Lowassa ajibu maswali magumu yanayomzunguka

WAZIRI Mkuu wa zamani, Edward Lowassa amezungumzia kwa mara ya kwanza sakata la Richmond lililosababisha ajiuzulu wadhifa huo, akisem...



WAZIRI Mkuu wa zamani, Edward Lowassa amezungumzia kwa mara ya kwanza sakata la Richmond lililosababisha ajiuzulu wadhifa huo, akisema alichukua tahadhari katika suala hilo na kuwa ubishi umeligharimu Taifa kulipa Dola za Marekani bilioni 120.

Mbali na hilo, Lowassa ametaka watu waache kumchonganisha na Rais Jakaya Kikwete, huku akimsifu kwa kutekeleza kwa mafanikio Ilani ya Uchaguzi ya CCM.

Aidha, amesema hana mpango wa kukihama Chama Cha Mapinduzi (CCM), na pia ametoa changamoto kwa wanaCCM wanaotaka kuwania urais wapimwe afya zao.

Lowassa aliyasema hayo jana katika mkutano wake na wahariri wa nyombo mbalimbali vya habari nchini uliofanyika nyumbani kwake Area C mjini hapa.

Lowassa aliyejiuzulu wadhifa wake huo Februari 2008, akihusishwa na sakata la Richmond – kampuni ya kufua umeme iliyoletwa nchini mwaka 2006 baada ya kuwapo kwa matatizo makubwa ya nishati ya umeme, alitoa sababu nne za kukaa kimya tangu wakati huo.

Alizitaja kuwa kwa mwanasiasa kukaa kimya pia ni silaha, hivyo aliamua kukaa kimya; kuogopa upotoshaji wa vyombo vya habari, siasa kuwa za uhasama, kusingiziana na kuogopa kuanzisha malumbano zaidi katika jamii.

Kuhusu Richmond alisema ‘zengwe’ hilo limeeleweka nchini kwani limeandikwa sana na kuzungumzwa sana.

“Lakini tunajifunza nini? Walikuja wakubwa wawili hapa Hillary Clinton na Rais Obama (Barack) wa Marekani…wote hawa walisema kuwa mtambo ule ulikuwa state of the art (wa kisasa sana),” alisema Lowassa na kuongeza:

“Kama alivyoeleza Mheshimiwa Mbowe bungeni hivi karibuni, ubishi ule umegharimu bilioni 120 (Dola za Marekani), tulitaka kuvunja mkataba wa Richmond.

“Nikasema wataalamu wasituingize mkenge, nikamwita Mwanasheria Mkuu wa Serikali nikamwambia kuna story hii, be careful. (Anasema iliandikwa na gazeti la The Guardian).

“Baadaye nikaandika kwa maandishi kwa Mwanasheria Mkuu. Halafu kulikuwa na timu ya makatibu wakuu inaongozwa na Bwana Mgonja (Gray). Lakini ubishi wa kisiasa umetugharimu bilioni 120.”

Alisema pia Waziri wa Fedha wakati huo, Zakia Meghji hakutoa fedha zozote kwa kampuni hiyo na kwamba hata Rais alimwambia aliyekuwa Waziri wa Nishati, Ibrahim Msabaha “kuwa makini, vinginevyo utakwenda kujinyonga kwenu Msoga.”

Lowassa aliongeza kuwa asingependa kulijadili suala hilo zaidi, lakini akatolea mfano alipokuwa Waziri wa Maji na Mifugo, alivyoweza kuvunja mkataba wa City Water.

“Chini ya Rais Mkapa tuliweza kuvunja mkataba ule. Tukafanya vikao saa tisa mchana, tukafanya timing ya benki, kisha ili mzungu yule asipate muda, tukampa warrant, saa tisa akampanda KLM kurudi kwao.

“Tulihofia kuwa kama tusingewahi angekwenda kuweka court injections, kwa uzoefu ule wa 1995, tulitaka kuvunja mkataba, lakini nakumbuka rafiki yangu mmoja, Lipumba akasema tutalipa mabilioni, si kweli. Kwa hiyo, wakati ule sikuweza kwa sababu mamlaka hayakuwa kwangu,” alifafanua Lowassa.

