Je ulisikia mdahalo huu...wa uwezeshajui vilabu kama hapana soma muhtasari huu nawe ujipambanue

MUHTASARI WA KONGAMANO LA MABADILIKO YA UENDESHAJI WA KLABU ZA SOKA TANZANIA Kongamano la mabadiliko ya uendeshaji wa klabu za soka l...

MUHTASARI WA KONGAMANO LA MABADILIKO YA UENDESHAJI WA KLABU ZA SOKA TANZANIA

Kongamano la mabadiliko ya uendeshaji wa klabu za soka limefanyika Jumamosi Oktoba 22, 2016 kwenye ukumbi wa Uwanja Mkuu wa Taifa, Dar es Salaam.
Kongamano hilo lililoandaliwa na chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzani (TASWA) lilishirikisha wadau zaidi ya 60 nchini.
Kituo cha televisheni cha Azam kilionesha live (mubashara) kongamano hilo huku wajumbe wakikubaliana masuala kumi ya msingi.
Kwanza wajumbe walikubali kuwa kuna umuhimu wa kufanya mabadiliko sasa kwa sababu muundo unaotumika kuendesha klabu za soka una matatizo mengi.
Pili iliamuliwa klabu zijiandae vya kutosha kukaribisha mabadiliko hayo ikiwa ni pamoja na kuboresha utawala bora (governance) kwenye uendeshaji wa klabu.
Tatu mifumo yetu kama nchi inawezesha klabu kuwa na aina nyingi za mifumo ya kiuendeshaji hivyo wanachama waelimishwe kwa kina kuhusu mifumo hiyo ili wachague ulio bora zaidi kwa manufaa ya klabu zao.
Nne ili mabadiliko haya yafanyike kwa haki, inatakiwa wamiliki wa timu hizi (wanachama) waelimishwe  vya kutosha juu ya thamani yao ili wajitambue. Kwamba thamani ya klabu kubwa nchini haiwezi kulinganishwa na kiasi cha fedha kinachotolewa na wawekezaji hivyo wanachama wasiingie kwenye mabadiliko wakiwa wanyonge kwa sababu wao ndio wana mtaji mkubwa kuliko hela zinazoletwa kwa ajili ya uwekezaji.
Tano mabadiliko haya hayawezi kufanywa na wanachama na wawekezaji pekee bila kuishirikisha serikali. Hivyo klabu zinapojipanga kwa mabadiliko haya zihakikishe zinashirikisha serikali na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Sita mabadiliko haya yasifanywe kishabiki bali yafanywe kitaalamu ili  kutengeneza msingi Imara utakaoepusha migogoro hapo baadaye.
Saba kuelekea mabadiliko haya, hasa katika kipindi hiki ambacho uelewa wa wanachama ni mdogo, serikali inatakiwa kulinda maslahi ya walio wengi kwa kuingilia kati pale inapoona kuna mwelekeo wa kuwa na mabadiliko yanayominya maslahi ya walio wengi.
Nane mpira ni biashara ya kipekee ambayo mafanikio yake yanategemea jinsi washindani wanavyoshirikiana. Hivyo kuelekea mabadiliko haya wanatakiwa watumike wataalamu wa biashara ya mpira ili klabu zinapobadilika ziweke misingi itakayokubaliana na biashara ya soka.
Tisa  klabu zinao wajibu wa kulinda hadhi zake (brand) kwa sababu eneo hilo ndio msingi wa biashara ya mpira. Hivyo klabu zinapoelekea kwenye mabadiliko, lazima zizingatie hadhi zao zinalindwaje.
Kumi Chama cha Waandishi wa Habari na Michezo kiliombwa kufanya makongamao zaidi hasa kuhusiana na aina ya mabadiliko ambayo klabu zinaweza kuingia kwa sababu inaonekana wanachama ambao ndio wamiliki wa klabu hizi hawana uelewa wa kutosha hivyo inawapunguzia wigo wa kuchagua aina ya mabadiliko.
SHIJA RICHARD
KATIBU WA SEKRETARIETI
KONGAMANO LA MABADILIKO YA UENDESHAJI WA KLABU ZA SOKA

Oktoba 24, 2016.
..................................................

TAARIFA KAMILI

UFUNGUZI

Kongamano lilifunguliwa na Katibu Mkuu wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Mohammed Kiganja kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Prof. Elisante  Ole Gabriel.
Kiganja aliwataka wajumbe kujadili hoja badala ya watu au timu. Alisisitiza wajumbe wajadili mifumo na aina ya mabadiliko ambayo klabu hizi zinaweza kuelekea.
Pia aliwataka TASWA kuhakikisha Waandishi wake wanaripoti taarifa zenye weledi na zenye manufaa kwa familia ya wana michezo.
Aliongeza TASWA iunde kamati ya maadili kwa ajili ya kuwawajibisha wanachama ambao wanaenda kinyume cha maadili.
WACHANGIAJI

PROFESA PROSPER NGOWI- Chuo Kikuu cha Mzumbe
Katika mada yake, Profesa anasema wanachama na wadau kwa ujumla hawatakiwi kuogopa kufanya mabadiliko au kubadilisha namna ya kuendesha vitu kwa sababu hilo ni jambo la kawaida.
Hata hivyo akadokeza kuwa wanachama wa Simba na Yanga hawapaswi kuwa wanyonge kuelekea kwenye mabadiliko hayo kwa sababu mtaji wao ni mkubwa kuliko pesa zinazoletwa na wafadhili.
"....(Wanachama) Mtaji wao mkubwa pengine sio pesa. Mtaji wao mkubwa ni majina yaani brand ya timu hizi. Mtaji mwingine ni historia ndefu ya timu hizi ya zaidi ya miaka 80 na ‘fan base’ kubwa sana. Pia vikombe ambazo timu hizi zimeshida ni mtaji mkubwa sana katka meza ya majadiliano. Hii ni mitaji ambayo thamani yake ni kubwa kuliko pesa. Kwa hiyo wenye timu hizi hawapaswi kuwa wanyonge kifedha mbele ya wawekezaji. Thamani ya mitaji hii hasa brand ni kubwa kuliko pesa."
Aliendelea kueleza, "Lazima waelewe kama wanakodisha timu hizi, wanatoa na kupokea masharti gani? Hawapaswi kupokea tuu bali nao watoe masharti. Waamue wanawakilishwa vipi katika uendeshaji wa timu hizi katika nyanja zote? Brand ya timu hizi zinalindwa vipi? Ni muhimu pia kujua kuwa kama mwekezaji atataka muda mrefu wa mkataba, Lazima wenye timu wawe na muda na nafasi ya kufanya marekebisho ktk makubaliano baada ya muda fulani, mfano miaka miwili au mitatu badala ya kusubiri hadi mwisho wa mkataba, mfano miaka 10", anasema Profesa Ngowi ambaye ni mtaalamu wa masuala ya uchumi na biashara.
Profesa Ngowi anasisitiza kuwa kwa mtazamo wa kiuchumi na kibiashara mabadiliko ni jambo la kawaida na halipaswi kuonekana la ajabu.
"Jambo hilo linapaswa kuwa la kawaida kwa yeyote anayependa. Hakuna sababu ya kuogopa kufanya mabadiliko au namna ya kufanya mambo" anasema Profesa Ngowi.
Anaendelea kueleza jambo la msingi katika mabadiliko hayo ni pande zinazohusika hasa wanachama ambao ni wamiliki wa klabu kujua ni kipi wanachokitaka.
"Inavyoonekana wanachotaka ni hali nzuri ya kiuchumi ya timu zao. Sio jambo baya. Wawekezaji nao wanataka maslahi ya kiuchumi nalo sio jambo baya hata kidogo," anasema Profesa Ngowi.
PATRIC MUSUSA - MENEJA WA MASOKO NA MIRADI KUTOKA SOKO LA HISA DSM (DSE)
Mususa anasema  klabu zinapotaka kuelekea kwenye mabadiliko hasa kwa matarajio ya kuingia kwenye soko la hisa, kwanza zihakikishe zinabadilisha mifumo yao iliyopo sasa ili iendane na mahitaji ya soko la hisa.
Anasema lazima zisajiliwe kuwa kampuni na Wakala wa Usajili wa Makampuni (BRELA) na pia ziandae taarifa za fedha.
Lazima zitatakiwa kuwa na Bodi ya Wakurugenzi (BOD) watakaochaguliwa na wanahisa ambao ni wanachama  wamiliki wa klabu hizo.
Kila mwanahisa atastahili kupata gawio la faida pale kampuni (klabu) yao itakapotengeneza faida na atakuwa huru kuuza hisa yake kama anataka  kuachanana na umiliki katika klabu hiyo.

ANGETILE OSIAH, KATIBU MKUU WA ZAMANI WA TFF
Angetile anasema klabu zikihitaji kubadilisha mifumo yao zinatakiwa kuzingatia utawala bora kwa kutofautisha majukumu sekretarieti na taasisi nyingine zilizopo ndani ya klabu.
Anasema ulimwengu wa sasa mchezaji ni rasilimali(asset) inayothaminishwa kwa fedha kwenye vitabu vya hesabu hivyo klabu lazima iwe na wataalamu watakaoweza kukabiliana na changamoto hizo za utaalamu na nyinginezo.
Anasema klabu lazima ziwe na kurugenzi za uendeshaji, habari, biashara, sheria, fedha na masoko na ziajiri wataalamu kwa ajili ya kuendesha shughuli hizi. Kurugenzi hizo zinahitaji wataalamu kama waliopo kwenye taasisi nyingine za serikali na makampuni binafsi.
Anaongeza kuwa uendeshaji wa klabu lazima uzingatie utawala bora kwa kuzipa Uhuru na mipaka ya kazi taasisi au idara zote zilizopo ndani ya klabu.
Anawakumbusha wadau kurejea azimio la Bagamoyo ambapo Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) lilileta utaratibu wa kutoa leseni kwa klabu zilizotimiza mashari.
Anasema masharti yanayotajwa yakiwemo kuwa na utawala bora, timu za vijana n.k kama yatazingatiwa, klabu nitakuwa katika nafasi nzuri ya kuchagua mfumo wa kujiendesha kama ni wa wanachama au wanahisa.
CHARLES NDAKI, Mtaalam wa Masuala ya Masoko
Ndaki anasema jina la timu (brand) ni rasilimali muhimu inayitakiwa kutunzwa na kuendelezwa kwa sababu ndio msingi wa biashara iliyopo katika soka.
Anasema klabu zinatakiwa kuweka mikakati ya kujipa upekee ili kujitofautisha na wengine kwa lengo la kutumia vizuri jina lake kibiashara.
Anasema kwa kufanya hivyo klabu itakuwa na wigo mpana wa wanachama na mashabiki (fun base) NA hivyo kuwa na uwezo mkubwa wa kufanya biashara kupitia jina la klabu.
MICHAEL WAMBURA - KATIBU WA ZAMANI WA TFF

Wambura anasema serikali ndio inayoweza kulinda maslahi ya wengi katika mabadiliko haya hivyo watumie vyombo vyake kuhakikisha yanafanyika mabadiliko yenye maslahi kwa walio wengi.
Anasema ni vyema mabadiliko yakafanyika kwa kuzingatia Sheria za nchi, TFF, CAF na FIFA hivyo aliviomba vyombo vinavyohusika, TFF, BMT na Wizara kuhakikisha zinawezesha mabadiliko haya kwa manufaa ya klabu, wanachama, wawekezaji na sekta ya michezo kwa ujumla.
HENRY TANDAU MKUFUNZI WA FIFA

Anasema wadau katika mabadiliko haya lazima wajifunze mifumo minne ya kuendesha soka kablaya kuelekea mabadiliko.
Anaongeza tatizo kubwa la wadau wa michezo hawapendo kujifunza wanaendesha klabu kwa mazoea.
Anasema biashara ya mpira ni ya aina yake kwa sababu ili ufanikiwe inahitaji ushirikoane na mshindani wako. Kutokana na upekee huo, biashara hii inatakiwa kuendeshwa na wataalamu wenye weledi nayo.
Anasema Azimio la Bagamoyo ndio lilitakiwa kuwa msingi mkubwa wa mabadiliko kwa sababu limeanisha vitu vingi vizuri ambavyo havijafanyiwa kazi.
Anaongeza kuwa japo tumechelewa lakini tulipofika tungeanza na Azimio la Bagamoyo kuelekea kwenye mabadiliko ya kweli.
JAMAL RWAMBOW, MJUMBE WA BARAZA LA MICHEZO LA TAIFA (BMT)
Anasema mabadiliko haya hawawezi kufanyika bila kuishirikisha serikali. "Itakuwa ni kujidanganya kuamini kwamba wawekezaji na wanachama wanaweza kufanya mabadiliko haya bila kuishirikosha serikali kwa sababu serikali ndio baba" anasema Rwambow.
Alitoa mwito kwa wadau kuishirikisha serikali na hasa kufuata maelekezo yaliyotolewa na BMT kuhusiana na utaratibu wa kufanya mabadiliko hayo kama klabu zi nataka kuelekea huko.

Mwishowe Katibu Mkuu wa TASWA, Amir Mhando aliahidi kwamba chama chake kitashirkiana wadau mbali mbali kuhakikisha makongamano kama hayo yanafanyika Mara kwa mara ili kutoa fursa kwa wadau ya kujifunza.


COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4816,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: Je ulisikia mdahalo huu...wa uwezeshajui vilabu kama hapana soma muhtasari huu nawe ujipambanue
Je ulisikia mdahalo huu...wa uwezeshajui vilabu kama hapana soma muhtasari huu nawe ujipambanue
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEid4K3xeD0XhmhLxrqqeajJZPEJnZt-3z-HwUYkK-feZzFmbULsLM07zWOaaOAiAeo9KGTtEShHLxzwn8pI3q4s0UIBa7alHgt5miGcJRlhI7_k76olkVXXe3qAly6kUe5Ji3XPRkRME0w/s1600/yanga+na+simba.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEid4K3xeD0XhmhLxrqqeajJZPEJnZt-3z-HwUYkK-feZzFmbULsLM07zWOaaOAiAeo9KGTtEShHLxzwn8pI3q4s0UIBa7alHgt5miGcJRlhI7_k76olkVXXe3qAly6kUe5Ji3XPRkRME0w/s72-c/yanga+na+simba.jpg
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2016/10/je-ulisikia-mdahalo-huuwa-uwezeshajui.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2016/10/je-ulisikia-mdahalo-huuwa-uwezeshajui.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy