilizaji na utazamaji wa vipindi kwa maslahi ya wamiliki wa vituo hivyo.
Siku za nyuma, nilitokea kuvutiwa sana na kipindi cha Planet Bongo kikiendeshwa na mtangazaji mahiri, Salama Jabir ambapo kimekuwa kikitoa fursa kwa wanamuziki mbalimbali hususan wa kizazi kipya, kueleza mafanikio lakini pia matatizo yao na kutoa elimu kwa chipukizi.
Salama ni mahiri katika kuhoji maswali rahisi na pia magumu, ambayo hulenga katika udadisi wa kutaka kumchimba msanii husika ili awe wazi kuelezea undani wake na afahamike zaidi na mashabiki na wasio mashabiki wake, lakini pia wasanii wenzake.
Lakini alipokwenda Uingereza kimasomo, Salama alitoa fursa kwa Abdallah ‘Dulla’, anayejiita wakati mwingine kuwa ni mjukuu wa Ambua, kukiendesha kipindi hicho lakini baada ya kupitia mchujo wa watu waliokuwa wakiwania kukiendesha.
Dulla amekuwa akikiendesha kipindi hicho kwa mafanikio makubwa pia, lakini hajapata kufikia kiwango alichokuwa nacho Salama katika eneo hilo, kwa kuwa aliweza kujizolea watazamaji kibao.
Mtangazaji Salama aliendelea kuwa mahiri hata katika ujaji kwenye mashindano ya kusaka mwimbaji bora chini ya Kampuni ya Benchmark. Kipindi kinachojulikana kama Bongo Star Search au BSS na sasa Epic Bongo Star Search ambako amejizolea marafiki na maadui pia.
Sambamba na kuendelea na BSS, Salama hivi sasa anaendesha kipindi kingine cha Mikasi ambacho kama Planet Bongo, kinarushwa na kituo cha Televisheni cha East African (EATV) kila Jumatatu saa 3.30 usiku ambapo nami hupata fursa ya kukiangalia.
Kama ilivyo kwa Planet Bongo, hiki kina wahusika ambao si tu wasanii bali watu mashuhuri katika jamii ambao pengine si rahisi kukutana nao ana kwa ana na kuzungumza nao. Lakini hivi sasa Salama anawakutanisha na hadhira kupitia luninga.
Anawahoji nao wanajieleza bila hofu, huku wakitengenezwa nywele na hata kucha. Pamoja na kukipenda kipindi hiki hasa kutokana na kuwa na matumaini na mwandaaji wake, Salama, nimethibitisha sasa kuwa kumbe mgema akisifiwa tembo hulitia maji.
Salama anaanza kunitilia maji tembo hili ambalo nimekuwa nikipenda kulinywa kila Jumatatu! Nasema hivi nikirejea kipindi cha Mikasi cha Jumatatu ya Agosti 13, ambapo Salama alikuwa na mgeni mwingine mashuhuri, msanii wa kizazi kipya, Nasib Abdul ‘Diamond’.
Ingawa mimi si mpenzi sana wa msanii huyu, lakini navutiwa na unadhifu wake, kitu ambacho hata yeye anajivunia na kuutambia.
Kama kawaida, Salama na wasaidizi wake walimhoji kuhusu maisha yake na muziki wake na hasa mafanikio aliyopata kwa jumla na akaonesha dhahiri kwamba nyuma ya mafanikio yake mhimili mkuu ni mama yake mzazi, lakini pia akataja watu wengine kadhaa na kusema ni wengi anaotambua mchango wao na asingeweza kuwataja.
Ni kweli na alikuwa mwungwana kwa hilo. Lakini Salama alikuja kutia tembo maji kutokana na maswali yake yaliyokosa staha. Mathalan alipomwuliza ni lini ilikuwa mara ya mwisho kujamiiana; au kuwapo uvumi kwamba mama yake ‘anatembea’ na vijana wadogo au anasikia ‘amejaaliwa’ (akimaanisha sehemu zake za siri) !
Kwa kweli ilihitaji saikolojia rahisi tu, kujua ni swali gani la kumwuuliza mtu ambaye alishatangulia kueleza kuwa siku moja alilia machozi baada ya kufikiria kuwa mama yake akifariki dunia itakuwaje, seuse kumwambia uvumi wa mama huyo ‘kutembea’ na vijana –Serengeti boys! Hakika ni kumkosea heshima mama huyo na mwanawe.
Na hiyo ilitokana na swali la Salama kwake kwamba ni lini anakumbuka alilia sana. Ndipo akamweleza kuhusu mama huyo bila kubaini kuwa baadaye atakumbana na swali kama hilo, la kuutibua moyo wake na hasa lihusulo mama yake kipenzi.
Maswali yote hayo yalionesha wazi kumkirihisha Diamond ingawa alionekana kucheka, lakini hata mimi, nadhani na wenzangu baadhi tulikerwa na maswali ya aina hiyo yanayoulizwa katika chombo kinachoheshimika kama EATV, bila kujua wanaoangalia ni watu wa aina gani na hasa ikizingatiwa muda ule wa mapema.
Pengine hali hiyo inatokana na kukosekana wasimamizi wa vipindi kama ambavyo hufanyika katika baadhi ya vituo makini vya redio na televisheni. Kama ndivyo basi kuna hatari iko siku tutasikia matusi, tutashuhudia watu wakiwa uchi na hata wengine wakijamiiana katika vipindi kama hivyo.
Sina ubaya wala chuki na Salama, lakini naweza kuwa na ubaya na chuki na maudhui ya vipindi vyake hivyo. Ni vema akalenga kuuliza maswali ya kidadisi zaidi yenye staha, maswali ambayo yatajenga udadisi na kiu ya kujifunza kwa wasanii wachanga ili kuiga wasanii nguli badala ya kuwafundisha matusi kama hayo.
Source: Habarileo: imeandikwa na Joseph Kulangwa Mhariri habarileo
Binafsi nawapongeza wanahabari wa aina hiyo, ambao kila kukicha hufikiria na kuja na ubunifu wa hali ya juu katika kutimiza dhima yao kwa jamii, lakini pia wakishawishi usikilizaji na utazamaji wa vipindi kwa maslahi ya wamiliki wa vituo hivyo.
Siku za nyuma, nilitokea kuvutiwa sana na kipindi cha Planet Bongo kikiendeshwa na mtangazaji mahiri, Salama Jabir ambapo kimekuwa kikitoa fursa kwa wanamuziki mbalimbali hususan wa kizazi kipya, kueleza mafanikio lakini pia matatizo yao na kutoa elimu kwa chipukizi.
Salama ni mahiri katika kuhoji maswali rahisi na pia magumu, ambayo hulenga katika udadisi wa kutaka kumchimba msanii husika ili awe wazi kuelezea undani wake na afahamike zaidi na mashabiki na wasio mashabiki wake, lakini pia wasanii wenzake.
Lakini alipokwenda Uingereza kimasomo, Salama alitoa fursa kwa Abdallah ‘Dulla’, anayejiita wakati mwingine kuwa ni mjukuu wa Ambua, kukiendesha kipindi hicho lakini baada ya kupitia mchujo wa watu waliokuwa wakiwania kukiendesha.
Dulla amekuwa akikiendesha kipindi hicho kwa mafanikio makubwa pia, lakini hajapata kufikia kiwango alichokuwa nacho Salama katika eneo hilo, kwa kuwa aliweza kujizolea watazamaji kibao.
Mtangazaji Salama aliendelea kuwa mahiri hata katika ujaji kwenye mashindano ya kusaka mwimbaji bora chini ya Kampuni ya Benchmark. Kipindi kinachojulikana kama Bongo Star Search au BSS na sasa Epic Bongo Star Search ambako amejizolea marafiki na maadui pia.
Sambamba na kuendelea na BSS, Salama hivi sasa anaendesha kipindi kingine cha Mikasi ambacho kama Planet Bongo, kinarushwa na kituo cha Televisheni cha East African (EATV) kila Jumatatu saa 3.30 usiku ambapo nami hupata fursa ya kukiangalia.
Kama ilivyo kwa Planet Bongo, hiki kina wahusika ambao si tu wasanii bali watu mashuhuri katika jamii ambao pengine si rahisi kukutana nao ana kwa ana na kuzungumza nao. Lakini hivi sasa Salama anawakutanisha na hadhira kupitia luninga.
Anawahoji nao wanajieleza bila hofu, huku wakitengenezwa nywele na hata kucha. Pamoja na kukipenda kipindi hiki hasa kutokana na kuwa na matumaini na mwandaaji wake, Salama, nimethibitisha sasa kuwa kumbe mgema akisifiwa tembo hulitia maji.
Salama anaanza kunitilia maji tembo hili ambalo nimekuwa nikipenda kulinywa kila Jumatatu! Nasema hivi nikirejea kipindi cha Mikasi cha Jumatatu ya Agosti 13, ambapo Salama alikuwa na mgeni mwingine mashuhuri, msanii wa kizazi kipya, Nasib Abdul ‘Diamond’.
Ingawa mimi si mpenzi sana wa msanii huyu, lakini navutiwa na unadhifu wake, kitu ambacho hata yeye anajivunia na kuutambia.
Kama kawaida, Salama na wasaidizi wake walimhoji kuhusu maisha yake na muziki wake na hasa mafanikio aliyopata kwa jumla na akaonesha dhahiri kwamba nyuma ya mafanikio yake mhimili mkuu ni mama yake mzazi, lakini pia akataja watu wengine kadhaa na kusema ni wengi anaotambua mchango wao na asingeweza kuwataja.
Ni kweli na alikuwa mwungwana kwa hilo. Lakini Salama alikuja kutia tembo maji kutokana na maswali yake yaliyokosa staha. Mathalan alipomwuliza ni lini ilikuwa mara ya mwisho kujamiiana; au kuwapo uvumi kwamba mama yake ‘anatembea’ na vijana wadogo au anasikia ‘amejaaliwa’ (akimaanisha sehemu zake za siri) !
Kwa kweli ilihitaji saikolojia rahisi tu, kujua ni swali gani la kumwuuliza mtu ambaye alishatangulia kueleza kuwa siku moja alilia machozi baada ya kufikiria kuwa mama yake akifariki dunia itakuwaje, seuse kumwambia uvumi wa mama huyo ‘kutembea’ na vijana –Serengeti boys! Hakika ni kumkosea heshima mama huyo na mwanawe.
Na hiyo ilitokana na swali la Salama kwake kwamba ni lini anakumbuka alilia sana. Ndipo akamweleza kuhusu mama huyo bila kubaini kuwa baadaye atakumbana na swali kama hilo, la kuutibua moyo wake na hasa lihusulo mama yake kipenzi.
Maswali yote hayo yalionesha wazi kumkirihisha Diamond ingawa alionekana kucheka, lakini hata mimi, nadhani na wenzangu baadhi tulikerwa na maswali ya aina hiyo yanayoulizwa katika chombo kinachoheshimika kama EATV, bila kujua wanaoangalia ni watu wa aina gani na hasa ikizingatiwa muda ule wa mapema.
Pengine hali hiyo inatokana na kukosekana wasimamizi wa vipindi kama ambavyo hufanyika katika baadhi ya vituo makini vya redio na televisheni. Kama ndivyo basi kuna hatari iko siku tutasikia matusi, tutashuhudia watu wakiwa uchi na hata wengine wakijamiiana katika vipindi kama hivyo.
Sina ubaya wala chuki na Salama, lakini naweza kuwa na ubaya na chuki na maudhui ya vipindi vyake hivyo. Ni vema akalenga kuuliza maswali ya kidadisi zaidi yenye staha, maswali ambayo yatajenga udadisi na kiu ya kujifunza kwa wasanii wachanga ili kuiga wasanii nguli badala ya kuwafundisha matusi kama hayo.
Source: Habarileo: imeandikwa na Joseph Kulangwa Mhariri habarileo
COMMENTS