Alisema imewachukua Hillary Clinton na Rais Obama kuja nchini kueleza kuwa mitambo ile ni ya kisasa, na ndiyo maana alibainisha kuwa alipojiuzulu alisema ajenda ilikuwa ni Uwaziri Mkuu.

Alipoulizwa nani alikuwa anautaka Waziri Mkuu, Lowassa ambaye ni Mbunge wa Monduli, alisema hilo anamuachia muuliza swali.

Kuhusu uhusiano wake na Rais Kikwete, Lowassa ambaye alisema Jumamosi atatangaza nia yake ya kuwania urais akiwa Arusha, aliwataka watu waache kumchonganisha na mkuu huyo wa nchi.

“Kwa nini urafiki wetu uwe ajenda? Kwa nini mnapandikiza hilo, yeye ni rafiki yangu, achene maneno yasiyo na maana,” alisema Lowassa na kuongeza kuwa hata kama walichukua fomu pamoja mwaka 1995, lakini miaka mingi imepita na muhimu ni kuangalia kama urafiki wao umeshawishi kitu fulani.

Akizungumzia utajiri wake, mwanasiasa huyo alikiri kumiliki nyumba kadhaa (hakuzitaja idadi) na pia anazo ng’ombe kati ya 800 hadi 1,000, lakini akaongeza kuwa anauchukia umasikini na anatamani utajiri.

“Hili ni swali zuri sana, lakini mtashangaa majibu yangu. Namiliki nyumba kadhaa na nina ng’ombe kati ya 800 na 1,000. Na kule kwetu ninakotoka, ili uwe kiongozi lazima uwe na mifugo ya kutosha,” alisema na kuongeza:

“Lakini kama watu wanataka kufahamu utajiri wangu waende Sekretarieti ya Maadili, unalipa kidogo utasoma kila kitu. Lakini ngoja niseme kidogo, natamani utajiri.

“Tuache kuwabeza matajiri, kuwa na matajiri kama Mzee Mengi, Bakhresa, kina Karamagi, ni jambo zuri sana na hawa ni role model, tungekuwa nao 20,000.

“I hate (nachukia) umasikini. Nataka uongozi ili kuwaondoa Watanzania katika umasikini. Kama mtu amepata utajiri kwa njia za uhalali, amejinyima, ni nzuri sana. Nachukia watu wanaopata fedha na kuishia katika ulevi na wanawake. Kina mama mnisamehe. Sitaki kupata uongozi kwa kudanganya, nachukia umasikini.”

Alipoulizwa kuhusu harambee mbalimbali anazozifanya misikitini, makanisani na kwingineko na kuchangia mamilioni ya fedha, Lowassa alizitetea harambee hizo na kueleza kuwa fedha zinachangwa na marafiki zake.

“Zile sio fedha zangu, kwa mfano kule Arusha juzi, zilichangwa milioni 200, watu wamesema nimechangia shilingi milioni 200, hapana. Mimi na marafiki zangu wa Arusha, Dar na kwingineko tumechanga shilingi milioni 100, Makamu wa Rais amechangia shilingi milioni 10,” alieleza Lowassa na kuongeza:

“Kuchangia misikitini, makanisani na katika maendeleo ni jambo zuri, kwa wenzetu wa Kenya harambee ndio kila kitu. Nawashauri viongozi na wabunge kwenda vijijini kusaidia maendeleo kwa njia ya harambee.

“Hili la shule za kata ambalo ni mawazo ya CCM na maelekezo ya Rais, limefanikiwa kwa nguvu za Serikali na wananchi, kwa hiyo harambee zinafaa.”

Kuhusu afya yake, alisema yuko fiti na ni upuuzi kusema kuwa ni mgonjwa, na akatoa changamoto kwa wanaCCM watakaojitokeza kuwania urais, wakapimwe afya zao.

“Nimetembea pale Dar kilometa tano, wakasema siwezi kukimbia hata kilometa 100 na kuwa nimepelekwa Ujerumani kutibiwa. Huu ni upuuzi, ni chuki kutakiana mabaya. Niko fit and kicking. Fit kwa chochote kile.

“Tukapimwe afya zetu kujua nani mgonjwa, tutakutana kwenye uwanja wa mapambano, na I will beat them by far (nitawashinda kwa mbali).”

Alipoulizwa kama asipoteuliwa na CCM kuwania urais, atahama chama hicho, tawala, Lowassa alisema hana mpango B katika hilo, na CCM ni haki yake.

“Sina mpango wa kuhama. Nimeingia CCM mwaka 1977 na sijawahi kutoka katika majukumu yake zaidi ya pale nilipokuwa Mkurugenzi Mtendaji wa AICC.

“My right is CCM (haki yangu ni CCM), sio kwa hao kina kadeti. Huyo ambaye hanitaki CCM ndio ahame. Hakuna mpango B, nina mpango A na naamini utafanya kazi.”

Aidha, akizungumzia kuhusu madai kuwa akiwa Rais atalipiza kisasi, Lowassa alisema yeye ni Mkristo, na imani yake inamtaka kusamehe mara 70, hivyo hatalipa kisasi, moyo wake ni mweupe na yaliyopita yamepita.

Akitoa maoni baada ya kuulizwa kuhusu chama chao CCM, Lowassa alisema hakipaswi kubweteka kwani upinzani umepata nguvu sana mijini na vijijini.

“Tusibweteke wenzetu wamejiandaa, na mkiondolewa hamrudi madarakani, angalia KANU, UNIP na vinginevyo. Lakini faida kubwa ya CCM ni kuwa Rais Kikwete ametekeleza vizuri sana Ilani, hii ndio kete yetu, jamaa mmoja alisema mtaji wetu, lakini isitubweteshe, tutatue matatizo ya wananchi na watu wahimizwe kujiandikisha kwa wingi,” alibainisha mwanasiasa huyo.

Lowassa ambaye baadhi ya maswali aliyajibu juu juu au kukataa kuyajibu kwa kuwa alisema yapo katika hotuba yake ya Jumamosi mkoani Arusha, alisisitiza suala la elimu kuwa kipaumbele namba moja na pia tatizo la ajira kama bomu lisiposhughulikiwa ipasavyo.

Kuhusu ajira, alisema chama chochote kinachotaka kushika madaraka, lazima kizungumzie ajira na jinsi litakavyotengeza fursa hizo, akitoa mfano wa uchaguzi wa karibuni wa Uingereza kati ya David Cameroun na Ed Milbrand na pia Obama alipoingia madarakani.

Aliwataka Watanzania walifikirie hilo kwa umakini.

Katika elimu, alisisitiza kuwa kwake kipaumbele cha kwanza, cha pili, cha tatu ni elimu, na kwamba nchi ikiwekeza vizuri kielimu, itasonga mbele kiuchumi.

Alisema elimu nchini imeparaganyika na hakuna budi kusakwa jibu la maarifa kwani imefikia mahali watu wanawachukia Wachina kwa sababu wanakuja na kuajiriwa kama walinzi Kariakoo.

Lowassa alipoulizwa kama angekuwapo serikalini hadi sasa na akaomba kuwania urais, alisema: “Naamini kwa kasi ile, ningepunga mkono, na kuzoa kura zote. Lakini nasikitika hatufanyi maamuzi, yawe mabaya au mazuri. Rais amefanya kazi nzuri, lakini hatukupaswa kuachwa nyuma na Waganda, Wanyarwanda.”

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4816,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: Lowassa ajibu maswali magumu yanayomzunguka
Lowassa ajibu maswali magumu yanayomzunguka
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg48WJGDDcSM5ULyKLqCUraZIMLsd4HLp8Dqz9pP4r1858drCgK_c19EAD8KXSt0TVvng4nu3KMNrFDqMO5WqsKbkQHbDbizoZ6pFjtHcAP1_WBAA8Vfw_KkYSnYhqMLh7kyDz9tDoPdBU/s320/edward-lowassa.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg48WJGDDcSM5ULyKLqCUraZIMLsd4HLp8Dqz9pP4r1858drCgK_c19EAD8KXSt0TVvng4nu3KMNrFDqMO5WqsKbkQHbDbizoZ6pFjtHcAP1_WBAA8Vfw_KkYSnYhqMLh7kyDz9tDoPdBU/s72-c/edward-lowassa.jpg
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2015/05/lowassa-ajibu-maswali-magumu.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2015/05/lowassa-ajibu-maswali-magumu.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy