TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI ESB International yasherehekea mafanikio ya mradi kabambe 10 Aprili 2013, Kampuni ya ESB Int...
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
ESB International yasherehekea mafanikio ya mradi kabambe
10
Aprili 2013, Kampuni ya ESB Internatioanl (ESBI) ya Ireland, leo inasherekea
mafanikio makubwa ya jukumu lake kama mhandisi mshauri kinara wa moja ya miradi
kubwa zaidi Afrika wa nishati – Mradi huo wa Nishati uliochini ya Millennium
Challenge Account Tanzania (MCA-T), kwa kuwasha rasmi njia mpya ya msongo wa
umeme wa 132kV unaotoka Tanzania bara kwenda Zanzibar.
Kiunganishi
hicho [Interconnector], ambayo ni moja tu ya kipengele cha mradi huo wa
nishati, kitakuwa na uwezo wa kusafirisha megawati 100 za umeme kutoka Tanzania
Bara kwenda visiwani Zanzibar, ambayo ni mara mbili zaidi ya uwezo uliopo sasa
wa upitishaji wa umeme katika njia zilizopo.
Mwaka
2008, ESBI ilishinda zabuni ya kimataifa ya mhandisi mshauri ya kutoa huduma
kiushauri za nishati kwa MCA-T. Moja ya changamoto kubwa nchini, ni maendeleo
duni ya miundombinu kwenye tasinia ya nishati. Kwani ni aslimia 15 ya idadi ya
watu inayopta umeme toka gridi ya taifa. Serikali ya Marekani ilifadhili mradi
huo wa nishati kwa kutoa dola za Marekani 200milioni kupitia MCA-T. Lengo la
mradi huo ni kuhakikisha maendeleo ya muda mrefu katika usambazaji wa umeme kwa
kizazi kijacho.
Akizungumza
kuhusu mradi huo, Bwana. Karl Fickenscher, Mkurugenzi Mkazi wa Millennium
Challenge Corporation (MCC) alisema: "tunafahari kufadhili mradi huu
muhimu na tunafuraha kuona umefikia hatua hii. Kwa uwekezaji wanamna hii tu
tunataraji kuimarisha ubora na upatikanaji wa umeme katika Tanzania. Na ni
matumaini yetu, kwa msaada wa washirika kama vile ESB, watu zaidi ya milioni
1.5 watafaidika kutokana na mradi wa umeme wa MCC kwa zaidi ya miaka 20 ijayo.
"
Sherehe
za uzinduzi huo zilifanyika Ikulu ya Zanzibar na kuhudhuriwa na Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein,
Mkurugenzi Mtendaji wa MCC Daniel W. Yohannes, Bw Fickenscher, Mkurugenzi
Mtendaji wa MCA-T Bernard Mchomvu, na Kaimu Mkureugenzi Mtendaji wa MCA-T Ahmed
Rashid. Wenginewaliohudhuria sherehe hizo ni pamoja na Kaimu Mkuregenzi
Mtendaji ESB John Shine, Mkurugenzi Mtendaji ESB Ollie Brogan
na Mkurugezi wa Miradi ESB John Ashley.
Akizungumza
juu ya mradi Bw Brogan alisema: "Tumefurahi kwa kufikiwa kwa hatua hii
kubwa ya uzinduzi wa njia hii kubwa mpya ya umeme leo. Tumetoa huduma ya
ushauri kwa MCA-T, ikiwa ni pamoja na vipimo na usimamizi wa ufungaji wa mambo
yote ya viunganishi ikiwa ni pamoja na vituo vidogo vya kupoozea umeme, na
mkonga wa nchini ya bahari,. Pia tumetoa huduma za ushauri kwa miradi
inayoendelea MCA-T ya umeme vijijini ambayo inajengwa zinajengwa katika mikoa
saba ya Tanzania. "
Aliongeza:
"Hii inaonyesha uwezo wa ESB wa kuchanganyika kirahisi na tamaduni
nyingine, kuweza kufanyakazi na mashirika mengine ya umeme, kusimamia makampuni
mbali mbali ya ukandarasi ya matiafa mengine pamoja na kusimamia masuala ya
kijamii na kimazingira kama yanavyojitokeza. Ujio wa umeme huu utabadilisha
maisha ya watu na kutoa mwanga mpya kwa vizazi vya baadaye kama ilivyokuwa
katika Ireland katika miaka ya 1950. "
-
Mwisho -
Kuhusu
ESB International
ESB International
(ESBI) ni moja ya kampuni kubwa za uhandishi ushauri barani Ulaya na imejikita
kuongoza uhandisi maalumu katika sekta ya umeme. Tangu kuanzishwa kwake karibu
miongo minne iliyopita, imekamilisha miradi katika nchi 115. Kampuni pia
imebobea kwenye miradi mikubwa ya miundombinu kwa niaba ya kampuni tanzu ya ESB
ikiwa ni pamoja na wateja wa kimataifa.
ESBI hutoa ushauri wa
mtaalamu katika masuala yote ya mafuta na nishati mbadal, usambazaji na ugawaji
wa umeme wa kimkakati kama vile teknolojia ya kisasa. Ufuaji umeme toka
baharini. Kwa sasa imeajiri zaidi ya wafanyakazi 800.
Kuhusu Millennium
Challenge Corporation (MCC)
Millennium
Challenge Corporation (MCC) ni shirika la misaada linalojitegemea la Kimarekani
ambalo leno lake ni kuongoza mapambano dhidi ya umaskini duniani lilianzishwa
na Bunge la Congress ya Marekani Januari 2004, Mtizamo wa MCC ni kutafuta namna
bora zaidi na nzuri ya ubatikanaji wa misaaada toka Marekani kwa kuzingatia
sera rafiki, umiliki nchi, na matokeo. Mwaka 2008, serikali ya Marekani na
serikali ya Tanzania zilisaini makubaliano ya miaka mitano chini ya Compact
ilikuiwezesha Tanzania katika kufikia malengo ya ukuaji wa Millennium Challenge
kiuchumi na kupunguza umaskini kwa njia ya maendeleo ya miundombinu. Kama
sehemu ya Compact, serikali ya Marekani ilitoa ruzuku ya dola za marekani
686,000,000 kufadhili miradi ya miundombinu katika sekta Nishati, Usafiri na
Maji.
Taarifa
kuhusu mkataba wa mhandisi ushauri wa ESBI
Mwaka
2008 ESBI ilishinda mkataba wa ushahuri huduma wa jumla wa dola za kimarekani
25 millioni kupitia mchakato wa kimataifa na unatakiwa kukamilika Septemba
2013. Mradi huo ni pamoja kufanya yafuatayo: –
-Utoaji
na ufungaji wa msongo wa 132kV wa chini ya bahari kutoka Tanzania Bara kwenda
Zanzibar
- Utoaji
na ufungaji wa nyanya za juu za 132kV sehemu ya nchi kavu upande wa
Tanzania Bara na Zanzibar
- Utoaji
na uwekaji wa vifaa vya kusambazia umeme kwa vituo vidogo 22 pamoja na vituo
vingine katika mtandao huo nchini kote.
-Utoaji
na uwekaji wa mifumo mipya ya mtandao wa usambazaji na ukarabati wa mifumo ya
iliyopo katika mikoa saba ya Tanzania
-Ubunifu
wa awali wa mtambo wa kuzalisha umeme wa 40MW Magharibi mwa Tanzania.
-Mipango
ya kuyajengea uwezo mashirika ya TANESCO kwa Tanzania bara na ZECO,kwa Zanzibar
.
Awamu
za mkataba zilijumuisha:
- Kuandaa mipango -------Planning phase
- Maandalizi ya kiufundi ya nyaraka za tenda na uchambuzi wa tenda.
- Majadiliano ya mikataba na walioshinda tenda.
- Upitiaji na uidhinishaji wa michoro ya ujenzi ya wakandarasi iliyowasilishwa.
- Usimamizi wa utekelezaji wa mambo yote ya mradi.
- Kupokea na kuthibitisha ukamilishaji wa mambo katika mradi.
- Provision of Defects Liability Period services
Kwa
taarifa zaidi tembelea: www.esbi.ie
Kwa
maelezo zaidi wasiliana na:
Ogilvy
Ireland -Colette Campbell at 01 660 030. /colette.campbell@ogilvy.com
Ogilvy
Dar es Salaam –Martin Kasavuli - martin.kasavuli@ogilvyafrica.com
COMMENTS