For record Purposes:Shirika la Ndege la Uturuki lazindua safari za Zanzibar

Shirika la Ndege la Uturuki limezindua safari zake za moja kwa moja kutoka Instabul- Uturuki hadi Zanzibar. Safari hiyo ambayo ni kutoka...

Shirika la Ndege la Uturuki limezindua safari zake za moja kwa moja kutoka Instabul- Uturuki hadi Zanzibar. Safari hiyo ambayo ni kutoka Istanbul – Kilimanjaro – Zanzibar – Istanbul (IST-JRO-ZNZ-IST ) itakuwa ni mara tatu kwa wiki. Kuzinduliwa kwa safari hiyo kunafanya shirika hilo kuwa na maeneo 50 inayoyahudumia katika bara la Afrika. Kutokana na kuanzisha kwa huduma hiyo, shirika hilo ambalo linaheshimika duniani kutokana na kuwa na maeneo mengi inayotoa huduma za usafiri wa anga, litakuwa sasa lina maeneo 293 duniani ambayo inahudumia. Maeneo ya Afrika ambayo shirika hilo linatoa huduma zake ni pamoja na miji ya Afrika Mashariki ya Dar es Salaam, Kilimanjaro, na Zanzibar; Nairobi, Mogadishu, Djibouti, Asmara, Addis Ababa, Kigali na Entebbe. img_3898

Ndege ya shirika la ndege la Uturuki (Turkish Airlines), Boeing 737-900 ikiwa na abiria 150 ikipokea saluti ya maji wakati ilipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume kuanza safari tatu katika wiki za moja kwa moja kati ya Instabul na Zanzibar.

Ikiwa ni mruko TK567, ndege ya shirika hilo litawezesha wateja wake kuwa na safari ya moja kwa moja hadi uwanja wa ndege wa kimataifa wa Istanbul wa Atatürk ambako kutoka hapo wataweza kuunganishwa na mji mingine muhimu ya Ulaya kama Frankfurt, Muscat, Munchen, Dubai, Paris, London, Milano, Amsterdam, Zurich, Bombay, Copenhagen, Stockholm, Rome, Brussels, Berlin, Vienna, Hamburg, Tel-Aviv, Düsseldorf, na Prague. "Shirika la ndege la Uturuki liko katika biashara ya kuhamisha elimu, mawazo, ndoto na fursa katika maeneo mbalimbali duniani. Tuko hapa leo kujenga daraja jingine kati ya dunia na Zanzibar, daraja ambalo pia litaimarisha uhusiano uliopo kati ya wananchi wa Uturuki na wa hapa Zanzibar", alisema Bw. Ahmet Olmustur, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Masoko wa Shirika la Ndege la Uturuki. Akifafanua zaidi kauli hiyo alisema: "Ni jambo la furaha kuona kwamba uzinduzi wa safari ya kuja Zanzibar na kwenda Instabul umefanyika kabla ya msimu wa sikukuu. Kutokana na hali hiyo, uzinduzi huu sio tu wa kuanzisha safari za ndege , bali ni sehemu ya maadhimisho ya hatua kubwa iliyopiga Zanzibar, Tanzania na Afrika kwa ujumla katika usafiri wa anga. Kupitia uwanja wa ndege wa Instabul, tutawaunganisha wasafiri kutoka Zanzibar kwenda katika vituo zaidi ya 161 duniani, kazi tunayoifanya kwa ufanisi kuliko shirika jingine lolote lile la ndege". eh4a8337 Kwa mujibu wa taarifa za Shirika hilo Tanzania inakuwa nchi ya 50 barani Afrika kufikiwa na Shirika la Ndege la Uturuki baada ya kuongezwa safari hizo tatu kwa wiki kwenda Zanzibar Hivi sasa shirika hilo lilikuwa linafanya safari 49 barani Afrika baada ya hivi karibuni pia kuongeza safari ya kwenda Visiwa vya Shelisheli. Likiwa ni shirika la nne kwa kuwa na mtandao mkubwa wa safari duniani kote kuliko mashirika mengine, ndege ya Shirika iliondoka Istanbul saa 6:30 usiku na kuwasili saa 3:30 asubuhi. Akizungumza katika tukio hilo la kihistoria, Waziri wa Miundombinu, Mawasiliano na Uchukuzi, Balozi Ali Abeid Amani Karume alisema Zanzibar imefurahishwa sana kufanyakazi na moja ya mashirika ya ndege yenye mafanikio makubwa duniani ambayo yamekuwa yakitengeneza faida. eh4a8355

Ofisa Masoko Mkuu wa Shirika la ndege la Uturuki, Bw. Ahmet Olmustur (kulia) na Mjumbe wa bodi ya Shirika la ndege la Uturuki Ogun Sanlier wakishuka kwenye ndege mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume mjini Zanzibar.

“Sisi Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, tunakaribisha sana ushirikiano huu kwa sababu nyingi, kwa kuwa si tu inafungua lango la watalii lakini pia tunatengeneza fursa mpya kwa wananchi wetu”, alisema Balozi Karume. Pia aliamini kwamba kuja kwa ndege za Shirika hilo kutawezesha watu wengi zaidi kuja Zanzibar kwa utalii na pia kutoa fursa kwa watu mbalimbali wanaoanzia safari zao Zanzibar kuunganisha safari zao kwenda nchi mbalimbali Ulaya kwa urahisi zaidi. Aliwahimiza wananchi wa Zanzibar kutumia fursa hiyo kutengeneza nafasi ya nyingi zaidi za kibiashara na kuongeza idadi ya watalii nchini humo. Ndege ya shirika hilo la Uturuki aina ya Boeing 737-900 ikiwa na abiria 150 iliwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume majira ya saa 3.30 asubuhi na kupokea saluti ya maji kabla abiria hawajaruhusiwa kushuka. Baadae ndege hiyo TK567 iliondoka Zanzibar saa 4:25 asubuhi na ilitarajiwa kuwasili Istanbul saa 11:45 jioni.

img_3958

Ofisa Masoko Mkuu wa Shirika la ndege la Uturuki, Bw. Ahmet Olmustur na Mjumbe wa bodi ya Shirika la ndege la Uturuki Ogun Sanlier pamoja na wageni walioshuka na ndege ya Uturuki wakiangalia burudani ya ngoma za asili mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume mjini Zanzibar.

eh4a8395

Katibu Mkuu wa Wizara ya Miundombinu, Mawasiliano na Uchukuzi Zanzibar, Mustafa Aboud Jumbe (katikati) pamoja na uongozi wa Shirika la ndege la Uturuki wakikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa safari hiyo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume mjini Zanzibar.

eh4a8411

Ofisa Masoko Mkuu wa Shirika la ndege la Uturuki, Bw. Ahmet Olmustur na Mjumbe wa bodi ya Shirika la ndege la Uturuki, Ogun Sanlier wakimshukuru Katibu Mkuu wa Wizara ya Miundombinu, Mawasiliano na Uchukuzi Zanzibar, Mustafa Aboud Jumbe (wa nne kushoto) baada ya kuzindua rasmi safari hiyo.

eh4a8444

Mgeni rasmi Waziri wa Miundombinu, Mawasiliano na Uchukuzi Zanzibar, Balozi Abeid Amani Karume (wa sita kulia) katika picha ya pamoja na Balozi wa Uturuki nchini Yasemin Eralp (wa tisa kulia) pamoja na uongozi wa Shirika la Ndege la Uturuki katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume mjini Zanzibar.

eh4a8420

Ofisa Masoko Mkuu wa Shirika la ndege la Uturuki, Bw. Ahmet Olmustur (kushoto) na msafara wake wakielekea kwenye chumba maalum cha mapumziko baada ya kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume mjini Zanzibar.

img_4016

Sehemu ya abiria waliotua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume mjini Zanzibar na Shirika la Ndege la Uturuki ikiwa ni safari ya kwanza visiwani humo.

img_4029

eh4a8509

Waziri wa Miundombinu, Mawasiliano na Uchukuzi Zanzibar, Balozi Abeid Amani Karume akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika Hotel ya Park Hyatt visiwani Zanzibar. Kushoto ni Ofisa Masoko Mkuu wa Shirika la ndege la Uturuki, Bw. Ahmet Olmustur.

dsc_1069

Ofisa Masoko Mkuu wa Shirika la ndege la Uturuki, Bw. Ahmet Olmustur akiongea katika mkutano na waandishi wa habari kuhusu safari mpya kutoka Zanzibar -Kilimanjaro-Istanbul (ZNZ-JRO-IST-ZNZ ) ambayo itakuwa ni mara tatu kwa wiki.

dsc_1119

Sehemu ya waandishi wa habari wakichukua matukio muhimu yaliyojiri kwenye mkutano huo.

dsc_1058

Balozi wa Uturuki nchini Yasemin Eralp (wa pili kushoto) akichukua matukio ya picha katika mkutano na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa safari mpya ya Shirika la Ndege la Uturuki mjini Zanzibar.

eh4a8528

Ofisa Masoko Mkuu wa Shirika la ndege la Uturuki, Bw. Ahmet Olmustur (wa pili kushoto) akikabidhi mfano wa sanamu ya ndege ya Shirika la Ndege la Uturuki Boeing 737-900 iliyopewa jina la Zanzibar kwa Waziri wa Miundombinu, Mawasiliano na Uchukuzi Zanzibar, Mh. Balozi Abeid Amani Karume kuashiria mwanzo wa mahusiano ya mawasiliano ya anga kati ya Uturuki na Zanzibar. Shirika hilo jana lilizindua safari za moja kwa moja kati ya Zanzibar na Instabul, Uturuki. Wengine wanaoshuhudia ni Mjumbe wa bodi ya Shirika la ndege la Uturuki Ogun Sanlier (wa pili kulia) na wafanyakazi katika ndege iliyotua jana mjini Zanzibar.

eh4a8527

Ofisa Masoko Mkuu wa Shirika la ndege la Uturuki, Bw. Ahmet Olmustur akimuonyesha jina la Zanzibar kwenye mfano wa sanamu ya ndege ya Shirika la Ndege la Uturuki Boeing 737-900 Waziri wa Miundombinu, Mawasiliano na Uchukuzi Zanzibar, Mh. Balozi Abeid Amani Karume (kulia) wakati wa mkutano na waandishi wa habari (hawapo pichani) uliofanyika katika Hoteli ya Park Hyatt visiwani Zanzibar. Wa pili kushoto ni Mjumbe wa bodi ya Shirika la ndege la Uturuki, Ogun Sanlier.

eh4a8535

Mgeni rasmi Waziri wa Miundombinu, Mawasiliano na Uchukuzi Zanzibar, Mh. Balozi Abeid Amani Karume akiwa ameshikilia sanamu la ndege ya Shirika la Ndege la Uturuki katika picha ya pamoja na Balozi wa Uturuki nchini Yasemin Eralp (katikati), Ofisa Masoko Mkuu wa Shirika la ndege la Uturuki, Bw. Ahmet Olmustur (wa pili kushoto), Mjumbe wa bodi ya Shirika la ndege la Uturuki, Ogun Sanlier (wa pili kulia) pamoja na wafanyakazi katika ndege iliyotua jana mjini Zanzibar.

eh4a8543

Sanamu la ndege ya Shirika la Ndege la Uturuki Boeing 737-900 iliyopewa jina la Zanzibar iliyotua jana mjini Zanzibar.

eh4a8549

Mgeni rasmi Waziri wa Miundombinu, Mawasiliano na Uchukuzi Zanzibar, Mh. Balozi Abeid Amani Karume na Mjumbe wa bodi ya Shirika la ndege la Uturuki, Ogun Sanlier wakiweka vituo Istanbul-Zanzibar kwenye ramani wakati wa mkutano na waandishi wa habari (hawapo pichani) mjini Zanzibar.

eh4a8551

Mgeni rasmi Waziri wa Miundombinu, Mawasiliano na Uchukuzi Zanzibar, Mh. Balozi Abeid Amani Karume na Mjumbe wa bodi ya Shirika la ndege la Uturuki, Ogun Sanlier wakionyesha vituo vya safari ya Istanbul - Zanzibar kwenye ramani mbele ya waandishi wa habari.

eh4a8555

Picha ya pamoja baada ya mkutano na waandishi wa habari.

eh4a8557

Taarifa zaidi kuhusu ratiba ya safari:
Namba ya ndege Kuanzia Siku Kuondoka Kuwasili
TK 567 14 Desemba 2016 Jumatatu Jumatano Jumamosi Istanbul 20:30   3:20 (+1) Kilimanjaro
TK567 15 Desemba 2016 Jumanne Alhamis Jumapili Kilimanjaro 04:15 5:30 Zanzibar
TK 567 15 Desemba 2016 Jumanne, Alhamis Jumapili Zanzibar 06:25 13:45 Istanbul
    Muda uliotajwa ni wa LMT.

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4816,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: For record Purposes:Shirika la Ndege la Uturuki lazindua safari za Zanzibar
For record Purposes:Shirika la Ndege la Uturuki lazindua safari za Zanzibar
http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2016/12/IMG_3898.jpg
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2016/12/for-record-purposesshirika-la-ndege-la.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2016/12/for-record-purposesshirika-la-ndege-la.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy