Bayport yajivunia miaka 10 ya kutoa huduma ya mikopo nafuu ya kifedha Tanzania

  Dar es Salaam, 21 st   October 2016 –  Taasisi inayoongoza Tanzania kwa kubobea katika kutoa mikopo nafuu, Bayport Financial Se...



 Dar es Salaam, 21st  October 2016 –  Taasisi inayoongoza Tanzania kwa kubobea katika kutoa mikopo nafuu, Bayport Financial Services katika kipindi cha miaka 10  iliyopita  imechangia kwa kiwango kikubwa  katika kuboresha maisha ya maelfu ya Watanzania kupitia  utoaji wa mikopo.
 Bayport Tanzania ni miongoni mwa taasisi tanzu kumi za Taasisi ya Bayport Group ambayo hutoa ufumbuzi wa kifedha  kwa watu binafsi walioko katika ajira rasmi au waliojiajiri ndani ya soko linaloibukia. Huduma zinazotolewa na taasisi hiyo  zinaboresha ujumuishwaji kifedha  kwa watu ambao hawana uwezo wa kuzifikia  huduma za kawaida za kibenki  au walio na kiasi kidogo cha fedha katika benki.
Baada ya kuanza shughuli zake  nchini Zambia mwaka 2001, shughuli za Bayport  kwa hivi sasa zinaendeshwa katika nchi saba barani Afrika na  nchi mbili ndani ya Amerika Kusini. Nchi hizo ni Zambia, Uganda, Ghana, Tanzania, Botswana, Afrika Kusini, Msumbiji, Colombia, na Mexico.
 Hivi sasa Bayport  imekuwa ni msingi wa kuaminiwa na mteja ikiwa na  takribani wateja 518,000 ambao  kila mara wamekuwa wakipata  na hata na kufurahia huduma inazozitoa.  
 Kwa mujibu wa Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bayport Tanzania, John Mbaga, Bayport imeshatoa  zaidi ya  shilingi bilioni 48 katika kipindi cha mwaka wa fedha 2015 peke yake. Kwa upande mwingine Bayport inachukuliwa kuwa ni ‘mlipa kodi mkubwa’  nchini Tanzania  ikiwa  imelipa  zaidi ya shilingi bilioni 7 kwa mwaka wa fedha 2014.

“Matamanio yetu ni  kuboresha maisha ya  wateja wetu  na kuwapa fursa  ambazo zitawanufaisha  sio wao peke yao bali pia  watoto wao na kizazi kijacho,” alisema Mbaga  katika mazungumzo yake na wanandishi wa habari hivi karibuni.
Aliongeza, “Tunawasaidia kwa kuangalia unafuu utakaotokana na  mtiririko wa fedha katika kipindi kifupi ambapo matokeo yake  husaidia familia katika kuongeza na kuwa na ustawi wa kifedha  wa kudumu.”
 Bayport Tanzania  ilianzishwa mwaka 2006, na kwa haraka  imekuwa ni  mtoaji wa mikopo kwa wafanyakazi katika sekta za umma na binafsi. Kuwepo kwa ofisi zake 83 za kudumu na matawi 45 ya muda  kumeifanya  kufika kila mkoa kwa Tanzania Bara.
 Kampuni hii ina wafanyakazi wa kudumu 300 na mtandao wa mawakala wa mauzo zaidi ya 1000.
 “Kazi ambazo tumekuwa tunazitoa zimechangia kupunguza ukosefu wa ajira kwa vijana hapa nchini,” anasema Mbaga.
 Kwa mujibu wa utafiti wa Ujumuishaji wa Nguvu Kazi (Integrated Labour Force Survey 2014), kiwango cha ukosefu wa ajira  nchini Tanzania kilikuwa  ni asilimia 13.7.
 Mbali na kutoa mikopo, mambo mengine ambayo Bayport inajishughulisha nayo  ni pamoja na  bidhaa za bima kama vile Sera ya Ulinzi Kielimu ambayo inashughulikia utegemezi wa ada katika elimu kwa muda wa hadi miaka mitatu katika iwapo kwa bahati mbaya mwenye bima  hiyo atafariki. Sera ya Bima ya Maisha ya Bayport inahusisha kulipia salio lililobakia  iwapo wateja watapunguzwa kazi, watakuwa wamepata ulemavu, watafariki au  kupatwa na maradhi kama vile saratani.
 Hivi karibuni Bayport ilizindua  aina ya mikopo kwa ajili ya nyumba ambayo inawawezesha  wateja  kumiliki kiwanja kilichopimwa. Bidhaa hiyo inawezesha Bayport kuifikisha mikopo yake kwa mkopaji kwa  kutumia  kiwanja kilichopimwa kama dhamana.

Akizungumza kuhusu sera ya Bayport kuhusu  kuwajibika kwa huduma za kijamii, Mbaga alisema  kwamba elimu ndio kipaumbele chake. “Kupitia mkakati wa ‘Badilisha Maisha’ tumeshafanya ukarabati wa  madarasa katika shule kadhaa, kutoa msaada wa madawati, kutoa udhamini wa masomo kwa  wanafunzi wa vyuo vikuu pamoja na kutoa msaada wa vitabu. Tangu mwaka 2006, tumetoa misaada ya moja kwa moja kwa wanafunzi 1,500 wa shule za msingi na sekondari.”
 Bayport pia inawasaidia watoto yatima. Mradi wa mfano unajidhihirisha kwa kuisaidia shule ya watoto yatima inayodhaminiwa na Mfuko wa Fursa kwa Wote (EOTF) ambapo Bayport imeboresha  shule hyo ya awali kuwa katika viwango vya kisiasa.
Uwekezaji wa shilingi milioni 200 uliofanywa na Bayport umewezesha kuwepo kwa mazingira rafiki  ukiwepo mwanga wa asili na sehemu asilia za kupitisha hewa kwa ajili ya watoto 40 wanaohudumiwa akatika kituo cha EOTF  na wengine 60  kutoka katika vijiji jirani wakinufaika.
 Akiangazia kuhusu safari ya miaka kumi ya mafanikio katika biashara hapa nchini, Mbaga anasema  kwamba Kampuni hiyo  inajivunia kukua kwake  na kukomaa  ambako imeweza kufikia katika kipindi cha mwongo mmoja uliopita. “Tunasherehekea  fursa hii na  uwezo wa kuleta mabadiliko katika maisha ya wateja wetu, wadau, wafanyakazi na jumuia katika maeneo  tunakoendesha shughuli zetu.”
 Alidokeza kuwa dira ya kimkakati ya taasisi hiyo na utekelezaji wake uliokwishafanyika umejikuta ukipata msaada kutoka kwa wawekezaji, miongoni mwao  ni kampuni ya uwekezaji wa Sweden  ya AB Kinnevik. Julai 2010 kampuni hiyo iliwekeza  dola milioni 40 katika Bayport Group na hivyo kuwa taasisi pekee yenye hisa nyingi ndani ya Bayport.
 Miezi minne baadaye Bayport ilitoa kwa mara ya kwanza katika masoko ya madeni ya mitaji kimataifa  kwa kukusanya jumla ya  dola milioni 100.

“Mwaka 2016 uongozi wa Bayport  uilifikia  dola milioni 250  ikiwa ni uwezo wa salio kubwa  kupatikana kutoka Shirika la Uwekezaji Binafsi Ng’ambo (Overseas Private Investment Corporation-OPIC), ambayo ni  taasisi ya maendeleo ya fedha ya serikali ya Marekani. Mkopo huo wa muda mrefu utasaidia ujumuishwaji wa kifedha  wa taasisi na ajenda yake ya kukua  katika  shughuli zake zote. Kama taasisi tanzu ya Bayport, Bayport Tanzania  inachangia katika historia ya uwekezaji wa taasisi na faida zinazotoka ndani yake.”
 Kwa mujibu wa Mbaga mkakati wa kibiashara wa Bayport upo katika mabadiliko ya bidhaa  na ubunifu wa kiteknolojia  na ‘watu wakiwa ndio nguzo yetu kuu’.
 Ndani ya mkakati huo wa taasisi, Bayport Tanzania mwaka 2015 utambulisho wake ulipata chapa mpya  ikiwa na ujumbe uliojikita kwa watu, na hivyo kuipa taasisi  fursa ya  ya  kujiweka tena yenyewe katika  mtoaji wa ufumbuzi wa kifedha.
“Bidhaa yetu mpya haikuanzishwa katika hali ya upweke. Iliibuka ndani ya falsafa yetu ya kibiashara ambayo inaitwa ‘The Bayport Way”, Mbaga alifafanua  na kuongeza, “Falsafa hiyo  inahusu mambo yote  ya namna tunamchukulia mteja, awe ni mwajiriwa, mteja au mwekezaji, na jinsi ambavyo tunaongeza thamani  katika maisha yao.”
 Kama taasisi Bayport inaamini  kwamba mikopo ni nyenzo yenye nguvu inapotumiwa kistaarabu na katika mazingira yaliyo na ufanisi. “Hakuna kinachotufanya kama pale ambapo tunapowaona wateja wetu  wakiitumia mikopo katika matumizi chanya na kuendesha shughuli za kiuchumi ambazo kimsingi  zinaboresha maisha yao,” Mbaga alisema.
 Ofisa Mtendaji Mkuu huyo aliwashukuru wateja wa Bayport Tanzania, wafadhili, serikali na wadau wengine  kwa kuiunga mkono taasisi hiyo  bila kuchoka  katika kipindi chote cha miaka kumi.
Alisema, “Imekuwa  ni safari ya kuvutia iliyojaa mafanikio. Bila wadau wetu hawa hatungaweza kufikia hatua hiii. Nawahakikishia  kwamba Bayport Tanzania  inaimarika kila mwaka. Wakati tunaelekea katika mwongo mwingine  tumejipanga na tumejikita katika kufanikiwa  hata katika viwango vya hali ya juu vya ufanisi katika kutoa  kutoa bidhaa zisizo na ushindani nchini Tanzania.”

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4816,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: Bayport yajivunia miaka 10 ya kutoa huduma ya mikopo nafuu ya kifedha Tanzania
Bayport yajivunia miaka 10 ya kutoa huduma ya mikopo nafuu ya kifedha Tanzania
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjiywFBcFgnBbwwaXRrR0xSrK6Cc51fAp5XUmN70MSn__LagoFgAn3tWVRbroWoFGNj2vUg_dnypQg4eMZySF04PMFVt8-rt5COrZAm6CmEm4LEFVhHHi6i1boOJJfZCA876E33p8ybaK8/s640/CEO+Mbaga+Bayport.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjiywFBcFgnBbwwaXRrR0xSrK6Cc51fAp5XUmN70MSn__LagoFgAn3tWVRbroWoFGNj2vUg_dnypQg4eMZySF04PMFVt8-rt5COrZAm6CmEm4LEFVhHHi6i1boOJJfZCA876E33p8ybaK8/s72-c/CEO+Mbaga+Bayport.JPG
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2016/10/bayport-yajivunia-miaka-10-ya-kutoa.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2016/10/bayport-yajivunia-miaka-10-ya-kutoa.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy