Ikiwa leo ni siku ya mwisho kwa wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kurudisha fomu kwa ajili ya mchakato wa kuteuliwa kupeperusha be...
Ikiwa leo ni siku ya
mwisho kwa wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kurudisha fomu kwa ajili ya
mchakato wa kuteuliwa kupeperusha bendera ya chama ni wanachama 33 wamefanikiwa
kurudisha fomu hizo makao makuu ya CCM.
Jumla ya wanachama 42
walichukua fomu hizo ambapo walitakiwa kuwa na wadhamini 450 ambao watapatikana
katika mikoa 15 ikiwemo mikoa mitatu ya Zanzibar.
Ni wanachama tisa
waliobaki ambapo wanatakiwa kurejesha fomu hizo ambapo mwisho wake ni saa 10
kamili jioni.
Wagombea hao ni Waziri wa
Mawasiliano Sayansi na teknolojia, January Makamba, Mbunge wa Sengerema William
Ngeleja, Godwin Mwapongo, Balozi Patrick Chokala, na Peter Nyalile.
Wengine ni Ritha Ngowi,
Helena Elinewinga, Anthony Chalamila and Sonoko Banda. Hata hivyo katibu wa
Sekteratieti Organaizesheni wa CCM,
Mohamed Seif Khatib alisema hakuna adhabu kwa mtu ambaye atashindwa kurudisha
fomu.
Miongoni mwa wanachama
waliorudisha fomu jana ni Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa.
Lowasa alisema
amedhaminiwa na wadhamini 879,000 na kutaka wote wanaomtuhumu kwa ufisadi
kuacha mara moja.
Alisema ikiwa atateuliwa
kuwa Rais atahakikisha anatumia raslimali zote kwa faida za Watanzania.
Alisema kwa bahati mbaya
watu ambao wanakosa hoja, wamekuwa wakiwatuhumu wenzao kwa vitu ambavyo havina
ukweli wowote.
“Nataka nitumie nafasi
hii kwa wale wote ambao wamekuwa wakinituhumu kwa miaka kadhaa sasa na
kunihusisha na suala zima la rushwa kuwaambia waache mara moja kwani hakuna
hata chembe ya ukweli wa maneno hayo” alisema.
Alisema kwa yeyote mwenye
ushahidi wa tuhuma hizo za kipuuzi, autoe, aeleze kwa ushahidi rushwa yoyote
inayomhusu.
“Aseme nimechukua rushwa
lini, kwa nani, kwa lipi na kwa kiasi gani” alisema Pia alisema tofauti na
maeneo yanayosemwa kwamba amehonga hakuna mdhamini yoyote aliyehongwa.
“Hayo ni maneno ambayo ni
upuuzi tu na wanaonituhumu kwa ufisadi waache mara moja.” Alisema.
Alisema majungu kwake
sasa yametosha na ikiwa atateuliwa basi ataongoza nchi kwa haki.
Alisema maelfu ya wana
CCM walijitokeza kumdhamini katika mikoa
yote aliyofika .
“Mafanikio haya ya awali
ni ishara njema kuelekea hatua zilizobaki na kwa uwezo wa mwenyezi Mungu na kwa
ushirikiano kwa pamoja tutavuka daraja ili hatimaye kuwatumikia kwa utumishi
uliotukuka nikiwa Rais wa awamu ya tano” alisema.
Alisema ana shahuku kubwa
kuunganisha uwezo wa kila Mtanzania katika kupambana na umaskini wa
nchi,umaskini wa watu siyo amri ya Mwenyezi Mungu kwani kwa pamoja raslimali
tulizonazo kwa bidii,
maarifa na ufanisi zaidi
ili kuutokomeza umaskini.
“Ni lazima sasa tufike
mahali tuseme imetosha, majungu yametosha, upotoshwaji umetosha, rushwa
imetosha na kwa pamoja tunaweza kukomesha haya, tutayakomesha kwa kusimamia
ukweli, uadilifu, uaminifu na kutenda kwa haki” alisema.
Hata hivyo waandishi wa
habari hawakupewa nafasi ya kumuuliza maswali kutokana na muda aliokuwa
ametengewa kuisha.
Dk Asha Rose Migiro
Mwanachama mwingine
aliyerudisha fomu jana ni Dk Asha-Rose Migiro ambaye alisema hayuko tayari
kuzungumza na waaandishi wa habari.
Eldefonce Bilohe
Pia Mkulima kutoka
Kigoma, Elfonce Bilohe naye alirejesha fomu akikishukuru chama kwa demokrasia
iliyoionyesha.
Bilohe alisema hayo
wakati akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kurudisha fomu.
Alisema yeye ni mkulima
lakini amepata nafasi ya kushiriki katika kinyang'anyiro hicho kitendo ambacho
kweli kimeonyesha kuwa ni chama cha wakulima na wafanyakazi.
Akizungumzia zoezi la
kutafuta wadhamini amesema limeenda vizuri na amekabidhi idadi ya wadhamini
waliohitajika kutoka katika mikoa 15 kama chama kilivyotaka.
Alisema alikutana na
changamoto ya kuombwa rushwa.
“Changamoto kubwa sana
ambayo nimekutana nayo katika kuwapata wadhamini ni baadhi ya watu kuniomba
kitu kidogo kama maji ya kunywa” alisema
Waziri Nyalandu
Mwingine wa CCM
aliyerudisha fomu jana ni Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu .
Akizungumza na waandishi
wa habari alisema ana imani na Watanzania na yupo tayari kuhakikisha CCM
inashika dola mwaka 2015.
Alisema kila alipokuwa
akipita ameona watu wakiwa na mapenzi makubwa na chama chao na hiyo ni ishara
kuwa bado wana imani na chama chao. Akizungumzia kuhusu umoja uliopo katika
Taifa alisema alisema kuwa ni lazima
kuhakikisha tunu hiyo inalindwa na kuenziwa na kusisitiza kuwa
ni lazima kupiga vita
ubaguzi wa aina yoyote.
Luhaga Mpina
Kwa upande wake mbunge wa
Kisesa Luhaga Mpina alisema ametembelea mikoa
17 na kusema zoezi lililenda vizuri.
Alitoa ushauri kwa CCM
kuweka mdahalo kwa wagombea wote wa nafasi ya urais ili kujua nini ambacho
watakifanya kwa Watanzania.
kusema kuwa hana presha
na wagombea 42 ambao wamekwishachukua fomu na anaamini kuwa itashinda.
Alisema anaamini jina
lake litakuwwepo katika tatu bora kwa wale watakaoteuliwa na chama.
Malick Malupu
Mwanachama mwingine
aliyerudisha fomu ni Malick Malupu, mwanafunzi wa shahada ya uzamili ya
utumishi wa umma Chuo kikuu cha mzumbe alirudisha fomu aliwataka wagombea wenzake kuwa
makini na wapambe wao
kwani wanaweza kusababisha mtafaruku au mgongano
baina yao.
Alisema kama kuna mtu
anamuabudu mgombea aachane na chama.
“Ukiona mtu anakatwa jina
lake akalalamika ujue ameingia kwa hujuma au kwa njia ya ubatili pamoja na
kutoa rushwa” alisema
Dk Hamisi Kingwangala
Mbunge wa Nzega Dk Hamisi
Kingwangala naye alirudisha fomu na kusema amefanikiwa kupata wadhamini kama
ilivyo agizo la chama. Alisema atahakikisha anashughulikia suala la rushwa na
ufujaji wa fedha za umma.
Hadi taarifa hii
inaandikwa wagombea ambao wamerudisha fomu na wanasuburi kuingia kwenye
mchakato wa kuteuliwa kupeperusha bendera ya CCM katika uchaguzi mkuu wa Rais
Oktoba 25, mwaka huu ni Waziri wa Uchukuzi, Samwel Sitta, Makamu wa Rais Dk
Mohammed Gharib Bilal, Makongoro Nyerere, Waziri wa Ujenzi Dk. John Magufuli,
Waziri wa Kilimo na Ushirika Stephen Wassira, Balozi Ali Abeid Karume, Waziri
wa Mifugo Dk Titus Kamani na Boniface Ndengo,
Wengine mi Waziri wa
Mambo ya Ndani ya Nchi Mathias Chikawe, Profesa Sospeter Muhongo, Balozi Amina
Salum Ally, Jaji Mkuu Mstaafu Augustino Ramadhani, Leonce Mulenda, Waziri asiye
na Wizara maalum Profesa Mark Mwandosya, Waziri Mkuu Mizengo Pinda Pia wamo
Waziri wa Afrika Mashariki Dk Harrison Mwakyembe, Waziri Mkuu mstaafu Frederick
Sumaye na Waziri Mkuu aliyejiuzulu Edward Lowassa.
Wengine ni Waziri wa
Katiba na sheria Dk Asha Rose Migiro, Monica Mbega , Dk Mwele Malecela, Waziri
wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, Waziri wa mambo ya nje na Ushirikiano
wa Kimataifa Bernard Membe, Naibu Waziri
wa Fedha Mwigulu Nchemba.
Wengine ni Mbunge wa Nzega, Mbunge wa Nzega
Dk. Hamis Kigwangala, Dk Hans Kitine,
Balozi Augustino Mahiga,na mkulima kutoka kijiji cha Mjimtala Kasulu
Kigoma, Eldefonce Bilohe,
Pia Mbunge wa Kisesa
Luhaga Mpina, Amos Siyantemi, Mwanafunzi wa Chui Kikuu Mzumbe, Amos Robert na
Maliki Malupu.
Source: Sifa Lubasi,
Dodoma
COMMENTS