MAKONDA APOKEA MAGARI MABOVU YA POLISI KUYABADILI

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul C. Makonda akizungumza katika hafla ya kukabidhiwa magari mabovu kwa ajili ya Matengenezo. Leo June...

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul C. Makonda akizungumza katika hafla ya kukabidhiwa magari mabovu kwa ajili ya Matengenezo. Leo June 14, 2017 Oysterbay Jijini Dar es salaam
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul C. Makonda akikagua gwaride wakati wa hafla ya kukabidhiwa magari mabovu kwa ajili ya Matengenezo. Leo June 14, 2017 Oysterbay Jijini Dar es salaam
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Temeke, SACP Gilless B. Muroto akisoma taarifa ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Dar es salaam mbele ya Mkuu wa Mkoa huo wakati wa hafla ya kukabidhiwa magari mabovu kwa ajili ya Matengenezo. Leo June 14, 2017 Oysterbay Jijini Dar es salaam
Baadhi ya magari Mabovu yaliyokabidhiwa kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul C. Makonda kwa ajili ya Matengenezo. Leo June 14, 2017 Oysterbay Jijini Dar es salaam

Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo akifatilia hafla ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul C. Makonda kukabidhiwa magari mabovu kwa ajili ya Matengenezo. Leo June 14, 2017 Oysterbay Jijini Dar es salaam

Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo (Kulia) na Mkuu wa Wilaya ya kinondoni Mhe ally Happi (Kushoto) wakijadili jambo mara baada ya kumalizika hafla ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul C. Makonda kukabidhiwa magari mabovu kwa ajili ya Matengenezo. Leo June 14, 2017 Oysterbay Jijini Dar es salaam
Mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul C. Makonda akiyakagua magari mabovu aliyokabidhiwa kwa ajili ya Matengenezo. Leo June 14, 2017 Oysterbay Jijini Dar es salaam
Mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul C. Makonda akiyakagua magari mabovu aliyokabidhiwa kwa ajili ya Matengenezo. Leo June 14, 2017 Oysterbay Jijini Dar es salaam
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Temeke, SACP Gilless B. Muroto akitoa maelezo ya magari hayo mabovu mbele ya Mkuu wa Mkoa huo Mhe Paul C. Makonda wakati wa hafla ya kukabidhiwa magari mabovu kwa ajili ya Matengenezo. Leo June 14, 2017 Oysterbay Jijini Dar es salaam
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul C. Makonda akiteta jambo na Mkuu wa wilaya ya Kigamboni Mhe Hashim Mgandilwa, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe Ally Happi, Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare makori, na Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg john Lipesi Kayombo mara baada ya hafla ya kukabidhiwa magari mabovu kwa ajili ya Matengenezo. Leo June 14, 2017 Oysterbay Jijini Dar es salaam
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul C. Makonda sambamba na wanajeshi wa Jeshi La Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wakishirikiana kusukuma gari bovu tayari kwa safari ya kuelekea Mkoani Kilimanjaro kwa matengenezo, wakati wa hafla ya kukabidhiwa magari mabovu kwa ajili ya Matengenezo. Leo June 14, 2017 Oysterbay Jijini Dar es salaam

Na Mathias Canal, Dar es salaam

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul C. Makonda leo June 14, 2017 amekabidhiwa magari mabovu 26 ya Jeshi la Polisi kwa ajili ya kuyatengeneza kwa lengo la kuliongezea ufanisi jeshi la polisi katika kukabiliana na uhalifu katika Mkoa wa Dar es salaam.

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano ya magari hayo iliyofanyika katika kituo cha Polisi  Oysterbay ambapo ameelekeza magari hayo yote kwenda Mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya matengenezo pasina gharama za serikali, Mkuu huyo wa Mkoa alisema kuwa serikali imedhamiria kulifanya Jiji la Dar es salaam kuwa salama zaidi ili wafanyabiashara, Wanunuzi, na wananchi wote kufanya kazi zao kwa amani masaa 24.

Alisema kuwa safari ya mabadiliko katika Jeshi la polisi imefanywa kila mara lengo ikiwa ni kulifanya Jeshi la Polisi kuwa na weledi zaidi na kuondoa dhana na mazoea ambayo imeanza kujengeka kati ya Jeshi la Polisi na wananchi jambo ambalo limepelekea uwajibikaji kupungua kwa baadhi ya Askari.

Rc Makonda alisema kuwa pamoja na Jitihada mbalimbali zinazofanywa na Jeshi la Polisi Jijini Dar es salaam katika kukabiliana na uhalifu lakini zipo changamoto mbalimbali ambazo kwa njia moja ama nyingine zinakwamisha kufikiwa kwa malengo huku akizitaja changamoto hizo kuwa ni pamoja na Upungufu wa magari ya Doria,, Vifaa vya mawasiliano, Radio za mkononi na za magari, ufinyu wa bajeti ya mafuta na matengenezo magari.

Mhe Makonda ameyataja mambo manne ambayo ameamua kuyafanya ili kuliongezea nguvu jeshi la polisi katika kukabiliana na uhalifu ambayo ni pamoja na kufanya mchakato wa kutafuta Bastola 500, Vitanda pamoja na Radio Call, Baiskeli 500 pamoja na Pikipiki 200 kwa ajili ya Doria.

Kufunga Kamera kwenye vituo 20 vya Polisi Jijini Dar es salaam kwa ajili ya kupata taarifa na kuondoa usumbufu na mianya ya Rushwa, Kuweka kompyuta 8 kwenye vituo 20 sambamba na kuzindua utaratibu wa wahalifu kupigwa picha pindi wanapoingia kituoni na taarifa zao kuwekwa kwenye mfumo wa kompyuta ili kurahisisha upatikanaji wa taarifa za wahalifu.

mambo mengine ni pamoja na kuhakikisha Jeshi la Polisi linaondoa biashara zote haramu na Bandari Bubu sambamba na kufunga kamera za barabarani ili kubaini utovu wa nidhamu unaofanywa na madereva na kurahisisha upatikanaji haraka wa taarifa za uvunjaji wa sheria barabarani badala ya askari kukimbizana na madereva wanaovunja sheria.

Mhe Makonda pia amelielekeza Jeshi la Polisi kubaini maduka yote yanayouza vifaa vya magari na utambuzi wa mahali wanaponunua vifaa hivyo lengo ikiwa ni kubaini na kukomesha wizi wa vifaa vya magari unaofanyika katika maeneo mbalimbali Jijini Dar es salaam.

Amewasihi wananchi kuendelea kutoa taarifa za kufichua wahalifu sambamba na kuiombea serikali inayoongozwa na Rais Magufuli ili kuvuka kipindi hiki kigumu cha kuwakabili wanyonyaji na wabadhilifu wa rasilimali za watanzania.


Mhe Makonda pia amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli kwa kumteua kamanda Simon Sirro kuwa Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) kwani kwa muda mfupi aliofanya nae kazi ameonyesha weledi mkubwa katika uwajibikaji hususani katika kuukabili uhalifu katika Kanda ya Kipolisi ya Dar es salaam.

Awali akisoma taarifa kuhusu Uhalifu katika Jiji La Dar es salaam kwa niaba ya Inspekta Jenerali wa polisi (IGP) na askari wote wa Mkoa wa Dar es salaam Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Temeke, SACP Gilless B. Muroto alisema kuwa hali ya uhalifu imepungua kutoka matukio 56,856 yaliyoripotiwa kwa mwezi Januari hadi Mwezi Mei mwaka 2017 ikilinganishwa na Matukio 59,695 yaliyoripotiwa katika kipindi cha Mwezi Januari hadi Mwezi Mei mwaka 2016.

Kamanda Muroto Alisema kuwa Matukio makubwa ya jinai yaliyoripotiwa mwaka 2017 ni 5,879 ambapo mwezi Januari hadi Mwezi Mei 2016 kulikuwa na matukio 8,252 pungufu ya matukio 2,373 sawa na asilimia 28.7%.

Alisema kuwa kupungua kwa uhalifu sambamba na matukio makubwa ya jinai ni kutokana na juhudi mbalimbali za kudhibiti uhalifu zinazofanywa na Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na wananchi ambapo Oparesheni mbalimbali hupelekea wahalifu kukamatwa kwa wingi.

MWISHO

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4816,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: MAKONDA APOKEA MAGARI MABOVU YA POLISI KUYABADILI
MAKONDA APOKEA MAGARI MABOVU YA POLISI KUYABADILI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjxS4l7Z5o3FCeHHzVQ4NloppiiVrX0TfnisoTgwVyBHtFbCgj1wdWksE24gHDVuyW8f8BUMFtZsB7N0Z1k2I-qVZR_bXeF6D5SLDCo4sOtd7_XrLFrZ4TZkJ8V8cm_JPbBRqJ8j02I9xo/s640/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjxS4l7Z5o3FCeHHzVQ4NloppiiVrX0TfnisoTgwVyBHtFbCgj1wdWksE24gHDVuyW8f8BUMFtZsB7N0Z1k2I-qVZR_bXeF6D5SLDCo4sOtd7_XrLFrZ4TZkJ8V8cm_JPbBRqJ8j02I9xo/s72-c/1.jpg
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2017/06/makonda-apokea-magari-mabovu-ya-polisi.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2017/06/makonda-apokea-magari-mabovu-ya-polisi.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy