Na Rahel Pallangyo WAKATI wa safari yangu ya Tanga hivi karibuni katika michuano ya Ngao ya Jamii kwenda kuandika habari na kupiga picha za...
Na Rahel Pallangyo
WAKATI wa safari yangu ya Tanga hivi karibuni katika michuano ya Ngao ya Jamii kwenda kuandika habari na kupiga picha za michezo, nilipita karibu kabisa na jumba la sinema la Majestic lililopo barabara ya Mkwakwani.
Jumba hilo la Shirika la Nyumba (NHC) ni la zamani na mpaka sasa linaendelea kuonesha filamu na kufanya kazi nyingine za burudani. Ikumbukwe kuwa ka tika miaka ya 1980 ambako kulikuwa na mdororo wa kiuchumi hamu ya kwenda sinema ilipungua kutokana na majumba hayo kutokuwa na bidhaa mpya inayovu tia wakawa wanababia na kuchosha wapenzi wa sinema.
Katika jengo hilo Tanga wapenzi wa sinema wa naopenda kuona vitu hivyo katika ‘Big Screen’ walipo teza burudani hiyo kutokana na kufungwa kwa majumba ya sinema ambayo yalikuwa na uwezo wa kuonesha mm 35 bado wanaendelea kuona kwa kutumia jengo lao am balo ujenzi wake ni urithi safi wenye kumbukumbu.
Ingawa wapenzi wa bu rudani hiyo kabla ya miaka ya 1980 hawakuweza kufikiri hata mara moja kwamba kutakuwa na kufungwa kwa majumba ya sinema ukiz ingatia wananchi walikuwa wanafurika kuona sinema za kidosi au za kizungu.
Mathalani Dar es Salaam majumba yote yaliyokuwa yakionesha filamu kama Drive in, Empire, Avalon, Empress, Odeon, Cameo, New Chox na Star Light yamegeuka kuwa majumba ya kazi nyingine na mpaka kesho inaonekana haiweze kani tena kurejea katika mazingira ya zamani.
Ukiachia Dar es Salaam mji wenye starehe za kipekee wa Morogoro ulikuwa na Shani Cinema na Sapna. Vivyo hivyo katika Mkoa wa Lindi ambapo pale penye ukumbi unaoitwa Y2K kulikuwa na jengo kubwa la filamu. Mpaka mwishoni mwa miaka ya 1990 ilikuwa ni ada kutafuta magazeti kuona nini kinaendelea katika majumba ya sinema ya Dar es Salaam na hata huko mikoani katika mbao za matangazo ya ma jumba hayo.
Ingawa majumba mengi yamekuwa nyumba za ibada, maduka au yamefungwa au kubomolewa na majengo mengine kusimamishwa badala yake, Tanga wame onesha kwamba Majestic yao ambayo ilitumika kuonesha filamu ya kwanza huru, Shamba Kubwa, inaweza kuendelea kuwapo.
Majestic Theatre haikuwa peke yake katika mji huu am bao kuingia ni rahisi na ku toka ni kazi kwani kulikuwa na Regal, Novelty na Tanga Cinema lakini leo hii unaona kwamba Majestic ndio wa meendelea kuwapo mpaka kesho na bado wanaonesha inawezekana kuendelea kuonesha filamu.
Historia inasema katika Jiji hilo jengo la kwanza kufa ni Tanga cinema, ikafuata Novelty, Regal na mwisho Majestic ambao kwa sasa wamefufuka.
Nilipata nafasi ya kuzun gumza na mmoja wa walimu wa sanaa ya filamu, Profesa Martin Mhando kuhusiana na jengo la Tanga na kunia mbia ndilo lililotumika kuon esha filamu ya kwanza huru ya Shamba Kubwa ambayo pia ploti yake ilikuwa Mkoa wa Tanga.
Aliniambia ingawa Majes tic ya Tanga haina uhusiano na jengo la jina kama hilo Zanzibar ambalo lilipiganiwa kuimarishwa na kuendelea na kazi yake ya kuonesha filamu, anaamini utamaduni wa kuona sinema unarejea kutokana na juhudi mbalim bali za watengeneza filamu hapa nchini na duniani kwa ujumla.
Shamba Kubwa moja ya filamu zilizoanzisha tena utengenezaji wa filamu Tan zania baada ya kampuni ya filamu kufa na filamu zake kubaki Zimbabwe zilipoenda kwa ‘treatment’. Shamba Kubwa sinema ya mwaka 1994 ilimtambulisha Jimmy Mponda kama J. Plus wengine wakimuita Jimmy Master ilipata jina kubwa na pia kuleta vuguvugu mpya ya matamanio ya burudani kupitia majumba ya sinema.
“Majestic Theatre ya Tanga naijua kama moja ya majumba ambayo yalibaki kuonesha filamu kwa muda mrefu wakati majumba mengine yalipokufa kabisa Tanzania. Mwaka 1995 ilipo tengenezwa Bongo Movie ya kwanza iliyoitwa “Shamba Kubwa” na Amri Bawji na Kassim El Siagi, filamu hiyo ilioneshwa Majestic, Tanga,” anasema Profesa Mhando na kusema kuwa hali iliyokuta majumba ya sinema nchini Tanzania Bara na Visiwani matokeo ya mdororo wa kiuchumi.
“Uchumi ulidorora miaka ya 1980,” Mhando alisema. “Tiketi zilikuwa zimegharimu dola za Marekani 1-2, lakini tulijua ikifika dola 3 uchumi wa sinema utaporomoka na ndivyo ilivyokuwa. Watu hawakuwa na uwezo wa kutazama sinema. Video zili kuja na kukaa ndani. Kufikia 1996, sinema zote zilikuwa zimefungwa.”
Anasema ingawa hana uhakika kuwa Majestic ya Tanga na Majestic Zanzibar zilihusiana ingawa inawezekana, maana waliokuwa wa nahodhi majumba ya sinema walikuwa Watanzania wenye asili ya India, kuendelea kuwepo kwa jengo hilo likiendelea na kazi ya kuleta burudani inatia matumaini si tu kwa urithi wa kizazi kijacho bali na uhakika wa maeneo ya kuonesha uwezo wa binadamu katika skrini kubwa.
Anasema alikuwa anapigania sana Majestic ya Zanzibar na anafikiria safari ni nzuri kwa kuwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ime kuwa tayari kulifufua Jumba la Majestic kwa kupata misaada ya kimataifa. “Mimi nimekuwa nikip igia kelele na kuliwekea kifua ili lisibadilishiwe matumizi kama majumba mengine. Kwa sasa jumba hilo limetolewa kwa Muungano wa taasisi tano kusimamia ukarabati na kulipa matumizi mengi zaidi,” anasema Pro fesa huyo ambaye amebobea katika filamu.
Taasisi hizo tano ni ZIFF, Hifadhi, Sauti za Busara, Women Reclaim Center na Abdul Mawazo. Anasema Unesco imesaidia kupata kia si cha fedha toka serikali ya Japan ili kufanya upembuzi yakinifu na kuanza mipango ya kukarabati jumba hilo. Ingawa kuna utata katika uhodhi/umiliki wa jumba le nyewe maana nalo lilitaifish wa wakati wa mapinduzi na sasa familia iliyokuwa inali miliki imerudi tena ili kutaka kuliendesha, mazungumzo yanaendelea kuhusu umiliki na hivyo kazi ya upembuzi imesimama. Unesco ndiyo inasimamia ukarabati.
Hekaheka za kurejesha jumba hilo la Zanzibar linaenda na ukweli kuwa majumba ya sinema ka tika miaka ijayo ni muhimu katika kuhakikisha ukuaji mzuri wa tasnia kwani hata Ulaya walikoendelea bado majumba ya sinema yanafan yakazi hasa kuwezesha pato la kwanza katika kuingia katika majukwaa mengine. Majestic ya Zanzibar ni moja ya majumba ya kwanza ya sinema barani Afrika, katika miaka ya 1920. Zanzibar ilikuwa na majengo ya sinema 53 yakajifia na kubaki mawili likiwemo hilo la Majestic.
Mtengenezaji wa filamu Mwingereza Nick Broom field, anayejulikana kwa filamu za Biggie na Tupac, Aileen Wuornos: The Selling of a Serial Killer na Battle For Haditha anafurahishwa na juhudi za kurejeshwa kwa majumba ya sinema.
Akizungumzia jumba la Zanzibar ambalo halina paa kwa sasa watu wakiangalia sinema wazi alisema: “In gawa sinema haina paa, watu wanaitumia na kuweka pro jekta yao wenyewe. Pengine ina kumbukumbu nyingi kwao. Ni mahali ambapo watu walienda kwa kustare he na kukutana na rafiki zao wa kike wa kwanza.
“Sinema ni uzoefu wa pamoja. Kama mtengenezaji wa filamu, jambo la ajabu zaidi kuhusu kutazama na kikundi cha watu ni kwamba unaweza kujua ni sehemu gani za filamu zinafanya kazi na zipi hazifanyi kazi.
“Ni jambo la kuungani sha, njia ya kufanya kikundi au eneo pamoja. Nilipokuwa mdogo, kila mtu alienda kwenye sinema Jumamosi asubuhi ili kuona katuni. Ilikuwa ni ushirikiano wa kijamii, na hiyo ni moja ya mambo ya kusisimua am bayo yanaweza kutokea.
“ Broomfield anasema: “The Majestic ni kipande cha usa nifu wa ajabu ... Kwa upande wa jumuiya ya watengenezaji filamu wa Afrika Mashariki, umuhimu wa Zanzibar ungewekwa katika kufufua Majestic. Ingekuwa faraja kwa watu kuchukua sinema kwa uzito. Pia itakuwa vy ema kwa tamasha la filamu la Kimataifa la Zanzibar.”
“Nadhani ikiwa inger ekebishwa ipasavyo, watu wangeweza kwenda kwenye sinema huko mara kwa mara. Bado ina mapambo mazuri ya sanaa.”
Mmoja wa wapenzi wa sinema Beda Msimbe anas ema ana tumaini kizazi kipya kikionja ladha ya kuingia majumba makubwa na uta maduni wake wataona raha.
“Wazee bado wana ndoto zao za kutazama sinema kila wiki, wanakumbuka utukufu wa zamani wa majumba haya na enzi za ujana wao. Huo ndio umuhimu wa uta maduni wa sinema kwao.
” Majestic ya Tanga hivi karibuni ilionesha filamu ya kisayansi ya Eonii na mhudu mu wa jumba hilo anasema walijaza watu wa rika zote na kutamani hali hiyo kuendelea kuwa hivyo.
COMMENTS