MJUMBE wa Bunge Maalumu la Katiba, Hamad Rashid Mohamed amemchana wazi wazi Makamu wa Rais wa Kwanza wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzib...
MJUMBE wa Bunge Maalumu
la Katiba, Hamad Rashid Mohamed amemchana wazi wazi Makamu wa
Rais wa Kwanza wa
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ambaye pia ni Katibu Mkuu
wa Chama cha
Wananchi-CUF, Maalim Seif Rashid Hamad kuwa ni kiongozi hatari na
kigeugeu ambae awali
alikuwa na msimamo wa Serikali tatu lakini sasa anasimamia
muungano wa mkataba.
Hamad ambaye mbali na
ujumbe wa Bunge Maalumu ni Mbunge wa Jimbo la Uwakilishi la Wawi
kupitia chama cha CUF,
nafasi aliyorejeshewa na mahakama baada ya kutaka
kunyang’anywa na chama
chake, amesema mwaka 1992, uongozi wa CUF ulisimamia
serikali tatu lakini juzi
Maalim Seif katika mikutano ya hadhara anasema
msimamo wa chama hicho ni
Muungano wa mkataba.
“Tuangalieviongozi
wanaobadilika badilika, mwaka 1992 msimamo wa CUF ulikuwa serikali
tatu, juzi serikali ya
mkataba, kila baada ya dakika tatu, ‘posti’ nafasi
inabadilika kila wakati,
kiongozi wa aina gani huyu?,” alihoji Hamad.
Alisema wakati wakidai
Katiba mpya, CUF na vyama vingine vya upinzani viliandamana na
kuwaingiza watu kwenye
ulemavu, wajane na watoto, wanafunzi walikosa masomo na
leo badala ya kuhakikisha
Katiba inapatikana, wanahatarisha amani na kutaka
mapinduzi tena.
Hamad aliyasema haya jana
jioni, bungeni mjini hapa, akichangia mjadala wa Raismu ya Katiba
kuhusu sura ya kwanza na
ya sita.
Alihoji kati yake na
Maalim Seif, msaliti ni nani kwani wakati wakiwa wanatafuta serikali ya
umoja wa kitaifa,
walikutana sehemu mbalimbali ikiwemo Dodoma na kuafikiana
namna ya kufanya serikali
hiyo, lakini alishangaa wenzake watano akiwemo Maalim
Seif walijifungia ndani,
wakaja na masuala ya mkataba, na kuhoji kama ni
usaliti, nani msaliti wa
wenzake.
“Tulienda kwenye kikao
cha Halmashauri Kuu na ikapendekezwa Mwinyi (Rais Ali Hassan) agombee
Urais na kwa vyovyote
Maalim Seif awe Waziri Mkuu…..kama haitoshi, wakati Idrisa
akiwa Rais, Seif
aliendelea kuwa Waziri Kiongozi Zanzibar, sasa Wazanzibari
msaliti mnamfahamu,”
alisema Hamad.
Alisema Mwalimu Julius
Nyerere mwaka 1992 walienda kwake wakiwa saba na aliwaambia kama kuna
makosa amefanya ni
kuitambua Biafra na kuwatambua wao lakini alisema hiyo ni
siasa na kusema Nyerere
katika yote hayo, aliwaagiza kuhakikisha kuwa Muungano
unabaki hai.
“Kwanza tushukuru tuna
Rais mstaarabu, mvumulivu, watu wanampa ‘ultimatum’ (masharti ya
shinikizo) siku saba lakini
anacheka tu, kwa wenzetu hili halitokei…utakuwa jela,’ alisema Hamad.
Akisisitiza zaidi, alisema
Bunge hilo linapaswa kufanya uamuzi kwamba ni theluthi mbili ya wajumbe
kutoka Bara na vivyo
hivyo kutoka Zanzibar na si vinginevyo. “Ukawa hawana
theluthi mbili wala
Tanzania Kwanza, wenye mamlaka ni Bunge hili.
“Theluthi mbili pande
zote tukae, hakuna dhambi tutafanya, tumeendesha maandamano na kudai
Katiba, Tume Huru, watu
wameumia na wengine kupoteza maisha, leo Katiba inapatikana,
hutaki, tukae tuhakikishe
Katiba inapatikana,” alisistiza Hamad.
Akielezea zaidi kuhusu
Ukawa kutoka nje, Hamad alisema, “Hata kama hoja yako ni ya wachache,
vizazi vitafanya utafiti
na kusema huyu alisema hili, unapotoka nje kutunga
sheria au Katiba unafanya
uuaji na hili
ni jambo bay asana.
“Bunge hili baada ya
kumaliza kazi ndio tunaenda kwa wananchi, mbona unatangulia bila
safari kuanza, tuangalie
viongozi wa aina hii, mwaka 1984 Maalim Seif alitaka
serikali mbili, mwaka
1992 akiwa CUF msimamo ukawa Serikali tatu, juzi mkataba,
huyu ni kiongozi wa aina
gani, ni kuwaongopea watu,” alisema Hamad.
Alisema yeye
tangu mwaka 1982 yupo
Tanzania Bara na kwamba uhusiano wake na Bara si wa
kawaida, ni wa kindugu wa
damu na kusema kama kuna watu wanasema yeye
amekimbia, hakimbii
mapambano wala hakimbii tendo la kihistoria.
“Mheshimiwa
Mwenyekiti nilifiwa mimi,
mtu wa kwanza kuja alikuwa Kingunge Kombare Mwiru
(Mjumbe wa Bunge hilo)
ndio wengine wakafuata, undugu wetu si wa kawaida,”
alisisitiza
Hamad.
Alisema juzi walipodai
amekimbia, alikuwa kwenye mkutano Mexico mitatu tofauti nchini humo
ukiwemo wa masuala ya
Rasilimali na alishangaa kuona kuwa hata washiriki wa
mikutano hiyo
wanafuatilia na kuzungumzia mchakato unaoendelea nchini.
“Wanashangaa nyie
Watanzania ndio walimu wetu lakini leo mmepata kichaa gani mnamsema vibaya
Nyerere na Karume, kama
ingekuwa ni hapa kwetu, mgeipata habari yenu,” alisema
na kuongeza kuwa muungano
ni hazina na jambo adimu duniani, unapaswa kuutunza
na kutoudharau kamwe.
Akizungumzia
safari za tiba za
viongozi, Hamad alisema kiongozi mmoja kama Makamu wa Rais,
hutumia sh zaidi ya
milioni 400 kutubiwa India hivyo gharama hizo kwa kuongeza
serikali nyingine, ni
kuwabebesha mzigo wananchi.
Alisema kuna
watu wanajinadi kuwatetea
Wazanzibar kuwa wao ndio Wazanzibar wa kweli bila
wanzanzibari wenyewe
akitaka Watanzania kuwa macho na watu wa aina hiyo.
Alionya wasiwaingize
kwenye mapinduzi
mengine kwa kuwa
Wanzanizbar wataikataa
Katiba itakayosema Serikali Tatu kwa kuwa wao kw amujibu
wa Tume ya Warioba,
asilimia 61 walitaka serikali ya mkataba hivyo si sahihi
kusema wanataka serikali
tatu, wakati Bara ni Serikali mbili kupitia mabaraza
ya Katiba ya Kata na Wilaya.
Baada ya
kumaliza kuchangia, Hamad
alivishwa skafu ya bendera ya Taifa na Mjumbe Mwigulu
Nchemba kuonesha
kazungumza mambo ya utaifa na Mwenyekiti Samuel Sitta,
alitangaza kuwa amevishwa
bendera ya Taifa.
SOURCE Habarileo
COMMENTS