Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF) kwa kushirikiana na Profesa Jin Sang LEE kutoka Chuo Kikuu cha New York – Korea (SUNY Korea) ...
Aidha alihimiza uzalendo na kujitosa huku mtu akiwa na mawazo, maono na mikakati ya kusonga mbele huku utekelezaji wa mambo kuelekea katika ustawi wa viwanda ukiambatana na sera .
Profesa Lee aliyasema hayo katika warsha ambayo ilijadili mafanikio ya Korea Kusini katika viwanda na nini kinaweza kuigwa na watanzania kufikia uchumi wa kati mwaka 2025. Alikuwa akizungumza kama mgeni mwalikwa katika warsha iliyoshirkisha wataalamu mbalimbali nchini Tanzania kutoka serikali na sekta binafsi
Akizungumzia sekta binafsi alitaka, kuchukua pale ambapo serikali itakuwa imeishia katika kutengeneza mifumo ya kuwezesha uchumi mkubwa kwa kuwa na utaratibu wa kuwezesha sayansi, teknolojia katika kukuza shughuli zao.
[caption id="attachment_3556" align="aligncenter" width="1404"] Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF Dkt. Tausi Kida akitoa neno la ukaribisho kabla yakumkaribisha mgeni rasmi Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mheshimiwa Anthony Mtaka kufungua warsha ambayo ilijadili mafanikio ya Korea Kusini katika viwanda na nini kinaweza kuigwa na watanzania kufikia uchumi wa kati mwaka 2025 iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.[/caption]Naye mtaalamu wa Maendeleo ya Sekta binafsi Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo (UNDP) Ernest Salla akizungumza wakati wa kufunga warsha hiyo alisema kwamba ipo haja ya watanzania kuwa wazalendo na kuhakikisha wanatimiza ndoto ya nchi ya viwanda kwa kuwekeza zaidi.
Aidha alisema kutokana na kuwapo kwa maendeleo makubwa ya teknolojia na sayansi Tanzania inaweza kutumia nafasi hiyo kusonga mbele kwa kasi kuelekea sekta ya viwanda
Alitaka kwa sasa sekta binafsi kuhakikisha inatumia fursa zilizopo kuleta maendeleo badala ya kuwa na woga na hofu kutokana na vikwazo vya hapa na pale.
[caption id="attachment_3557" align="aligncenter" width="1404"] Mgeni mzungumzaji Profesa Jin-Sang LEE kutoka Chuo Kikuu cha New York-( SUNY)- Korea akielezea jinsi Korea Kusini ilivyofanikiwa katika uchumi wakati wa warsha ambayo ilijadili mafanikio ya Korea Kusini katika viwanda na nini kinaweza kuigwa na watanzania kufikia uchumi wa kati mwaka 2025 iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.[/caption] [caption id="attachment_3558" align="aligncenter" width="1404"] Profesa Jin-Sang LEE kutoka Chuo Kikuu cha New York-( SUNY)- Korea akiwasilisha data mbalimbali za nchi ya Korea Kusini wakati wa warsha ambayo ilijadili mafanikio ya Korea Kusini katika viwanda na nini kinaweza kuigwa na watanzania kufikia uchumi wa kati mwaka 2025 iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.[/caption] [caption id="attachment_3563" align="aligncenter" width="1404"] Mtaalamu wa Maendeleo ya Sekta binafsi Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo (UNDP) Ernest Salla akizungumza wakati akifunga warsha ambayo ilijadili mafanikio ya Korea Kusini katika viwanda na nini kinaweza kuigwa na watanzania kufikia uchumi wa kati mwaka 2025 iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.[/caption] [caption id="attachment_3559" align="aligncenter" width="1404"] Katibu Mkuu Tanzania Science Academy, Dk. Gratian Bamwenda akiendesha kipindi cha majadiliano wakati wa warsha ambayo ilijadili mafanikio ya Korea Kusini katika viwanda na nini kinaweza kuigwa na watanzania kufikia uchumi wa kati mwaka 2025 iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.[/caption] [caption id="attachment_3560" align="aligncenter" width="1404"] Mwenyekiti wa Shirikisho la wenye Viwanda nchini (CTI), Dkt. Samuel Nyantahe akitoa maoni wakati wa warsha ambayo ilijadili mafanikio ya Korea Kusini katika viwanda na nini kinaweza kuigwa na watanzania kufikia uchumi wa kati mwaka 2025 iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.[/caption] [caption id="attachment_3561" align="aligncenter" width="5184"] Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Laurean Bwanakunu akihoji jambo warsha ambayo ilijadili mafanikio ya Korea Kusini katika viwanda na nini kinaweza kuigwa na watanzania kufikia uchumi wa kati mwaka 2025 iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.[/caption] [caption id="attachment_3562" align="aligncenter" width="1404"] Rais wa Vicoba endelevu Tanzania, Devotha Likokola akiuliza swali wakati wa warsha ambayo ilijadili mafanikio ya Korea Kusini katika viwanda na nini kinaweza kuigwa na watanzania kufikia uchumi wa kati mwaka 2025 iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.[/caption] [caption id="attachment_3564" align="aligncenter" width="1404"] Profesa Jin-Sang LEE (katikati) kutoka Chuo Kikuu cha New York-(SUNY)- Korea akijibu baadhi ya maswali kutoka kwa washiriki wa warsha ambayo ilijadili mafanikio ya Korea Kusini katika viwanda na nini kinaweza kuigwa na watanzania kufikia uchumi wa kati mwaka 2025 iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mheshimiwa Anthony Mtaka na kushoto ni Mtaalamu wa Maendeleo ya Sekta binafsi Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo (UNDP) Ernest Salla.[/caption] [caption id="attachment_3566" align="aligncenter" width="1404"] Pichani juu na chini ni sehemu ya washiriki wa warsha ambayo ilijadili mafanikio ya Korea Kusini katika viwanda na nini kinaweza kuigwa na watanzania kufikia uchumi wa kati mwaka 2025 iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.[/caption]
COMMENTS