NAPE AMSHUKURU MAGUFULI KWA KUMUAMINI KWA MWAKA MMOJA

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye amemshukuru Rais Dk Johna Magufuli kwa kipindi cha mwaka mmoja alichomuami...



Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye amemshukuru Rais Dk Johna Magufuli kwa kipindi cha mwaka mmoja alichomuamini kutumikia wizara hiyo kama kijana.
Nape alisema hayo LEO jijini Dar es Salaam mbele ya Kanisa la Mtakatifu Peter ambako alikwenda kukutana na waandishi wa habari kwenye hoteli ya Protea hata hivyo mkutano huo kuzuiwa na jeshi la polisi hivyo kulazimika kuzungumza akiwa juu ya gari.
 “Lengo la kwangu la kuja hapa la kwanza ilikuwa ni kumpongeza Rais kwa uamuzi alioufanya na pia kumshukuru kwa kuniamini kwa mwaka mmoja, na wale mliotumwa sikilizeni mkawaambie,” alisema Nape.
Alisema anamshukuru Rais alimuamini kama kijana na kumpa heshima ya kuingia kwenye baraza la mawaziri na kwamba kama ambavyo Rais alimuamini atumikie kwenye nafasi hiyo lakini sasa ameona na amemuweka Aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria Dk Harrison Mwakyembe.
Nape alisema anapongeza pia Dk Mwakyembe na pia anamuunga mkono  kwa uteuzi huo na kwamba kwasababu ni mwanahabari anaimani atasimamia vizuri tasnia hiyo.
Nape alisema hana kinyongo na Rais Magufuli katika uamuzi wake alioutangaza asubuhi jana wa kumteua Dk Mwakyembe kuwa Waziri wa wizara hiyo ambayo alikuwa akiiongoza yeye kushika nafasi yake.
“Kama ambavyo sikumshawishi Rais kunichagua ndivyo ambavyo sina say (kauli) na uamuzi aliofanya, lakini wakati anaunda baraza walikuwepo watu wengi sana, alipoamua kunichukua mimi kuna watu walikuwepo na walikubali, mimi leo nakatalia nini, sina sababu ya kukataa,” alisema Nape.
Baada ya Gari ya Nape kufika eneo la kanisa hilo wakati akishuka, alitokea mtu ambaye alianza kumsukuma Nape akimrudisha kwenye gari asishuke kwenda kuzungumza na waandishi wa habari ambao walikuwa wamejaa katika eneo hilo na baadaye kuja askari waliokuwa na sare.
Kitendo hicho cha Nape kusukumwa arudi kwenye gari na mtu yule aliyekuwa na nguo za kiraia ambaye Nape alisema hamfahamu na hajui ametumwa na nani Nape aliendelea kusisitiza kuwa hakuna haja ya kutumia nguvu na silaha akimtaka amuache aendelee kuzungumza na wanahabari.
Kutokutii huko kwa Nape kulimfanya mtu huyo ambaye alikuwa akimsukuma kulazimika kutoa silaha (bastola) akisisitiza Nape arudi kwenye gari.
Baada ya mvutano wa muda mrefu, Nape aliamua kusimama kwenye mlango wa gari na kuanza kuzungumza na wanahabari akiwa hapo na baadaye kuingia kwenye gari kufungua dirisha la juu ya gari akatoa kichwa na kuanza kuzungumza akiwa hapo huku wale watu waliokuwa wakimzuia wakiendelea kuwepo pale. 
Katika mazungumzo yake na wanahabari, Nape alisema amejitahidi kutimiza wajibu wake katika nafasi yake ya uwaziri.
“Jana wakati nilipoongea na vyombo vya habari wakati napokea ile ripoti, nilisema kuna gharama ya kulipa wakati wa kusimamia haki za watu na mimi niko tayari kulipa, sioni sababu kwanini vyombo vinapaniki,” alisema Nape na kuongeza kuwa  uzalendo wake kwa nchi hauwezi kutiliwa mashaka
“Nimekuwa mzalendo kwa nchi yangu, nimekuwa muungwana kwa nchi yangu na ninaapa kuendelea kuwa muungwana kwa nchi yangu hilo hakuna atakayelibadilisha,” alisema.
Alisema amekuwa pia mzalendo kwa CCM chama ambacho kiko kwenye shimo alisimama kukiinua uzalendo ambao haufai kutiliwa mashaka na kwamba alijifunza usemi wa ‘nitasema kweli daima fitina kwangu mwiko’ na alichokisimamia ni kusema kweli.
Alisema aliwataka watu hao waliokuwa wakimzuia pamoja na watu waliowatuma wasihangaike naye kwani ni mtu mdogo kuliko Tanzania badala yake wahangaike na mambo mengine yenye manufaa kwa nchi.
“Nimekuja hapa mtu anakuja na bastola ananiamrisha nirudi kwenye gari, nani amekupa mamlaka hayo, unalipwa kwa kodi ya kwetu, mnajua ni namna gani tumepambana kwaajili ya nchi hii, miezi 28 nalala porini angalieni mkono wangu huu,” alisema Nape.
Nape alisema hayo akionesha mkono ambao aliumia baada ya kupata ajali ya gari … ambapo alisema pia kuwa alipigana kuhakikisha Chama cha Mapinduzi (CCM) kinabaki madarakani.
Nape alisema vyombo vya ulinzi na usalama viangalie jambo hilo lililofanyika la kumzuia kushuka kwenye gari kwa kutumia nguvu na kummtolea bastola wakati hakuwa na nia mbaya.
“Nia yangu haikua mbaya kwa serikali yangu, nia yangu ilikuwa ni kuwaeleza watanzania kwamba maisha lazima yaendee, sasa wanapokuja watu wachache (wapuuzi) wanadhani wanaweza kukoroga hivi mambo,” alisema.
Alisema alipoteuliwa Rais John Magufuli hakumuuliza hivyo wakati anataka kumuweka mtu mwingine hana sababu ya kuulizwa na pia hana kinyongo na Rais.
“Sijasema chochote kwamba nina kinyongo na Rais wangu, kwani kuna watu wanataka wao ndio wawe waamuzi wa mawazo ya vijana wa nchi hii,” alisema Nape.
Aidha alisema kinachowakutanisha watu sio sare za CCM za rangi ya kijani bali imani ya kuwa wakweli kuachana na fitina.
Alisema uzalendo amefundishwa na baba yake marehemu Moses Nnauye ambaye alikuwa mwanasiasa mkongwe wa CCM kusema kweli na kusimamia anachokiamini na kama kitaleta matatizo hana shida kwani alishawahi kufukuzwa kwenye chama chake hicho.
Nape ambaye alishawahi kufukuzwa CCM alisema katika maisha ya siasa kupita kwenye migogoro ni jambo la kawaida kwani lazima mbegu ioze ndipo iote, “sasa mbegu niliyoipanda itaota, mbegu ya kusimamia haki hakika itaota.”
Aliwaasa vijana kusimamia ukweli, kutokuwa waoga na kusimamia kile wanachokiamini.
Nape alisema katika kipindi ambacho amekuwa katika wizara hiyo anaamini ametumia akili na uwezo wake wote kuwatumikia watu walioko chini na wizara hiyo na kwamba alipata ushirikiano wa kutosha.
“And I real love you people, napenda kufanya kazi na nyie na nimefurahi sana, sana kufanya kazi na nyie, na nina waombeni mumuunge mkono waziri mpya aliyepewadhamana na fanyeni nae kazi na pia endeleeni kumuunga mkono Rais Magufuli ndie rais tuliyepewa na Mungu na tuliyempigia debe watanzania,” alisema.
Aliwataka pia watanzania kuendelea kudumisha umoja na mshikamano wan chi na kwamba sio wakati wa kuvuruga nchi kwani kuna mambo mazuri mbele. lisema alipenda kuendelea kufanya kazi hiyo lakini wakati umefika amelazimika kuondoka
Nape alisema anarudi kufanya kazi katika jimbo lake kwa kuwatumikia katika yale waliyomtuma kama mbunge wao.



COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4816,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: NAPE AMSHUKURU MAGUFULI KWA KUMUAMINI KWA MWAKA MMOJA
NAPE AMSHUKURU MAGUFULI KWA KUMUAMINI KWA MWAKA MMOJA
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2017/03/nape-amshukuru-magufuli-kwa-kumuamini.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2017/03/nape-amshukuru-magufuli-kwa-kumuamini.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy