Demokrasia yetu isivyofanana na ya wenzetu

Na abdul mtemvu Ulimwengu wa siasa ulimalizika mwaka 2016 kwa kituko kikubwa cha aliekuwa rais wa Gambia, Yahya Jammeh, kwanza kuku...


Na abdul mtemvu

Ulimwengu wa siasa ulimalizika mwaka 2016 kwa kituko kikubwa cha aliekuwa rais wa Gambia, Yahya Jammeh, kwanza kukubali uchaguzi halali wa kidemokrasia kufanyika nchini kwake (hakulazimishwa na mtu yeyote).  Ukafanyika na akashindwa kihalali na, baadae mwenyewe,  kumpongeza aliemshinda (Adama Barrow), na dunia ikampongeza kwa kuwa muungwana wa kukubali matokeo. Dunia ilimpongeza kwa, pengine, kufikiria Afrika imejiingiza kwenye Ulimwengu wa demokrasia ya Kimagharibi. Kumbe sio! Yaliyotokea na kumkuta Yahya Jammeh ni historia, tofauti na heshima ambayo, pengine, angeipata kwa kukubali kwake kushindwa na kupata heshima iliyotukuka.
Mfano wake ni sawa na ule wa nchi ya Burkina Farso, ambayo iliinggia kwenye heka heka na misuko suko ya kijinga tu kwa Blaise Campaore kutaka kung’ang’ania madaraka! Sawa na yalioikumba Ivory Coast. Kisa, eti, ni wapambe  na ndugu hata marafiki walio karibu na kiongozi mhusika ambao hawako tayari kurudi kijiweni ilhali kuna lukuki ya wananchi wako kijiweni! Hawa ndio chimbuko la vurugu na machafuko yote! Wapambe nuksi. Nani asiejua Bagbo kaponzwa na nani? Alishindwa uchaguzi halali wa kidemokrasia nchini kwake na, baada ya kushindwa,  akashawishiwa na mkewe kuitumbikiza nchi yake kwenye machafuko makubwa ambayo hayana mithili. Leo, yuko wapi?  Hadithi kwa Afrika inaendelea na hakuna anaejifunza hadi kiyama kitukute.
Blaise Campaore (aliyempindua mwanamapinduzi wa mfano barani afrika na swahiba wake wa damu –Tomas Sankara),baada ya kunogewa na madaraka baada ya miaka takriban ishirini na saba madarakani  akakataa kuachia ngazi, huku akitaka kushawishi bunge kubadili katiba ili aendelee na uongozi wake usio na tija kwa nchi yake. Ya, Yahya  Jammeh ndio yalikuwa ya Blaise Campaore na ndio yaliyokuwa ya Bagbo! Hakuna aliejifunza kwa mwenzake?
Hawa ndio viongozi wetu wa bara letu ambao, kwa kiwango kikubwa, wengi wao wamechukua nafasi ile ile ya waliokuwa wakoloni wetu kupora rasilimali za nchi na, bila aibu, kuzipeleka  kule kule Ulaya! Neno demokrasia kwao ni msamiati tu usio maana wala tafsiri inayoeleweka. Demokrasia kwao ina tafsiri ya wao kuwepo madarakani, ama iwe kwa hila au ghilba. Alimradi na ikibidi wang’oke basi itakuwa ni kwa mbinde. Tena mbinde kweli kweli (wakati mwingine mpaka wazungu wawalazimishe). Kwao haijalishi madhara ama madhira gani wanasababisha kwa wananchi na nchi zao.
Aliekuwa rais wa awamu ya nne, Dk Jakaya Mrisho Kikwete, aliwashangaza mabalozi na wawakilishi wa Afrika, nchini China, wakati wa ziara yake nchini humo, alipozungumza kuhusu kuchoshwa na Urais na kutamani walau muda wake ungekuwa umeisha ili arudi nyumbani kuwa mtu wa kawaida! Rais Kikwete alizungumza hayo wakati hata muda wake wa mihula miwili ya miaka mitano mitano haijaisha rasmi. Wakati wa kuadhimisha miaka 53 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, Tanzania na Dunia ilishuhudia viongozi wastaafu wa Tanzania (Mzee Mwiyi, Mkapa, Kikwete na Karume) wakiwepo kwenye membari wakicheka na kufurahi. Nchi gani Afrika ambayo  ina viongozi wastaafu wanaoweza kuwepo pamoja kwenye hafla ya kitaifa wakawa hawana bifu miongoni mwao? Wanacheka tu!
Blaise Campaore, kama mwenzake Yahya Jammeh,  alikaribia kumaliza miaka ishirini na saba ya utawala ambao wangalau ulikuwa na chembe chembe za kidemokrasia pamoja na kuwa alikuwa akiipinda pinda, baada ya awali kuingoza nchi yake kijeshi, lakini ni wazi kwa tamaa yake hiyo, miaka yote hiyo hayakumtosha. Angetaka, si angefanya katiba ya kuwa kiongozi wa maisha! Nani angeweza kumzuia, lakini hakuelewa. Hakuelewa kuwa katiba ndio imemponza. Katiba haichezewei chezewi kama kutafuna tambuu.
Hata hivyo, hii sio hoja ya msingi. Hoja ya msingi ni kwamba, kaifanyia nini nchi yake na watu wake miaka yote hiyo? Alimpindua Tomas Sankara (kama mwenzake Yahya Jammeh alivompindua kiongozi halali), lakini ilikuwa  yeye afanye nini? Ni wazi kuwa kilichompelekea kumpindua, na hatimae kumuua, rafiki yake na mwanamapinduzi mwenzake ni wivu na uchu wa madaraka. Hakusukumwa na mwamko kuwa mapinduzi yale, chini ya kapteni Sankara, yalikuwa yamekosa mwelekeo na kuwa Sankara alishapoteza dira na, kwa hali hiyo, akajiona yeye ndio alifaa kurekebisha mambo.
Hata pale alipomuua mwenzake dunia ilimsamehe. Viongozi wenzake wa Afrika (wakati ule hata Mwalimu Nyerere alimsamehe), waliangalia pembeni wakidhani, pengine, ni ajali ya kisiasa ambayo hutokea nyakati za vugu vugu za mapinduzi. Kumbe hakuwa na Uanamapinduzi wowote! Uchu na tamaa za madaraka ndizo zilizotawala udhalimu wake.
Ni kwa nini viongozi wetu (wa Afrika) hawaheshimu katiba? Ni kwa nini wanafikiri wananchi wao ni kundi sawa na la kondoo la kuburuzwa buruzwa tu, kundi la kudanganywa danganywa kila mara na wao ndio waamuzi wa mwisho wa mustakabali wa taifa na watu wao? Kama Blaise Campaore na  Yahya Jammeh  wameshindwa kuipa msukumo wa maendeleo nchi zao badala ya kujitajirisha wao, jamaa na familia zao tu, kwa miaka yote waliokaa madarakani, wangeweza kufanya nini kwenye miaka mingine wanayotaka kujiongezea - hata kama wangekaa daima madarakani.
Nchini Burkina Faso, na baadhi ya nchi zinazofanana nayo, wakati wa Campaore,  wananchi wa Ufaransa na wageni wengine waliishi maisha ya peponi kuliko hata Waburkinabe wenyewe ambao wengi wao wakilindwa na vikosi vya jeshi maalum la Ufaransa huku vijana (wasomi wa Kiburkinabe) wakiwa hawana matumaini yoyote ya hatma za maisha yao ya siku hadi siku. Maisha yasio matarajio ya ahueni kwa leo wala kesho! Huu na hii ndio dhana ya uhuru wa baadhi ya nchi zetu barani Afrika! Maisha na hali ambapo viongozi wamekua sawa na mwewe wanaovizia na kutafuna vifaranga vya kuku. Wanachuma utajiri unaoishia nchi za Ulaya. Kwao, wananchi wao ndio vifaranga na wao ndio mwewe!
Tony Blair, wakati akiwa madarakani, aliwahi kukaririwa akisema, kwamba: ‘Africa is not poor but is poorly governed’ dhana ambayo haina ubishi kwa kuwaangalia aina ya viongozi wengi barani kwetu. Kwa hakika, tumefika mahali, wazungu tunaowaenzi sana wamewafanya viongozi wetu wengi kuwa kama wanasesere wao! Nchi yoyote Afrika ambayo balozi wa Ulaya akiletwa na akikaa miaka miwili ndio anaishia kuwa mtaalam wa mambo ya Afrika nchini kwao.  Ni aibu! Bongo tuna watu wamekaa miaka hata ishirini vijijini wakiwa viongozi, lakini hatuna hata mtaalam mmoja ambae kaandika kitabu cha changamoto ya Wilaya ua Kijiji alichokiongoza! Mzungu anakuja nmiaka miwili tu, lakini mwaka mmoja tu anatoa darasa kwao! Anajiita mtaalam na hata kutufundisha sisi wenyewe wenye nchi yetu.
Hakika, tufike mahali viongozi wetu wabadilike. Kama mifumo ya kigeni imetushinda, basi, turudi ama tubuni mifumo itakayoendana na tamaduni na historia zetu. kwani kuna ulazima gani, mathalan, kuwa na vipindi vitano vitano vya mihula miwili vya Urais? Kwa nini tusifanye miaka kumi kumi ya vipindi viwili ili kiongozi atosheke ama hata kipindi cha muhula mmoja wa miaka kumi na ushee ya rais kutawala angalau atosheke yeye na wapambe wake? Mbona Papa, Kadinali au Mufti hawana muhula wa uongozi? Akitawazwa ni mpaka umauti umfike ndio aje mwingine.
Ili balaa la viongozi wetu kutaka katiba iseme mihula ya utawala katuletea nani wakati hatuiheshimu? Iweje, viongozi wetu wanaoridhia balaa hili la kutaka mihula ndio hao hao wawe chanzo cha machafuzi ya nchi zetu? hakika, ipo haja ya kutafakari ili.
Wasalaam.


COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4816,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: Demokrasia yetu isivyofanana na ya wenzetu
Demokrasia yetu isivyofanana na ya wenzetu
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEij23DFuPQpTxO1LJzJaQfvDcAfprf3_nkTBZA7Liee-sUGJeAUz3s4qp2sAWr2HB36NNo0gjpYVszQnBlAB54R-YIUbWYK_AlFRM34igLAduJ-gH9jhHZaVirk0Z1yt3siscebszYrLio/s1600/democracy.png
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEij23DFuPQpTxO1LJzJaQfvDcAfprf3_nkTBZA7Liee-sUGJeAUz3s4qp2sAWr2HB36NNo0gjpYVszQnBlAB54R-YIUbWYK_AlFRM34igLAduJ-gH9jhHZaVirk0Z1yt3siscebszYrLio/s72-c/democracy.png
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2017/04/demokrasia-yetu-isivyofanana-na-ya.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2017/04/demokrasia-yetu-isivyofanana-na-ya.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy