Serikali yalegeza mambo muswada wa habari, maeneo 7 yarekebishwa

SERIKALI imewasilisha bungeni kwa mara ya pili Muswada wa Huduma za Habari wa mwaka 2016 ukiwa na mabadiliko katika maeneo saba ikiwemo k...

SERIKALI imewasilisha bungeni kwa mara ya pili Muswada wa Huduma za Habari wa mwaka 2016 ukiwa na mabadiliko katika maeneo saba ikiwemo kuviondolea vyombo vya habari adhabu kwa baadhi ya makosa ya mwandishi na ukamataji wa mitambo na vifaa vya wanahabari.
Aidha, Serikali imewatoa hofu waandishi kuhusu muswada huo na kusema ikiwa waandishi wa habari watasimamia maadili yao na kutii sheria, hawana haja ya kuhofu kwani Serikali itakuwa mlinzi wao namba moja.
Muswada huo ukiwa na maboresho, uliwasilishwa jana na Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Nape Nnauye.
Wakati Serikali ikieleza hayo, Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni inayohusika na habari, imeupinga Muswada huo na kueleza kuwa unakuja kuua na kuzika kabisa haki na uhuru wa kupata habari kwa wananchi, kuwafunga wahariri na waandishi na umelenga kusambaratisha kabisa tasnia ya habari.
Msemaji wa Kambi hiyo bungeni, Joseph Mbilinyi, katika hotuba yake jana, alishauri Waziri mwenye dhamana ya habari asiachiwe mamlaka ya kuweka viwango vya elimu katika kanuni bali Bodi ya Ithibati na Baraza Huru la Habari likaweka viwango hivyo. Ilipendekeza kiwango kiwe diploma.
Kambi hiyo ilitaka Bodi ya Ithibati isiishie kwa waandishi wa habari bali pia iwe na mamlaka ya ithibati kwa elimu inayotolewa na vyuo mbalimbali vya uandishi wa habari nchini.
Mbilinyi alipendekeza kuwepo kifungu mahsusi cha kuwalinda wanahabari  dhidi ya vitendo viouvu vinavyoweza kufanywa  dhidi yao na kuzungumza kuhusu habari za uchunguzi ambazo alidai umeziua kabisa.

Hata hivyo kambi hiyo ya upinzani iliunga mkono kuanzishwa kwa Bodi ya Ithibati pamoja na Baraza Huru la Habari ili kuwe na viwango na uangalizi pamoja na uratibu wa kitaaluma katika tasnia ya habari pamoja na kuwakatia bima waandishi wa habari.
Aidha, Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii, kuhusu muswada huo, imependekeza pamoja na uvaaji wa vitambulisho kwa waandishi wa habari, kanuni zieleze kuhusu mavazi kama ilivyo kwa wanasheria, madaktari na wauguzi. Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Peter Selukamba, ndiye aliyetoa maoni ya kamati hiyo bungeni jana.
Maboreshi saba:
Nape alisema walifanya maboresho kwa kuzingatia mawazo ya wadau ikiwemo Kamati ya Bunge, taasisi za habari kama Jukwaa la Wahariri (TEF), Baraza la habari (MCT), Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake (Tamwa), Taasisi ya Wanahabari Kusini mwa Afrika, Tanzania (MISA-TAN) na Umoja wa Wamiliki wa Vyombo vya Habari (MOAT)
Waziri Nape pamoja na kueleza kuwa muswada huo uliopigwa danadana kwa zaidi ya miaka 23 utaleta mapinduzi na kuweka historia katika tasnia ya habari nchini, alieleza maboresho kadhaa.
Maboresho hayo ni katika eneo la kuanisha haki na wajibu wa wanahabari; kuainisha haki ya chombo cha habari kukata rufaa; uwakilishi wa wanahabari katika Bodi ya Ithibati; Jaji Mkuu kuweka utaratibu kusikiliza haraka kesi za kashfa.
Maeneo mengine ni kuviondolea vombo vya habari adhabu kwa baadhi ya makosa ya mwandishi; vyombo vya dola kukamata mitambo na vifaa vya wanahabari na mitambo kutohusika moja kwa moja kwa kosa la gazeti.
Akifafanua kuhusu maboresho hayo, Nape alisema kuhusu haki ya wanahabari lazima kuzingatia mikataba ya kimataifa ambayo nchi imesaini na kuridhia pamoja na matakwa ya Kikatiba.
"Muswada sasa umeweka mfumo wa wazi zaidi na wa kidemokrasia ambapo uamuzi wa Mkurugenzi wa Idara ya habari-Maelezo hautakuwa wa mwisho. Chombo husika kinaweza kukata rufaa kwa Waziri wa Habari na kisiporidhika na uamuzi kinaweza kupinga suala hilo mahakamani," alisema Nape.
Nape alisema katika uwakilishi wa Bodi ya Ithibati, kati ya wajumbe saba, wakiwemo wanne waandishi, sasa kutakuwa na uwiano katika sekta binafsi ya ya umma. Awali hakukuwa na uwiano huo.
Kuhusu kusikiliza kesi za kashfa kwa haraka, Nape alisema Jaji Mkuu kwa kuzingatia tathimini ya uwezo wa mahakama na rasilimali, na kama ilivyo kwa kesi nyingine za uchaguzi na za biashara, atatunga kanuni zitakazoweka muda wa kumalizika kwa kesi. Awali muswada haukueleza hilo.
"Moja ya mageuzi makubwa ya muswada ni kuviondolea vyombo vya habari au umiliki wake adhabu ya makosa yanayomuhusu mwandishi binafsi. Sasa mwandishi kama mwanataaluma kamili anaweza kuwajibishwa na Bodi ya Ithibati kwa makosa ya kimaadili badala ya mtindo wa sasa wa kila kosa la mwandishi kubebwa na chombo chake," alisema Nape.
Kuhusu kukamata mitambo, Nape alisema maoni ya wadau yamezingatiwa na sasa mamboresho yamemuondoa Mkurugenzi wa Idara ya Habari kuwa na mamlaka ya kukamata mitambo badala yake kazi hiyo itafanywa na Polisi kwa mujibu wa Sheria ya Makosa ya Jinai (CPA).
Aidha, Nape alisema kuhusu mitambo ya uchapishaji kuwa sehemu ya makosa chombo cha habari kinapoandika uchochezi au makosa mengine ya kashfa, wachapaji wameondolewa katika makosa yanayotokana na maudhui ya watu wengine.
Muswada huu unajadiliwa kwa siku mbili, jana na leo bungeni, utapitiwa kifungu kimoja baada ya kingine, kabla ya kupitishwa.
Source: HabariLeo

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4816,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: Serikali yalegeza mambo muswada wa habari, maeneo 7 yarekebishwa
Serikali yalegeza mambo muswada wa habari, maeneo 7 yarekebishwa
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhXsKWbhEAveDHCEdnmHKbFhOknxnyntS-2uJLOlEIv07a6PMZtO0SbotYEalv0_ewnoaWmuOh8l0VfC_MC4sL_00KNFysYMM3tmqBD4AbKBVpaxajfWoHup27LgHSMMDzBk4Jh9AbWRoQ/s1600/nape.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhXsKWbhEAveDHCEdnmHKbFhOknxnyntS-2uJLOlEIv07a6PMZtO0SbotYEalv0_ewnoaWmuOh8l0VfC_MC4sL_00KNFysYMM3tmqBD4AbKBVpaxajfWoHup27LgHSMMDzBk4Jh9AbWRoQ/s72-c/nape.jpg
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2016/11/serikali-yalegeza-mambo-muswada-wa.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2016/11/serikali-yalegeza-mambo-muswada-wa.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy