Wazo la HabariLeo latamanisha maarifa katika dunia huru.. wapi mipaka

BAADHI ya wanahabari nchini wamekuwa wabunifu na hivyo kuanzisha vipindi katika vituo vya televisheni na redio, ambavyo si tu vinavutia, l...

BAADHI ya wanahabari nchini wamekuwa wabunifu na hivyo kuanzisha vipindi katika vituo vya televisheni na redio, ambavyo si tu vinavutia, lakini pia vinaburudisha na kuelimisha jamii kwa jumla.
Binafsi nawapongeza wanahabari wa aina hiyo, ambao kila kukicha hufikiria na kuja na ubunifu wa hali ya juu katika kutimiza dhima yao kwa jamii, lakini pia wakishawishi usikilizaji na utazamaji wa vipindi kwa maslahi ya wamiliki wa vituo hivyo.
Siku za nyuma, nilitokea kuvutiwa sana na kipindi cha Planet Bongo kikiendeshwa na mtangazaji mahiri, Salama Jabir ambapo kimekuwa kikitoa fursa kwa wanamuziki mbalimbali hususan wa kizazi kipya, kueleza mafanikio lakini pia matatizo yao na kutoa elimu kwa chipukizi.
Salama ni mahiri katika kuhoji maswali rahisi na pia magumu, ambayo hulenga katika udadisi wa kutaka kumchimba msanii husika ili awe wazi kuelezea undani wake na afahamike zaidi na mashabiki na wasio mashabiki wake, lakini pia wasanii wenzake.
Lakini alipokwenda Uingereza kimasomo, Salama alitoa fursa kwa Abdallah ‘Dulla’, anayejiita wakati mwingine kuwa ni mjukuu wa Ambua, kukiendesha kipindi hicho lakini baada ya kupitia mchujo wa watu waliokuwa wakiwania kukiendesha.
Dulla amekuwa akikiendesha kipindi hicho kwa mafanikio makubwa pia, lakini hajapata kufikia kiwango alichokuwa nacho Salama katika eneo hilo, kwa kuwa aliweza kujizolea watazamaji kibao.
Mtangazaji Salama aliendelea kuwa mahiri hata katika ujaji kwenye mashindano ya kusaka mwimbaji bora chini ya Kampuni ya Benchmark. Kipindi kinachojulikana kama Bongo Star Search au BSS na sasa Epic Bongo Star Search ambako amejizolea marafiki na maadui pia.
Sambamba na kuendelea na BSS, Salama hivi sasa anaendesha kipindi kingine cha Mikasi ambacho kama Planet Bongo, kinarushwa na kituo cha Televisheni cha East African (EATV) kila Jumatatu saa 3.30 usiku ambapo nami hupata fursa ya kukiangalia.
Kama ilivyo kwa Planet Bongo, hiki kina wahusika ambao si tu wasanii bali watu mashuhuri katika jamii ambao pengine si rahisi kukutana nao ana kwa ana na kuzungumza nao. Lakini hivi sasa Salama anawakutanisha na hadhira kupitia luninga.
Anawahoji nao wanajieleza bila hofu, huku wakitengenezwa nywele na hata kucha. Pamoja na kukipenda kipindi hiki hasa kutokana na kuwa na matumaini na mwandaaji wake, Salama, nimethibitisha sasa kuwa kumbe mgema akisifiwa tembo hulitia maji.
Salama anaanza kunitilia maji tembo hili ambalo nimekuwa nikipenda kulinywa kila Jumatatu! Nasema hivi nikirejea kipindi cha Mikasi cha Jumatatu ya Agosti 13, ambapo Salama alikuwa na mgeni mwingine mashuhuri, msanii wa kizazi kipya, Nasib Abdul ‘Diamond’.
Ingawa mimi si mpenzi sana wa msanii huyu, lakini navutiwa na unadhifu wake, kitu ambacho hata yeye anajivunia na kuutambia.
Kama kawaida, Salama na wasaidizi wake walimhoji kuhusu maisha yake na muziki wake na hasa mafanikio aliyopata kwa jumla na akaonesha dhahiri kwamba nyuma ya mafanikio yake mhimili mkuu ni mama yake mzazi, lakini pia akataja watu wengine kadhaa na kusema ni wengi anaotambua mchango wao na asingeweza kuwataja.
Ni kweli na alikuwa mwungwana kwa hilo. Lakini Salama alikuja kutia tembo maji kutokana na maswali yake yaliyokosa staha. Mathalan alipomwuliza ni lini ilikuwa mara ya mwisho kujamiiana; au kuwapo uvumi kwamba mama yake ‘anatembea’ na vijana wadogo au anasikia ‘amejaaliwa’ (akimaanisha sehemu zake za siri) !
Kwa kweli ilihitaji saikolojia rahisi tu, kujua ni swali gani la kumwuuliza mtu ambaye alishatangulia kueleza kuwa siku moja alilia machozi baada ya kufikiria kuwa mama yake akifariki dunia itakuwaje, seuse kumwambia uvumi wa mama huyo ‘kutembea’ na vijana –Serengeti boys! Hakika ni kumkosea heshima mama huyo na mwanawe.
Na hiyo ilitokana na swali la Salama kwake kwamba ni lini anakumbuka alilia sana. Ndipo akamweleza kuhusu mama huyo bila kubaini kuwa baadaye atakumbana na swali kama hilo, la kuutibua moyo wake na hasa lihusulo mama yake kipenzi.
Maswali yote hayo yalionesha wazi kumkirihisha Diamond ingawa alionekana kucheka, lakini hata mimi, nadhani na wenzangu baadhi tulikerwa na maswali ya aina hiyo yanayoulizwa katika chombo kinachoheshimika kama EATV, bila kujua wanaoangalia ni watu wa aina gani na hasa ikizingatiwa muda ule wa mapema.
Pengine hali hiyo inatokana na kukosekana wasimamizi wa vipindi kama ambavyo hufanyika katika baadhi ya vituo makini vya redio na televisheni. Kama ndivyo basi kuna hatari iko siku tutasikia matusi, tutashuhudia watu wakiwa uchi na hata wengine wakijamiiana katika vipindi kama hivyo.
Sina ubaya wala chuki na Salama, lakini naweza kuwa na ubaya na chuki na maudhui ya vipindi vyake hivyo. Ni vema akalenga kuuliza maswali ya kidadisi zaidi yenye staha, maswali ambayo yatajenga udadisi na kiu ya kujifunza kwa wasanii wachanga ili kuiga wasanii nguli badala ya kuwafundisha matusi kama hayo.
Source: Habarileo: imeandikwa na Joseph Kulangwa Mhariri habarileo

COMMENTS

BLOGGER: 2
Loading...
Name

Anga,12,Arusha,27,batiki,1,Burudani,447,burundani,2,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,78,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,288,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,haba,1,habar,3,Habari,7077,habari dodoma,39,habari. dodoma,32,habaria,1,hadithi,23,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,52,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,6,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,739,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,miochezo,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,376,muziki na fasheni,20,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,10,SAYANSI ANGA,12,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,17,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,urembo,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTALII,1,UTAMADUNI,4,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: Wazo la HabariLeo latamanisha maarifa katika dunia huru.. wapi mipaka
Wazo la HabariLeo latamanisha maarifa katika dunia huru.. wapi mipaka
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2012/08/wazo-la-habarileo-latamanisha-maarifa.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2012/08/wazo-la-habarileo-latamanisha-maarifa.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy