PROFESA JIN SANG LEE WA KOREA AWAFUNDA WATANZANIA SAFARIK YA VIWANDA

Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF) kwa kushirikiana na Profesa Jin Sang LEE kutoka Chuo Kikuu cha New York – Korea (SUNY Korea) ...

Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF) kwa kushirikiana na Profesa Jin Sang LEE kutoka Chuo Kikuu cha New York – Korea (SUNY Korea) kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) waliandaa mhadhara wa kubadilisha uzoefu ili kuweza kufikia malengo ya uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025. Mhadhara huo ulifanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF na kufunguliwa na Mheshimiwa Anthony Mtaka – Mkuu wa Mkoa wa Simiyu. Akizungumza katika mhadhara huo, Mheshimiwa Mtaka alisema, nchi yetu imejipanga kufikia uchumi wa kati kwa kuwa na sera na mikakati mbalimbali. Aliongeza kwa kusema kilichobakia ni kuendelea kuitekeleza sera na mikakati hiyo ili kutimiza ndoto ya kuwa na uchumi wa kati. Kwa upande wake, Dkt. Tausi Kida- Mkurugenzi Mtendaji ESRF alisema, mhadhara huo umekuja wakati muafaka kwa kuwa nchi yetu imedhamiria kufikia Uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025, ambapo sekta binafsi itakuwa injini ya ukuwaji wa uchumi. [caption id="attachment_3553" align="aligncenter" width="1404"] Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida (kushoto) akizungumza na Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mheshimiwa Anthony Mtaka ofisini kwake kabla ya ufunguzi wa warsha ambayo ilijadili mafanikio ya Korea Kusini katika viwanda na nini kinaweza kuigwa na watanzania kufikia uchumi wa kati mwaka 2025 iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.[/caption] Profesa Jin Sang LEE katika Mhadhara wake alianza kubadilishana uzoefu kwa kuelezea mapinduzi ya uchumi katika Korea ya kusini kuanzia miaka ya 1960. Alisema katika miaka hiyo Serikali ya Korea ya Kusini iliweka vipaumbele kadhaa ikiwamo kuondoa umaskini na kukuza viwanda. Katika miaka hiyo serikali ilijikita katika uchumi wa viwanda vidogo vidogo na wakijitahidi kuuza ndani na nje bidhaa ndogondogo. Katika miaka ya sabini Korea ilipiga hatua nyingine kwa kupanua techonoljia ili kuongeza tija katika viwanda vyake, Hayo yalikuwa yakifanywa kwa ushirikiano wa serikali na sekta binafsi. Katika miaka ya themanini, nchi ilizidi kujikita katika sayansi, teknolojia na ubunifu, waliweza kuwafundisha watu wake ili kuwa na wataalamu wengi ambao watasaidia katika kubuni mambo muhimu ya maendeleo. Katika miaka ya tisini, Korea Kusini ilinza kujikita katika kujiimarisha katika teknolojia ambayo iliyohitajika kimataifa kama vile teknolojia ya Tehama. Na katika miaka ya 2000, nchi ilieweza kuwa na mapinduzi makubwa ya viwanda vya kubuni bidhaa mbalimbali kama vile simu za mikononi, komptuta, magari n.k. Hayo yote ni matokeo ya uzalendo, kusomesha wataalamu, kuanzisha na kusimamia masuala ya utafiti na maendeleo, kufanyakazi kwa bidii kwa wananchi wa Korea Kusini. Masuala ya Utafiti na Maendeleo ni nguzo imara katika kuendesha sekta mbalimbali katika nchi. Alisisitiza pia , ushirikiano kati ya serikali na vyuo vikuu amboko ndio sehemu ambayo kutafumbuliwa na kukuzwa kwa sayansi, teknolojia na ubunifu. [caption id="attachment_3554" align="aligncenter" width="1404"] Mkuu wa Idara ya Maarifa na Ubunifu wa ESRF Bi. Margareth Nzuki (kulia) akiongozana na mgeni mzungumzaji Profesa Jin-Sang LEE kutoka Chuo Kikuu cha New York-( SUNY)- Korea (katikati) kuelekea kwenye ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.[/caption] Profesa Lee alisema katika upande wa viwanda Tanzania inatakiwa kuwa na viwanda vya msingi, masoko na kuwa na uelewa wa soko la kimataifa. Aidha kama taifa linatakiwa kuwa na nadharia zinazofaa kwa ajili ya kubeba mfumo huo wa viwanda kama Pia vyuo vikuu vinatakiwa kutengeneza wataalamu wa ngazi za juu watakaoweza kusaidia sekta mtambuka kwenye masuala ya sayansi na teknolojia kufanyakazi. Aidha ameshauri serikali kujenga uwezo wa viwanda nchini kwa kuviwezesha kushindana huku ikitilia maanani soko la ndani na nje. Katika hilo inatakiwa kukuza ujasirimali kwa kuwezesha maarifa katika menejimenti, kujiamini na kutengeneza ushirika na makampuni ya kigeni [caption id="attachment_3555" align="aligncenter" width="1404"] Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mheshimiwa Anthony Mtaka akitoa neno fupi la ufunguzi wa warsha ambayo ilijadili mafanikio ya Korea Kusini katika viwanda na nini kinaweza kuigwa na watanzania kufikia uchumi wa kati mwaka 2025 iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.[/caption]

Aidha alihimiza uzalendo na kujitosa huku mtu akiwa na mawazo, maono na mikakati ya kusonga mbele huku utekelezaji wa mambo kuelekea katika ustawi wa viwanda ukiambatana na sera .

Profesa Lee aliyasema hayo katika warsha ambayo ilijadili mafanikio ya Korea Kusini katika viwanda na nini kinaweza kuigwa na watanzania kufikia uchumi wa kati mwaka 2025. Alikuwa akizungumza kama mgeni mwalikwa katika warsha iliyoshirkisha wataalamu mbalimbali nchini Tanzania kutoka serikali na sekta binafsi

Akizungumzia sekta binafsi alitaka, kuchukua pale ambapo serikali itakuwa imeishia katika kutengeneza mifumo ya kuwezesha uchumi mkubwa kwa kuwa na utaratibu wa kuwezesha sayansi, teknolojia katika kukuza shughuli zao.

[caption id="attachment_3556" align="aligncenter" width="1404"] Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF Dkt. Tausi Kida akitoa neno la ukaribisho kabla yakumkaribisha mgeni rasmi Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mheshimiwa Anthony Mtaka kufungua warsha ambayo ilijadili mafanikio ya Korea Kusini katika viwanda na nini kinaweza kuigwa na watanzania kufikia uchumi wa kati mwaka 2025 iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.[/caption]

Naye mtaalamu wa Maendeleo ya Sekta binafsi Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo (UNDP) Ernest Salla akizungumza wakati wa kufunga warsha hiyo alisema kwamba ipo haja ya watanzania kuwa wazalendo na kuhakikisha wanatimiza ndoto ya nchi ya viwanda kwa kuwekeza zaidi.

Aidha alisema kutokana na kuwapo kwa maendeleo makubwa ya teknolojia na sayansi Tanzania inaweza kutumia nafasi hiyo kusonga mbele kwa kasi kuelekea sekta ya viwanda

Alitaka kwa sasa sekta binafsi kuhakikisha inatumia fursa zilizopo kuleta maendeleo badala ya kuwa na woga na hofu kutokana na vikwazo vya hapa na pale.

[caption id="attachment_3557" align="aligncenter" width="1404"] Mgeni mzungumzaji Profesa Jin-Sang LEE kutoka Chuo Kikuu cha New York-( SUNY)- Korea akielezea jinsi Korea Kusini ilivyofanikiwa katika uchumi wakati wa warsha ambayo ilijadili mafanikio ya Korea Kusini katika viwanda na nini kinaweza kuigwa na watanzania kufikia uchumi wa kati mwaka 2025 iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.[/caption]   [caption id="attachment_3558" align="aligncenter" width="1404"] Profesa Jin-Sang LEE kutoka Chuo Kikuu cha New York-( SUNY)- Korea akiwasilisha data mbalimbali za nchi ya Korea Kusini wakati wa warsha ambayo ilijadili mafanikio ya Korea Kusini katika viwanda na nini kinaweza kuigwa na watanzania kufikia uchumi wa kati mwaka 2025 iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.[/caption]   [caption id="attachment_3563" align="aligncenter" width="1404"] Mtaalamu wa Maendeleo ya Sekta binafsi Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo (UNDP) Ernest Salla akizungumza wakati akifunga warsha ambayo ilijadili mafanikio ya Korea Kusini katika viwanda na nini kinaweza kuigwa na watanzania kufikia uchumi wa kati mwaka 2025 iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.[/caption] [caption id="attachment_3559" align="aligncenter" width="1404"] Katibu Mkuu Tanzania Science Academy, Dk. Gratian Bamwenda akiendesha kipindi cha majadiliano wakati wa warsha ambayo ilijadili mafanikio ya Korea Kusini katika viwanda na nini kinaweza kuigwa na watanzania kufikia uchumi wa kati mwaka 2025 iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.[/caption] [caption id="attachment_3560" align="aligncenter" width="1404"] Mwenyekiti wa Shirikisho la wenye Viwanda nchini (CTI), Dkt. Samuel Nyantahe akitoa maoni wakati wa warsha ambayo ilijadili mafanikio ya Korea Kusini katika viwanda na nini kinaweza kuigwa na watanzania kufikia uchumi wa kati mwaka 2025 iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.[/caption] [caption id="attachment_3561" align="aligncenter" width="5184"] Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Laurean Bwanakunu akihoji jambo warsha ambayo ilijadili mafanikio ya Korea Kusini katika viwanda na nini kinaweza kuigwa na watanzania kufikia uchumi wa kati mwaka 2025 iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.[/caption] [caption id="attachment_3562" align="aligncenter" width="1404"] Rais wa Vicoba endelevu Tanzania, Devotha Likokola akiuliza swali wakati wa warsha ambayo ilijadili mafanikio ya Korea Kusini katika viwanda na nini kinaweza kuigwa na watanzania kufikia uchumi wa kati mwaka 2025 iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.[/caption] [caption id="attachment_3564" align="aligncenter" width="1404"] Profesa Jin-Sang LEE (katikati) kutoka Chuo Kikuu cha New York-(SUNY)- Korea akijibu baadhi ya maswali kutoka kwa washiriki wa warsha ambayo ilijadili mafanikio ya Korea Kusini katika viwanda na nini kinaweza kuigwa na watanzania kufikia uchumi wa kati mwaka 2025 iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mheshimiwa Anthony Mtaka na kushoto ni Mtaalamu wa Maendeleo ya Sekta binafsi Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo (UNDP) Ernest Salla.[/caption] [caption id="attachment_3566" align="aligncenter" width="1404"] Pichani juu na chini ni sehemu ya washiriki wa warsha ambayo ilijadili mafanikio ya Korea Kusini katika viwanda na nini kinaweza kuigwa na watanzania kufikia uchumi wa kati mwaka 2025 iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.[/caption]

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4816,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: PROFESA JIN SANG LEE WA KOREA AWAFUNDA WATANZANIA SAFARIK YA VIWANDA
PROFESA JIN SANG LEE WA KOREA AWAFUNDA WATANZANIA SAFARIK YA VIWANDA
http://www.thebeauty.co.tz/wp-content/uploads/2018/01/IMG_0011.jpg
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2018/01/profesa-jin-sang-lee-wa-korea-awafunda.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2018/01/profesa-jin-sang-lee-wa-korea-awafunda.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy