Mzee Machano akiwa na mwandishi wa makala haya Mimi nilikuwapo kwenye kutengeneza banda la fete pale Kisiwandui na nilikuwepo kwenye...
Mzee Machano akiwa na mwandishi wa makala haya |
Mimi nilikuwapo kwenye kutengeneza banda la fete pale
Kisiwandui na nilikuwepo kwenye doria wakati Sheikh Karume akitangaza mapinduzi
katika kituo cha radio pale Rahaleo, anasema
mzee Machano Mjomba Machano akiwa ameegemea ukuta pale nyumbani kwake
Gamba Mabatini, kiasi cha kilomita 25 kutoka Malindi.
Mpango wa fete uliokuwa umebuniwa na Chama cha Afro Shiraz
ulilenga sana katika kuondoa mashaka ya serikali ya Sultani na vyombo vyake na
kuwawezesha vikundi vya wanamapinduzi kuingia mjini na kutekeleza kazi yao.
Fete na mkutano ulilenga kuweka sawa mambo ambayo yanahitaji
usiri mkubwa.
Mzee Machano anasema alikuwa na kundi kubwa ambalo
analikumbuka kutoka katika jimbo lake ambalo lilishiriki moja kwa moja kama
viongozi wa vijana walioshiriki mapinduzi kutoka katika maeneo hayo.
Anamkumbuka Nasoro wa Donge , ambaye aliwaongoza wenzake
kwenda kwa miguu katika fete iliyowezesha usiku watu kuanza kazi ya kuvamia na
kushika maeneo muhimu. Wengine ambao aliwakumbuka wazi ni Ahmed Ameir, Kinyeshi
na haji mabunduki wa Kidoti.
Ukiwa mvumilivu unaweza kupata faida kubwa katika mazungumzo
na mzee huyu ambaye kama serikali ingelifanya juhudi kidogo ya kupima umri
wake, ni lazima ingelikuwa, sherehe kubwa kwa taifa kuwa na mtu mwenye umri
mkubwa anayeweza kuingia katika vitabu vya rekodi za dunia.
Kuwepo kwa rekodi sahihi ya Mzee Machano Mjomba Machano kwa
kuwa na matokeo ya vipimo kama vya skana (MRI) tungekomesha maneno ya watu
kwamba ukiwa katika nchi zinazoendelea huwezi kukatisha zaidi ya miaka 120 na
kutoa fumbo kubwa kwa ushiriki wake wa kwenye mapinduzi akiwa na umri mkubwa.
Kwenye mazungumzo yangu na mzee huyu niliyofanya hivi karibuni
nilifurahishwa sana jinsi anavyoelezea ushupavu, ushujaa wa kizazi chake katika
kufanikisha mapinduzi ya Zanzibar yaliyompa heshima Mwafrika baada ya
kudhalilika kwa kipindi kirefu.
Mwafrika katika visiwa vya Unguja alidhalilika kwa namna
tofauti kuanzia kipindi cha warenjo, waarabu na usulutani wao na Waingereza
waliojichukulia mamlaka ya kutawala visiwa na kasha kuwageuka waafrika kwamba
hawawezi kujitawala na kula sahani moja na sultani kuwapandisha Hizbu kwenye
chati.
Ni nadra sana kupata taarifa
za undani za mapinduzi hayo, kutokana na wengi walioshiriki moja kwa
moja kutangulia mbele za haki na kutokuwapo kwa taarifa za kutosha kuhusiana na
maandalizi na utekelezaji wa shughuli hiyo nzito, mtu mwenye masimulizi japo
kidogo ni Sheikh Thabiti Kombo Jecha.
Lakini unapokutana na mzee huyu akakusimulia jinsi watu
walivyotoka kwa wingi katika maeneo ya makodeni na hata katika jimbo hilo
ambalo ni la Chama cha Mapinduzi likiwa pia na uasili wa Afro Shiraz unajikuta
ukiuma meno kwa ushujaa wa kukataa uhuru bandia wa mwaka 1963 na kasha
kutengeneza mapinduzi yaliyorejesha heshima kwa mwafrika.
Pamoja na vizuizi vingi walivyowekewa na utawala wa sultani
kwa wakazi wa makodeni na shambani kutoshiriki pamoja na kwenda mjiini, akili
pevu ya kamati kuu ya ASP ambayo tangu
mkutano wa pili wa kutengeneza katiba London, walkiona hawana chao kwa jinsi
mambo yalivyokuwa yakisukwa, viongozi wa ASP mashambani waliendelea kunoa
vijana wao kukataa udhalilishaji mpya wa mwaka 1963.
Watu wengi wameandika kinyume na mapinduzi ya mwaka 1964, na
waandishi pamoja na maandishi yao ya kupinga na kulaani ni wale wenye uwezo
waliopokonywa tonge mdomoni baada ya sultani
kulazimika kukimbilia baharini na baadae Dare s salaam kwenye hifadhi ya
Mwalimu Nyerere akiwa njiani kwenda Uingereza.
Mzee Machano anasema japo yeye hajui kusoma na kuandika na
kwamba mapinduzi yalitokea akiwa na umri wa takribani miaka 70 amesema kwamba hasira za Wazanzibari weusi za
kunyimwa madaraka katika uchaguzi kwa njia ya voti, zilipoozwa na mafanikio ya
mapinduzi yaliyopangwa kwa usiri wa kutosha.
Anasema kabla ya mapinduzi yeye alikuwa anaongoza branchi
mbili za Kidoti na Tazari kabla ya Kidoti kukabidhiwa Haji mabunduki na kwamba
mafunzo ya mapinduzi yalifanyika kwa haraka.
Nilipata nafasi ya KMumuuliza John Okello na katika jibu lake alisema kwamba ni mtu aliyeingizwa
katika mapinduzi kusaidia kufunza watu na kuwaelekeza namna nzuri ya kufanya
mapinduzi bila kuwa na silaha za moto kwa kutumia marungu na mikuki.
Anasema katika mazungumzo kwamba Okello si mzanzibari bali
alikuwa mganda ambaye alikuwa anajua vyema medani na alifanya kazi njema ya
kufunza wazazibari namna ya kuendesha mafunzo hayo.
Wilaya ya kaskazini A katika mkoa wa Kaskazini Unguja ni
sehemu ambayo waafrika wengi wenyeji wa tumbatu na Paje wanaishi na ambao
mchango wao katika ufanisi wa mapinduzi ya Ungtuja si haba.
Baada ya Kamati kuu ya ASP kutambua kwamba hawana cha kufanya
zaidi ya kutwaa nchi kwa nguvu wakaanza kufanya maandalizi kwa kuwa uanzishaji wa vikundi ambapo juu yake muongozaji alikuwa Sheikh
Karume mwenyewe.
Kwa upande wake mzee Machano anakumbuka wajumbe wa baraza la
apinduzi akina Hamis Haji, Wagu, Nyangemse , Mwadini Ally na Musahaji.
Ingawa mtoto wake ambaye alikuwapo alisema kwamba haoni kama mzee wake
alifaidika na masuala ya siasa. Machano
anasema alianza kushiriki siasa kwenye mikaka ya 1930 wakati waafrika
walipoanza kuwa pamoja kutafuta nafuu ya mambo yao kufuatia kubanwa na mataifa
mengine kama waarabu na wahindi.
Wakati Afro Shiraz Party (ASP) ilipoanzishwa alikuja kuwa mtu wa kutegemea
katika eneo lake la Kaskazini ambalo kwa sasa ni jimbo la Mkwajuni.
“ Hapa katika eneo lote hili la Gamba , mzee anaheshimika sana
lakini kama unavyoona alivyo na eneo analokaa, na bado anaipenda CCM yake kama
alivyoipenda ASP” alisema Musa Machano Mjomba ambaye ni mtoto wake wa pili
kutoka mwisho.
Anasema Mzee wake baada
ya kushiriki mapinduzi ya mwaka 1964 alirejea gamba mabatini na kuishi hapo
akiendelea na nmaisha yake ya useremala na kulima muhogo na mpunga.
Hata hivyo katyika maisha yake pamoja na kusimuliwa na mzee wa
ke kuhusu mapinduzi na ushiriki wake wa karibu sana, hajawahi kuona
wanamapinduzi wengine wakienda kumjulia hali mzee huyo ambaye eliumu dunia
ambayo ingelimwezesha kusoma kuandika na kuhesabu hakuweza kuipata.
Anawakumbuka watu wengi akiwamo Thabiti Kombo Jecha ambaye
anasema wakati wakiwa viongozi vijana yeye alikuwa mzee na walikuwa wakitumia
makazi yake kwa shughuli mbalimbali zinazohusu siasa za kupigania uhuru na hadi
mapinduzi.
“Mimi naona kama mzee wamemtenda vibaya, ni mzalendo lakini
naona anaishi maisha ya shida. Mzee aliyepigania nchi hii anaishi kwa
shida.” Anasema Mussa ambaye anasema
haoni faida ya ushiriki wa baba yake katika mapinduzi kwani wengine waenziwa
yeye anataabika.
Huenda ni kweli kwani makazi ya mzee huyu hayana hadhi hata
kidogo hata kwa mtu wa kawaida, mtoto wake anasema anahitaji milioni moja
kurekebisha eneo analokaa mzee wake, ni hela ndogo lakini mwalimu wa skuli hana uwezo huku ikifikiriwa wazi ni lazima
ahakikishe mzee wake katika umri mkubwa vile anapata chakula na nguvu za kuendelea
mbele.
mwisho
COMMENTS