Na Beda Msimbe JARIDA la Mtandaoani la Golden woman limeandika makala ya kumweleza msanii wa muziki wa injili nchini Christina Shusho kam...
Na Beda Msimbe
JARIDA la Mtandaoani la Golden woman limeandika makala ya kumweleza msanii wa muziki wa injili nchini Christina Shusho kama moja ya wanamuziki wachache wa Injili wanaofanya vyema kimuziki hapa nchini na duniani kote ambako muziki wa injili wa lugha ya kiswahili unasikika.
Pia jarida hilo limeelezea maana ya nyimbo za mwanadada huyo katika maisha ya binadamu mintarafu kuabudu, kuomba na kusifu.
Shusho akiwa katika miaka yake ya arobaini ameelezwa na mwandishi wa makala hayo katika lugha ya kiingereza, kuwa ni msanii ambaye amekuwa na wafuasi wengi zaidi mtandaoni wanaofuatilia muziki wake katikiakipindi cha miaka 20 sasa.
Charles Mwangi alinukuliwa na https://goldenwoman.org/ kwamba unapomtafuta msanii wa muziki wa injili katika lugha ya kiswahili kwa namba ya vibao alivyotoa, idadiya watu wanaotembelea kupiga muziki wake na anayeongoza katika grafu, Christina Shusho anaongoza
mpaka sasa.
Anasema kwa dunia yenye wazungumzaji wa kiswahili milioni 150, Christina Shusho kwa takwimu anaonesha kutamba miongoni mwa wanamuziki wa Injili wa kike.
Akiwa katika miaka yake ya arobaini, Shusho amekuwa na sauti ile ile aliyoanzia safari miaka 20 iliyopita, huku akiendelea kutoa vibao vikali zaidi ya kumsifu Mungu, kumtukuza na kuomba hisani yaani muziki wa maombi. Ukipanga idai ya muziki ambao ameshautoa mpaka sasa ukatafuta wastani unabaini kwamba kila mwezi mwanadada huyo amekuwa akitoa kibao kimoja cha kuzungumza na Mungu ama katika maombi au katika kusaka hisani.
Binti huyo aliyezaliwa Kigoma, kwa kuendelea kung'ang'ania katika muziki huo ameonesha umahiri katika huduma yake kwa kutokuwa mchoyo wa nyimbo kwa kuendelea kuzitengeneza huku wakati mwingine akishirikiana na waimbaji vinara na hata chipukizi.
Kwa kizazi cha miaka ya 2000 watakuwa wanamwelewa vyema kwa nyimbo zake kama “Wa Kuabudiwa” iliyomo katika albamu ya 'Unikumbuke.”
Kiukweli wasanii wengi wa muziki wa injili huja na kuondoka,lakini mwanadada huyu ambaye mkononi ana albamu nane zenye jumla ya nyimbo 80, amekuwa tofauti kwani mwaka hadi mwaka amekuwa akikonga nyoyo za wapenzi wa muziki wa injili huku kila albamu yake ikiwa na ujumbe mahsusi kwa wanadamu unamhusu Mungu.
Akiwa na historia ya kuanza kuimba tangu katika shule ya mafunzo ya dini ya watoto wadogo (Sunday School) mkoanio Kigoma, alipofika kuanzamaisha Dar es Salaam aliingia katika kwaya ya kabla ya kuanza kurekodi solo muziki wa injili; na kutoka wakati huo hajarudi Snyuma akichangia kwa kiasi kikubwa uamsho wa mapenzi kwa Mungu kupitia nyimbo zake.
Sauti yake ya kuvutia na kupendeza, inayokua ikiwa katika nakshi ya mambo ya kawaida yanayofuata mistari ya Kibiblia imeondokea kupendwa na watu wengi na kumpeleka kimataifa.
Mwaka huu akiwa anadaa albamu ya shusha nyavu tayari vibao vyake ikiwamo ya shusha nyavu vimekuwavitamba mtandaoni vikionesha kwamba vitakimbiza kuliko "Kitu Gani Kinitenge Na Upendo wa Bwana," na "Nipe Macho Nione". Ukifanya tathmini ya muziki wake unaona kwamba unasambaa kwa kasi kama moto katika vichaka kutoka nyumbani Tanzania, Afrika Mashariki na duniani.
Katika kuonesha kwamba anakubalika mdada huyu ameshafanya ziara za maonesho katika nchi za Marekani, Uingereza, Austria, Canada na kadha wa kadha Huku Kenya ikiwa kama nyumbani kwake.
Katika utafiti uliofanywa na mwanafunzi mmoja wa Chuo Kikuu cha SAUT kilichopo Mwanza binti huyu aliyefungua chaneli ya You Tube Machi 15,2013 ilipofika Septemba 2021 alikuwa na watu waliotembelea chaneli hiyo milioni 43 ambapo ukitafsiri ni kwamba kila siku muziki wake umekuwa ukitembelewa na watu 15,000 katika kipindi cha miaka minane na hii si idadi ndogo hata kidogo.
Ukiamngalia zaidi unaona kwamba ukijumlisha milioni 43 kwenye chaneli yake naidadi ya watu waliotembelea saiti nyingine mbalimbali wapatao milioni 40 unaona kwamba hakika Shusho yupo juu katika muziki wa injili wa kiswahili.
Utafiti wa mwanafunzi huyo unaonesha kwamba kwa vijana wanaouzamuziki kidijiti huwahawakosi mnyimbo za mwanamuziki huyo na kumfanya kuwa mwanamuziki pendwa wa injili kwa sasa.
Ukipanga albamu za Christina Shusho toka anaanza kuimba kwa mpangilio huwezi kupata hadithi nzuri ya Biblia au hadithi inayomhusu Christina Shusho, lakini ukichukua albamu zote ukasikiliza kwa mpangilio wa mahitaji utagundua kwamba kuna mambo muhimu ambayo Shusho anataka kukueleza kuhusu safari nzima ya maisha hapa duniani .
Katika albamu hizo nane bila mpangilio wa siku zilipotoka bali kuzingatia mtiririko unaona amefanyakazi ya ziada kuzungumzia wokovu na safari yake pia kuhusu mwenendo wa walimwengu katika vita vya utu dhidi ya karaha zilizopo ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kuwa mwisho mwema.
Hadithi yake kisanii ipo " Nipe Macho Nione"; "Nataka Nimjue"; "Ongoza Hatua Zangu";"Wataka akutendee nini":" Unikumbuke"; "Shusha Nyavu" na" Relax". Katika dunia yetu hii iliyojaa vurugu kuanzia katika maisha ya kimwili hadi ya kiroho tangu wazazi wetu wa kwanza kuvurugana na Mungu kwa kuonesha kiburi cha kutojali maagizo waliyopewa, haja ya kuwa na macho ya kuuona ukweli ni lazima iwepo , macho ya katika roho si macho tu yanayotuwezesha kuona na kutafakari mambo ya kidunia.
Ndio kusema Shusho amefanya vyema katika kutunga simulizi la maisha ya biandamu kupitiamistari yaBiblia na nyimbo zake zinazokupa maono ya uwezo wa wewe kuamua kati ya mambo mengi unayotakiwa kuyaamua ikiwamo ufuatiliaji wa maagizo mbalimbali ambayo Mungu aliyatoa moja kwa moja kwa watu watumishi wake waaminifu kama Musa, Adam na hata Abraham.
Biblia imejipambanua kama kitabu ambacho kina maelekezo na wakati mwingine ya kimigongano, lakini kama huyo unayetaka kumwabudu anataka umwabudu katika roho na kweli unalazimika kuomba macho, macho yenye upekee wa kumuona Mungu katika ukuu wake.
Christina katika albamu zake zote anataka kuonesha wa kumtegemea katika dunia hii inayoamini uwapo wa Mungu na manabii wake, ukiiangalia nyimbo zote utaona kwamba ni maombi kwa Mungu maombi ya kuonewa huruma na kusaidiwa kuona katika safari ya kufika mbinguni.
mwisho
COMMENTS