TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI YANGA, KOCHA VPL WAPIGWA FAINI KLABU ya Yanga na Kocha Msaidizi wa timu ya Toto Africans, Athuman Bilali wamep...
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
YANGA, KOCHA VPL WAPIGWA FAINI
KLABU ya Yanga na Kocha Msaidizi wa timu ya Toto Africans, Athuman Bilali
wamepigwa faini ya sh. 500,000 kila mmoja kutokana na makosa mbalimbali
katika mechi za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) inayoendelea nchini.
Adhabu hizo zimetolewa na Kamati ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu
Tanzania (TFF) iliyokutana Jumapili (Aprili 7 mwaka huu) jijini Dar es
Salaam kupitia ripoti za waamuzi na makamishna kwa michezo namba 108 hadi
171.
Yanga imepigwa faini hiyo baada ya kupata kadi tano za njano katika mechi
dhidi ya Kagera Sugar iliyochezwa Februari 7 mwaka huu. Vilevile Kagera
Sugar imepigwa faini ya sh. 100,000 kwa kuchelewa kufika kwenye kikao cha
maandalizi ya mechi (pre match meeting) dhidi ya African Lyon iliyochezwa
mjini Bukoba, Februari 23 mwaka huu.
Naye Kocha Bilali amepigwa faini hiyo na kufungiwa mechi tatu za ligi hiyo
kwa kumshambulia kwa maneno kocha wa timu pinzani, hali iliyosababisha
mwamuzi amtoe kwenye benchi la wachezaji. Alifanya tukio hilo kwenye mechi
kati ya Toto Africans na Tanzania Prisons iliyochezwa Aprili 3 mwaka huu
jijini Mwanza.
African Lyon na Simba zimepigwa faini ya sh. 500,000 kila moja kwa
kushindwa kuchezesha timu zao za U20 kwenye mechi za utangulizi wakati
zilipocheza na Oljoro JKT na Coastal Union, Machi mwaka huu kwenye viwanja
vya Azam Complex na Uwanja wa Taifa.
Suala la Meneja wa Coastal Union, Akida Manchai kumshambulia kwa maneno
yasiyo ya kiungwana Makamu Mwenyekiti wake Steven Mnguto baada ya kwenye
mechi kati ya African Lyon na Coastal Union iliyochezwa Machi 30 mwaka huu
Uwanja wa Azam Complex limepelekwa Kamati ya Nidhamu kwa ajili ya hatua za
kinidhamu.
Adhabu zote zimetolewa kwa mujibu wa Kanuni za Ligi Kuu ya Vodacom.
*POLISI KUJIULIZA KWA RUVU SHOOTING VPL*
Polisi Morogoro inapambana na Ruvu Shooting katika moja kati ya mechi tatu
za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) zitakazochezwa kesho (Aprili 10 mwaka huu).
Matokeo ya mechi hiyo yanatarajia kutoa mwanga kama Polisi inaweza kubaki
kwenye ligi hiyo msimu ujao.
Timu hiyo itakuwa nyumbani Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro katika mechi
hiyo itakayochezeshwa na Ibrahim Kidiwa kutoka Tanga akisaidiwa na Godfrey
Kihwili na Ephrony Ndissa wa Arusha.
Polisi Morogoro inayonolewa na Adolf Rishard inakamata nafasi ya mwisho
ikiwa na pointi 18 tu na imebakiza mechi tatu dhidi ya Simba, Kagera Sugar
na Coastal Union.
Mechi nyingine za kesho ni kati ya Tanzania Prisons iliyo nafasi ya 12
ikiwa na pointi 20 dhidi ya Mgambo Shooting. Mwamuzi Hashim Abdallah wa Dar
es Salaam ndiye atakayechezesha mechi hiyo kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya
Sokoine jijini Mbeya. Mgambo ina pointi 24 na iko katika nafasi ya tisa.
Mwamuzi Said Ndege wa Dar es Salaam atachezesha mechi kati ya wenyeji
Mtibwa Sugar na Toto Africans itakayofanyika Uwanja wa Manungu ulioko
Turiani mkoani Morogoro. Toto Africans ya Kocha John Tegete ina pointi 21
ikiwa nafasi ya 11 wakati Mtibwa Sugar iko nafasi ya tano na pointi zake 32.
Ligi hiyo itaendelea keshokutwa (Aprili 11 mwaka huu) kwa mechi moja kati
ya Azam na African Lyon itakayofanyika Uwanja wa Azam Complex.
*KAMATI YAZIPONGEZA ASHANTI, MBEYA CITY, RHINO *
Kamati ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imezipongeza
timu za Ashanti United ya Dar es Salaam, Mbeya City ya Mbeya na Rhino
Rangers ya Tabora kwa kupanda Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) msimu ujao
(2013/20114).
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Wallace Karia amezitaka timu hizo kufanya
maandalizi ya kutosha ili ziweze kushindana katika VPL ikiwemo kutimiza
masharti ya kuwa klabu za Ligi Kuu.
Moja ya masharti ya klabu zenye hadhi ya Ligi Kuu ni kuwa na timu ya pili
(U20) ambayo itakuwa na inacheza mechi za utangulizi kwenye uwanja wa
nyumbani kila timu ya wakubwa inapocheza.
Mbali ya kuthibitisha timu hizo tatu kupanda daraja, pia Kamati ya Ligi
imethibitisha rasmi timu tatu zilizoshuka daraja kurudi Ligi ya Mkoa katika
mkoa husika. Timu zilizoshuka kutoka Daraja la Kwanza (FDL) ni Small Kids
ya Rukwa kutoka kundi A.
Kundi B timu iliyoshuka ni Moro United ya Dar es Salaam wakati Morani FC ya
Manyara yenyewe imeporomoka kutoka kundi C.
*Boniface Wambura*
*Ofisa Habari*
*Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)*
YANGA, KOCHA VPL WAPIGWA FAINI
KLABU ya Yanga na Kocha Msaidizi wa timu ya Toto Africans, Athuman Bilali
wamepigwa faini ya sh. 500,000 kila mmoja kutokana na makosa mbalimbali
katika mechi za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) inayoendelea nchini.
Adhabu hizo zimetolewa na Kamati ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu
Tanzania (TFF) iliyokutana Jumapili (Aprili 7 mwaka huu) jijini Dar es
Salaam kupitia ripoti za waamuzi na makamishna kwa michezo namba 108 hadi
171.
Yanga imepigwa faini hiyo baada ya kupata kadi tano za njano katika mechi
dhidi ya Kagera Sugar iliyochezwa Februari 7 mwaka huu. Vilevile Kagera
Sugar imepigwa faini ya sh. 100,000 kwa kuchelewa kufika kwenye kikao cha
maandalizi ya mechi (pre match meeting) dhidi ya African Lyon iliyochezwa
mjini Bukoba, Februari 23 mwaka huu.
Naye Kocha Bilali amepigwa faini hiyo na kufungiwa mechi tatu za ligi hiyo
kwa kumshambulia kwa maneno kocha wa timu pinzani, hali iliyosababisha
mwamuzi amtoe kwenye benchi la wachezaji. Alifanya tukio hilo kwenye mechi
kati ya Toto Africans na Tanzania Prisons iliyochezwa Aprili 3 mwaka huu
jijini Mwanza.
African Lyon na Simba zimepigwa faini ya sh. 500,000 kila moja kwa
kushindwa kuchezesha timu zao za U20 kwenye mechi za utangulizi wakati
zilipocheza na Oljoro JKT na Coastal Union, Machi mwaka huu kwenye viwanja
vya Azam Complex na Uwanja wa Taifa.
Suala la Meneja wa Coastal Union, Akida Manchai kumshambulia kwa maneno
yasiyo ya kiungwana Makamu Mwenyekiti wake Steven Mnguto baada ya kwenye
mechi kati ya African Lyon na Coastal Union iliyochezwa Machi 30 mwaka huu
Uwanja wa Azam Complex limepelekwa Kamati ya Nidhamu kwa ajili ya hatua za
kinidhamu.
Adhabu zote zimetolewa kwa mujibu wa Kanuni za Ligi Kuu ya Vodacom.
*POLISI KUJIULIZA KWA RUVU SHOOTING VPL*
Polisi Morogoro inapambana na Ruvu Shooting katika moja kati ya mechi tatu
za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) zitakazochezwa kesho (Aprili 10 mwaka huu).
Matokeo ya mechi hiyo yanatarajia kutoa mwanga kama Polisi inaweza kubaki
kwenye ligi hiyo msimu ujao.
Timu hiyo itakuwa nyumbani Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro katika mechi
hiyo itakayochezeshwa na Ibrahim Kidiwa kutoka Tanga akisaidiwa na Godfrey
Kihwili na Ephrony Ndissa wa Arusha.
Polisi Morogoro inayonolewa na Adolf Rishard inakamata nafasi ya mwisho
ikiwa na pointi 18 tu na imebakiza mechi tatu dhidi ya Simba, Kagera Sugar
na Coastal Union.
Mechi nyingine za kesho ni kati ya Tanzania Prisons iliyo nafasi ya 12
ikiwa na pointi 20 dhidi ya Mgambo Shooting. Mwamuzi Hashim Abdallah wa Dar
es Salaam ndiye atakayechezesha mechi hiyo kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya
Sokoine jijini Mbeya. Mgambo ina pointi 24 na iko katika nafasi ya tisa.
Mwamuzi Said Ndege wa Dar es Salaam atachezesha mechi kati ya wenyeji
Mtibwa Sugar na Toto Africans itakayofanyika Uwanja wa Manungu ulioko
Turiani mkoani Morogoro. Toto Africans ya Kocha John Tegete ina pointi 21
ikiwa nafasi ya 11 wakati Mtibwa Sugar iko nafasi ya tano na pointi zake 32.
Ligi hiyo itaendelea keshokutwa (Aprili 11 mwaka huu) kwa mechi moja kati
ya Azam na African Lyon itakayofanyika Uwanja wa Azam Complex.
*KAMATI YAZIPONGEZA ASHANTI, MBEYA CITY, RHINO *
Kamati ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imezipongeza
timu za Ashanti United ya Dar es Salaam, Mbeya City ya Mbeya na Rhino
Rangers ya Tabora kwa kupanda Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) msimu ujao
(2013/20114).
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Wallace Karia amezitaka timu hizo kufanya
maandalizi ya kutosha ili ziweze kushindana katika VPL ikiwemo kutimiza
masharti ya kuwa klabu za Ligi Kuu.
Moja ya masharti ya klabu zenye hadhi ya Ligi Kuu ni kuwa na timu ya pili
(U20) ambayo itakuwa na inacheza mechi za utangulizi kwenye uwanja wa
nyumbani kila timu ya wakubwa inapocheza.
Mbali ya kuthibitisha timu hizo tatu kupanda daraja, pia Kamati ya Ligi
imethibitisha rasmi timu tatu zilizoshuka daraja kurudi Ligi ya Mkoa katika
mkoa husika. Timu zilizoshuka kutoka Daraja la Kwanza (FDL) ni Small Kids
ya Rukwa kutoka kundi A.
Kundi B timu iliyoshuka ni Moro United ya Dar es Salaam wakati Morani FC ya
Manyara yenyewe imeporomoka kutoka kundi C.
*Boniface Wambura*
*Ofisa Habari*
*Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)*
COMMENTS