BODABODA WABANANA NA POLISI, MABOMU MTINDO MZIMA

>>>Katavi wachimbaji, walinzi wapambana JESHI la Polisi mkoani Shinyanga limelazimika kupiga mabomu ya machozi na maji ya k...


>>>Katavi wachimbaji, walinzi wapambana

JESHI la Polisi mkoani Shinyanga limelazimika kupiga mabomu ya machozi na maji ya kuwasha kwa kundi la waendesha bodaboda zaidi ya 80.
Watu hao walikuwa wakiandamana katika eneo la Ibinzamata baada ya mwenzao, Joel Mamla (26) kupoteza maisha juzi wakati alipokuwa anapelekwa  Kituo cha Polisi mjini Shinyanga baada ya kuvunja sheria za barabarani.
Jeshi hilo lililazimika kutumia kikosi cha Askari wa Kutuliza Ghasia (FFU) kutuliza vurugu hizo, ambapo walitumia ‘section’ tano za askari, ambapo kila ‘section’ yenye askari tisa ilitumika kuwatuliza waendesha bodaboda hao baada ya kuwataka watawanyike kwa amani.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Jumanne Murilo, alithibitisha kutokea kwa vurugu. Alisema waliamua kuzuia maandamano hayo kwa kutumia mabomu kwa sababu urushaji wa mawe uliokuwa ukifanywa, ulionekana kuhatarisha hali ya usalama.
Alisisitiza kuwa maandamano hayo siyo si halali, na bodaboda hawakupaswa kufanya hivyo, bali walitakiwa kutii sheria bila shuruti, na kufuata taratibu za kudai kuonewa, na siyo kutishia kuharibu amani.
“Tulishaacha ule ukamataji wa bodaboda kwa kuwakimbiza, kwa sasa anapovunja sheria tunamfuatilia taratibu na kumkamata kwenye mazingira ambayo hayawezi kuhatarisha maisha yake,” alisema.
“Aliyefariki alifanya makosa na askari wetu wa usalama barabarani Koplo Lwehendela alimfuatilia mpaka akamkamata na alikubali makosa na kukubali kwenda kituo cha polisi. Baada ya kukubali, Lwehendela alimuelekeza Konstebo Edmond ambaye ni askari wanaovaa kiraia afuatane naye hadi kituoni.
“Lakini alitumia ujanja na kumweleza askari kuwa pikipiki ina matatizo hivyo askari apande ili waweze kuelekea kituoni, walipokuwa njiani ndipo dereva huyo alipokuwa kwenye barabara inayoelekea Tabora- Tinde, ndipo dereva huyo alipoongeza kasi ya pikipiki huku akiiyumbisha barabarani na alikuwa akimwambia askari wetu kuwa lazima wafe wote.
“Aliendelea kwenda kwa kasi huku wananchi wakiwa wanashangaa nini kilichotokea, ghafla waligonga nguzo pembeni ya barabara maeneo ya Huangija na kuanguka kwenye shimo, ndipo alipofariki dereva na askari wetu kujeruhiwa vibaya”, alisema.
Kamanda huyo alisema baada ya ajali hiyo juzi, jana walipata taarifa kuwa kuna mwanasiasa (jina wamelihifadhi) ambaye anadaiwa kuwahamasisha waendesha bodaboda takribani 1,000 kuandamana wakidai kuuawa. “Kuna mtu alikuwa anashinikiza madereva wafanye maandamano, lakini wengi wa madereva hao walionekana kutokubali na badala yake takribani 80 walifanya alivyokuwa amewaambia.”
“Tulipambana nao na tuliweza kurudisha amani. Na kwenye mchakato huo walipasua kioo cha mbele cha gari letu lenye namba PT 3705 kwa mawe waliyokuwa wakirusha. Lakini jeshi letu liliweza kuwakamata 28 na pia walikamata pikipiki 86 baada ya waandamanaji kukimbia na kuziacha,” alisema Murilo.
Taarifa za awali za tukio hilo, zinaeleza kuwa jeshi hilo lilitumia takribani saa sita ili kuwatawanya waendesha bodaboda hao, waliokuwa wakiandamana huku wakirusha mawe, kupinga kitendo cha mwenzao kufa wakidai kifo hicho kimesababishwa na askari polisi.

Hata hivyo, mshangao uliibuka kwa wananchi wa manispaa ya Shinyanga baada ya baadhi ya askari wa kikosi cha kutuliza ghasia, kuwatawanya waombolezaji waliokuwa katika msiba wa Mamla, kwenye nyumba aliyokuwa akiishi dereva huyo jana na kuzua taharuki zaidi.
Baadhi ya waendesha bodaboda, Simoni Bundala na Ramadhani Faraji walisema wameamua kuandama kwa madai ya kutaka kufikisha ujumbe ili serikali ione Polisi mkoani Shinyanga  isivyotenda haki, bali linawaonea.

Faraji alisema haiwezekani askari aliyevaa kiraia akamate pikipiki yenye makosa bila hata ya kuonesha kitambulisho, jambo ambalo ni hatari kwa kuhofia unyang'anyi wa pikipiki.

“Tukio la juzi bodaboda mwenzetu Joel (Mamla) mkazi wa mjini humo alikufa katika ajali iliyosababishwa na askari aliyemkamata kumkaba shingo hadi kusab
abisha ajali wakati akimlazimisha kwenda kituo cha polisi," alisema Bundala. 

Huko Mpanda, vurugu zimeibuka katika machimbo ya madini ya dhahabu  ya Isumamilo wilayani Mpanda katika mkoa wa Katavi  baina ya wachimbaji wadogo wapatao 6,000 na walinzi wa machimbo na kusababisha kibanda cha kupimia madini hayo  na ofisi kuchomwa na kuteketea kwa moto.
Kufuatia  vurugu hizo, walinzi wa machimbo hayo walilazimika kufyatua risasi za moto hewani  ili kuwatawanya wachimbaji hao wadogo.
Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, Benedict Mapujila amethibitika kutokea kwa tafrani hiyo na alisema vurugu hizo zilidumu zaidi ya saa moja zilitokea  jana  saa 2:30 asubuhi.
Alisema kuwa hadi sasa hakuna  mtuhumiwa yeyote  aliyekamatwa  wala hakuna  mtu yeyote aliyepoteza maisha na Polisi inaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.
Mapujila alisema vurugu hizo zilisababishwa  na walinzi wa machimbo hayo, kumkamata mchimbaji mdogo wa madini ya dhahabu akiwa na madini hayo akitaka kutoroka.
“Baada ya mchimbaji huyo mdogo wa madiniya dhahabu  kukamatwa na walinzi hao kumshambulia kwa kumpiga  mateke na marungu kitendo ambacho kiliwakasilisha  wachimbaji wenzake wakilalamika kuwa imekuwa ni tabia  ya walinzi wa machimbo hayo kuwapiga wachimbaji," alieleza Mapujila.
Akisimulia mkasa huo, alisema kuwa kundi kubwa la wachimbaji hao wadogo wakiwa na hasira, walijikusanya na kuanza kuvamia kibanda cha walinzi na ofisi ya kupimia madini hayo na kuteketeza kwa moto.
“Wakati wachimbaji hao  wakiteketeza kibanda hicho  kwa  moto walinzi wa machimbo hayo walilazimika kufyatua risasi za moto  hewani lakini  wachimbaji hao  hawakujali   waliendelea   bila   kujali risasi,” alieleza Kaimu Kamanda huyo.
Mkuu  wa   Mkoa  wa   Katavi, Raphael Muhuga   alifika  kwenye   eneo  hilo na kusikiliza kero  mbalimbali zilizotolewa na wachimbaji hao wadogo na aliwataka wafuate  taratibu  zilizowekwa na Serikali kulalamika.
“Kiitendo cha  wachimbaji kutorosha   dhahabu   bila  kupima kunasababisha  Serikali kukosa  mapato  yatokanayo na madini hayo," aliwaeleza.
Machimbo ya  Isumamilo  yamekuwa  maarufu kwa kipindi cha  miezi minne  sasa kutokana na kugundulika kwa dhahabu nyingi. Wachimbaji  wadogo  6,000  kutoka mikoa mbalimbali nchini hususani ya Kanda ya Ziwa, huchimba madini hapo.
Source:HabariLeo

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4816,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: BODABODA WABANANA NA POLISI, MABOMU MTINDO MZIMA
BODABODA WABANANA NA POLISI, MABOMU MTINDO MZIMA
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2017/06/bodaboda-wabanana-na-polisi-mabomu.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2017/06/bodaboda-wabanana-na-polisi-mabomu.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy