MKURUGENZI WA TAMWA ATUNUKIWA TUZO YA CEFM CHAMPION

Balozi wa Canada nchini Tanzania, Mh. Alexandre Lévêque akimkabidhi tuzo ya kwanza Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Wanahabari Wanawake Tan...

DSC_01311-1024x681 (1)

Balozi wa Canada nchini Tanzania, Mh. Alexandre Lévêque akimkabidhi tuzo ya kwanza Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania-TAMWA,Bi. Valerie Msoka kwa kufanikisha kampeni dhidi ya ndoa za utotoni.(Picha zote kwa hisani ya mtandao wa hivisasa.co.tz).

Na modewjiblog team

Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Habari Tanzania (TAMWA) Valerie Msoka, amekuwa mtu wa kwanza kutunukiwa tuzo ya CEFM Champion, na Ubalozi wa Canada nchini.

Katika sherehe fupi iliyofanyika Serena Hotel 24 Februari 2015, Balozi wa Canada nchini Bwana Alexandre Leveque alisema kuwa Valerie Msoka amekuwa mwanaharakati wa kwanza kutunikiwa tuzo hiyo na ubalozi wake kama ishara ya kukubali mchango wake kupiga vita ndoa za utotoni, za kulazimishwa na ukeketaji kwa watoto wa kike nchini.

“Watoto wa kike na wanawake wamevumilia machungu ya ndoa za utotoni na za kulazimishwa hivyo wanahitaji mtu wa kuwasemea: mtu ambae ataelezea taarifa zao zinakazosaidia kuwaweka watu pamoja na kuleta mabadiliko yenye tija,”amesema Balozi Lévêque. Valerie Msoka atakuwa mtetezi. Ninafuraha kumtangaza kuwa Mtetezi wa CEFM wa Ubalozi wa Canada nchini Tanzania.”

Valerie ametumia ujuzi wake kama mwanahabari aliyebobea, mwanaharakati na mpenda maendeleo kwa kushirikiana na wadau mbalimbali bila kujali litakalomtokea au kueleweka vibaya na jamii.

Ameandika taarifa zenye kuvuta hisia, huruma na kuhamasisha kasi ya mabadiliko Katika jamii na watunga sera,” alisema Balozi Leveque.

DSC_02031-1024x681

Wapili kutoka kushoto ni Balozi wa Canada nchini Tanzania Alexandre Lévêque , Mkurugenzi mtendaji wa TAMWA Valerie Msoka, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto, Anna Maembe na wawakilishi mbalimbali kutoka mashirika ya Umoja wa Mataifa wa masuala ya wanawake, UNFPA na UN Women.

Watoto wa kike milioni 14 duniani huozeshwa kila siku katika umri mdogo chini ya 18 jambo ambalo ni kinyume cha haki za mtoto na ukiukwaji wa haki za binadamu. Tanzania ni miongoni mwa nchi zinazoongoza kwa ndoa za utotoni na mikoa husika ni Shinyanga, Tabora, Mara, Lindi, Mbeya na Morogoro.

Balozi Leveque ameahidi kuunga mkono jitihada zinazomlinda mtoto wa kike ili kuendeleza kampeni ya Zero Marriage kwa mkoa wa Mara iliyozindiliwa mwaka 2014 na aliyekuwa mke wa Hayati Rais wa Kizalendo wa Afrika ya Kusini Nelson Mandela, Graca Machel.

Akitoa shukrani baada ya kupokea tuzo hiyo, Valerie Msoka alisema kuwa ndoa za utotoni za kulazimishwa na ukeketaji vyote vinaenda pamoja na ni wajibu wa wadau mbalimbali ikiwemo serikali na vyombo vya habari kuendeleza kutoa elimu, kufanya tafiti ili kuwa na rekodi inayofahamika kuhusu ukubwa wa tatizo, kufuatilia mwenendo na mafanikio ya kampeni mbalimbali na kuendeleza hamasa kwa jamii kwa nini ndoa za utotoni zikomeshwe.

“Tukitaka kufanikisha kampeni hii ni lazima tufanye kazi kwa pamoja na kwa moyo mmoja, kuelewa nani anafanya nini kwa kiwango gani. Serikali nayo bado tunaitegemea sana kwa hali na mali katika kubadilisha sera zinazomkandamiza mtoto wa kike kwa kuzingatia mabadiliko ya katiba mpya”, alisema Valerie.

DSC_01191-1024x681 (1)

Wadau mbambali wa masula ya wanawake na waandishi wa habari wakongwe (Ma-Veterans), kutoka kushoto ni Fatuma Aloo pamoja na Mama Rose Haji Mwalimu wakihsuhudia tukio hilo.

“Tuzo hii ni yetu wote, kama sio kwa ushirikiano wenu wadau wa maendeleo, vyombo vya habari ambavyo tumefanya kazi kwa karibu sana na jamii kwa ujumla. Ni matumaini yangu kuwa tutaendelea kushikamana kuhakikisha kuwa hadhi ya mtoto wa kike inalindwa ipasavyo”.

Hii ni mara ya pili kwa kiongozi wa Chama cha Waandishi wa Habari Tanzania (TAMWA) kupata tuzo ya kutambulika. Mwaka 2010 Ubalozi wa Marekani ulimtunuku Mkurugenzi aliyemaliza muda wake Ananilea Nkya tuzo ya Mwanamke Jasiri kutokana na mchango wake wa kuendeleza usawa, fursa na haki kwa wanawake wa wasichana wa Kitanzania.

Akitoa nasaha zake kwa niaba ya serikali, Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Watoto na Jinsia Bi Anna Maembe amempongeza Msoka kwa kazi nzuri na chama anachokiendesha kwa ujumla na kusema kwamba tuzo hii imetolewa wakati ambapo dunia na taifa kwa ujumla linatafakari matokeo ya Beijing +20 ambako Katika maazimio 20 yaliyoainishwa, Tanzania ilipendekeza kulifanyia kazi azimio moja ambalo ni la kumlinda mtoto wa kike.

Maembe amesema tuzo hii itatoa hamasa kwa wengine na itakuwa kielelezo cha serikali Katika jitihada za kutekeleza tamko la CEDAW linalolenga kumlinda mwanamke na mtoto wa kike.

DSC_01341-1024x681

Mmoja wa wafanyakazi wa Chama cha wanahabari wanawake Tanzania TAMWA akiwakilisha zawadi ya ua kwa Mkurugenzi wao Valerie Msoka baada ya kukabidhiwa tunzo ya umahiri na utambuzi wa kupinga ndoa za utotoni na Ukeketaji nchini Tanzania kutoka nchini Canada.

Amesema serikali itaendeleza jitihada hizo kwa kuhakikisha watoto wa kike hawaolewi katika umri mdogo kwa kulazimishwa kwa kujenga mazingira mazuri shuleni yatakayovutia watoto wa kike kubaki mashuleni, kuongeza hamasa za uelewa wa tatizo na kuhakikisha wale wote wanaohusika na kuwalazimisha watoto wa kike kuolewa Katika umri mdogo wanachukuliwa hatua za kisheria. Lakini pia kuharakisha kubadilisha sharia ya Ndoa ya mwaka 1971 ambayo haimlindi mtoto wa kike chini ya umri wa miaka 18 kuolewa.

“Watoto 2 kati ya 5 hujikuta wako Katika mazingira ya kuozeshwa kwa nguvu kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo kutokuwa na elimu ya kutosha, maisha duni vijijini, umaskini na mila na desturi potofu zinazoendelezwa na baadhi ya makabila na mahari”, amesema Maembe.

Tafiti zinaonyesha kwamba asilimia 39 ya watoto wa kike wenye elimu ya msingi wameolewa katika umri usiotarajiwa chini ya miaka 18 wakati wale wenye elimu ya kutosha wa mjini wameolewa baada ya kufikisha miaka 18.

DSC_02181-1024x681

Mkurugenzi wa mtendaji wa TAMWA akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Chama hicho.

Ndoa za utotoni ni pale mtoto wa kike anapoozeshwa kwa lazima akiwa katika umri chini ya miaka 18 na wakati mwingine yuko shuleni. Madhara yake ni makubwa kwa afya ya mtoto wa kike ikiwa ni pamoja na kupoteza uhai wake na mtoto mwenzake, kukosa maendeleo kimaisha na kuendeleza utamaduni wa kuwa tegemezi na kudumaza fikra na kumfanya kuwa duni Katika taifa.

Katiba ya nchi inamlinda mtoto wa kike kwa kutambua kwamba mtoto ni yule ambaye huko chini ya miaka 18 na hana sifa za kupiga kura. Lakini wakati huo huo Sheria ya Ndoa 1971 inasema mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka 16 anaweza kuoa na msichana mwenye miaka 14 anaweza kuolewa kwa ridhaa ya wazazi.

Sheria hizi mbili zinakinzana na hivyo hazimlindi mtoto wa kike moja kwa moja. “Tutahakikisha kwamba sheria ya ndoa inafanyiwa marekebisho ili iende pamoja na Katiba ya nchi, jitihada zinaendelea kwa kuungana na wanaharakati wote nchini kuleta mabadiliko hasa baada ya kuzindua kampeni ya “Ukanda Huru wa Ndoa za Utotoni” (Child Marriage Free Zone) na Graca Machel.

Tuzo ya CEFM Champion ilishuhudiwa na wadau mbalimbali kutoka serikalini na mashirika yasiyo ya kiserikali, wadau wa kuchangia maendeleo, Umoja wa Kimataifa, waandishi wa habari na wanajamii.

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4816,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: MKURUGENZI WA TAMWA ATUNUKIWA TUZO YA CEFM CHAMPION
MKURUGENZI WA TAMWA ATUNUKIWA TUZO YA CEFM CHAMPION
http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/02/DSC_01311-1024x681-1.jpg
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2015/02/mkurugenzi-wa-tamwa-atunukiwa-tuzo-ya.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2015/02/mkurugenzi-wa-tamwa-atunukiwa-tuzo-ya.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy