WAKUU WA VYUO VYA MAENDELEO YA JAMII WATAKIWA KUZINGATIA WELEDI ILI KUZALISHA WATAALAM WENYE SIFA

Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bw.Erasimus Rugarabamu wakati ak...

Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bw.Erasimus Rugarabamu wakati akifungua kikao kazi cha wakuu wa vyuo vya Maendeleo ya Jamii kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bi.Sihaba Nkinga mjini Dodoma.
Baadhi ya Wakuu wa vyuo vya Maendeleo ya Jamii wakifuatilia mada zilizokuwa zikiwasilishwa wakati wa Kikao kazi chao mjini Dodoma leo.
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bw.Erasimus Rugarabamu (katikati) akiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jamii wa Wizara hiyo Bw. Enterberth Nyoni (wa pili kushoto) na Mwenyekiti wa Wakuu wa Vyuo vya Maendeleo ya Jamii vilivyo chini ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wazee na Watoto Bw. Paschal Joseph Mahinyila wakifuatilia michango mbalimbali ya wakuu wa vyuo vya Maendeleo ya Jamii wakati wa kikao kazi cha wakuu hao leo mjini Dodoma.
Mmoja wa washiriki wa mkutano huo akichangia jambo

Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bw.Erasimus Rugarabamu (katikati mstari wa
mbele) akiwa katika picha ya pamoja na wa vyuo vya Maendeleo ya Jamii
nchini mjini Dodoma mara baada ya kufungua kikao kazi cha wakuu hao kwa
niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bi.Sihaba Nkinga.


Na. Aron Msigwa - Dodoma.
Serikali imewataka Wakuu wa vyuo vya Maendeleo ya Jamii nchini kufanya kazi kwa kuzingatia weledi , kanuni, miongozo na taratibu zinazosimamia uendeshaji wa vyuo hivyo ili kuiwezesha sekta hiyo kupiga hatua kwa kuzalisha wataalam wenye sifa wanaokidhi matarajio ya wananchi.

Kauli hiyo imetolewa leo mjini Dodoma na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bw.Erasimus Rugarabamu wakati akifungua kikao kazi cha wakuu wa vyuo vya Maendeleo ya Jamii kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bi.Sihaba Nkinga.

Bw. Rugarabamu amewataka wakuu wa Vyuo vya Maendeleo ya Jamii kuendelea kusimamia kwa umakini mkubwa wa Rasilimali za vyuo hivyo na kubainisha kuwa Serikali haitasita kuchukua hatua za kinidhamu na kisheria kwa mkuu wa Chuo yeyote atakayeshindwa kuzingatia weledi , sheria, kanuni na taratibu zinazosimamia uendeshaji wa vyuo hivyo.

" Ninyi ndio wasimamizi wa uzalishaji wa wataalam wa Maendeleo ya Jamii nchini, mnao wajibu wa kubadilisha fikra za wananchi na kuwa chachu ya maendeleo, hakikisheni mnasimamia vizuri suala la udahili wa wanafunzi kwa kuwa na wanafunzi wenye sifa.

Aidha, amewataka wakuu hao wa vyuo kuhakikisha kuwa wanapiga vita kwa vitendo udahili wa vyeti vya kughushi ( vyeti feki) akisisitiza kuwa Serikali haitasita kuchukua hatua za kisheria na kinidhamu kwa Mkuu wa Chuo yeyoye atakayehusika kwa namna moja au nyingine kusaidia udahili wa wananfunzi wasio na sifa.

Ametoa wito kwa wakuu na Wakuu wa taaluma wa vyuo hivyo kuwa makini katika suala la udahili wa wanafunzi wanaojiunga katika fani ya maendeleo ya jamii ili kuendelea kujenga heshima ya taaluma ya Maendeleo ya Jamii na kutimiza matarajio ya kuwaletea maendeleo wananchi.

" Hakikisheni mnaepuka maslahi binafsi katika usimamizi wa taaluma, suala la vyeti feki lisiwe na nafasi katika vyuo vyetu, fanyeni kazi kwa kuzingatia sheria ili tuendelee kutoa wahitimu bora" Amesisitiza Rugarabamu.

Katika hatua nyingine amewataka wakuu hao kuwa wabunifu ili vyuo wanavyovisimamia viweze kuhimili soko la ushindani kutoka vyuo vingine vya elimu ya Maendeleo ya jamiii hapa nchini ili vyuo chini ya wizara, viweze kutekeleza majukumu kwa ufanisi na kuzalisha wataalam wanaokidhi mahitaji ya soko.

" Ili vyuo vyetu viendelee kuonekana lazima viweze kuhimili ushindani kutoka katika vyuo vingine vinavyotoa taaluma kama hii, jambo hili lazima tulifanye kwa nguvu ili tuendelee kuwa wazalishaji bora wa wataalam wa elimu ya Maendeleo ya Jamii hapa nchini" Amesisitiza Rugarabamu.

Aidha, ametoa wito kwa wakuu hao kusimamia vizuri rasilimali za fedha na kufafanua kuwa suala la upimaji wa Wazi wa watumishi wa Umma (OPRAS) lazima lizingatiwe na watumishi wote wa vyuo hivyo kwa kuwa wao ni watumishi wa umma lazima wapimwe utendaji kazi wao kwa mujibu wa vigezo vilivyowekwa.

Aidha, amewataka Wakuu hao kuhakikisha kuwa wanavisimamia vyuo wanavyoviongoza kwa mujibu wa sheria na kuhakikisha kuwa wanawasilisha taarifa kuhusu maendeleo ya vyuo vyao kwa lengo la kuiwezesha Serikali kuchukua hatua za katika maeneo ambayo hayaendi vizuri kuviwezesha vyuo hivyo kupiga hatua kitaaluma.

Awali akizungumza kabla ya ufunguzi wa mkutano huo, Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jamii wa Wizara hiyo Bw. Enterberth Nyoni amesema kuwa Mkutano huo ni muhimu sana kwa kuwa umewakutanisha wakuu wa Vyuo na Makamu Wakuu wa Vyuo wanaozalisha Maafisa Maendeleo ya Jamii nchini ambao huajiliwa na Serikali katika Mamlaka za Serikali za Mitaa, taasisi na Mashirika mbalimbali.

Amesema kuwa kufanyika kwa mkutano huo kuna umuhimu mkubwa katika maendeleo ya nchi kupitia mchango wa maafisa maendeleo ya jamii ambao husimamia shughuli za maendeleo ya wananchi kuanzia ngazi ya kijiji, kata hadi Taifa pia usimamizi na utoaji wa elimu kuhusu Haki za makundi mbalimbali katika jamii.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Wakuu wa Vyuo vya Maendeleo ya Jamii vilivyo chini ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wazee na Watoto Bw. Paschal Joseph Mahinyila amesema kuwa vyuo vya Maendeleo ya Jamii vinaendelea kufanya kazi nzuri ya kuzalisha wataalam wa masuala ya maendeleo ambao wamekua msaada kwa wananchi.

Amesema kuwa Serikali inaendelea kuifanyia kazi changamoto ya uhaba na uchakavu wa majengo inayovikabili baadhi ya vyuo vya maendeleo ya Jamii ili viweze kudahili wanafunzi wengi zaidi na kuendelea kutoa elimu katika mazingira bora.

Aidha, amesema kuwa kupitia kikao kazi hicho changamoto ya Miongozo ya uendeshaji itaweza kufanyiwa kazi ili vyuo vyote viweze kuzungumza lugha moja na kutekeleza matakwa ya Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) pamoja na kuviwezesha vyuo vya maendeleo ya jamii vilivyo chini ya wizara hiyo kuanza kutoa wahitimu wa shahada ya kwanza kwa kujiunga na Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru, Arusha.

Naye Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Rugemba, Mafinga mkoani Iringa Bi. Santina Mbata akizungumzia mara baada ya ufunguzi wa kikao kazi hicho amesema kuwa kukutana kwa wakuu hao wa vyuo vya Maendeleo ya Jamii ni fursa pekee inayowapa fursa ya kujadili masuala mbalimbali ya kisera, kisheria, taratibu na miongozo mbalimbali inayosimamia vyuo hivyo.

Bi.Santina ameeleza kuwa licha ya chuo anachokiongoza kukabiliwa na changamoto mbalimbali Serikali inaendelea kukijengea uwezo ili kuhakikisha kuwa kinaendelea kutimiza malengo ya kuanzishwa kwake kwa kuendelea kuwajengea uwezo wananchi wanaopata mafunzo kukabilina na changamoto mbalimbali za maendeleo ya wananchi.


COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4816,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: WAKUU WA VYUO VYA MAENDELEO YA JAMII WATAKIWA KUZINGATIA WELEDI ILI KUZALISHA WATAALAM WENYE SIFA
WAKUU WA VYUO VYA MAENDELEO YA JAMII WATAKIWA KUZINGATIA WELEDI ILI KUZALISHA WATAALAM WENYE SIFA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh0hyphenhyphen3xRrw2KKvdmwNaC3cd-pkLpuFAW7ho8AuIvwmaC9Cyor95TX4Pgv7tyb_GM3KiuNGro1WV7nAvHVb0nAaY6AUgqkebJJ3iw0wyskukLzsw6FHgEkgFUEZEqC1FU67jDIsOVQcDDt9g/s640/tmp_12255-Picha+na+1-1793538332.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh0hyphenhyphen3xRrw2KKvdmwNaC3cd-pkLpuFAW7ho8AuIvwmaC9Cyor95TX4Pgv7tyb_GM3KiuNGro1WV7nAvHVb0nAaY6AUgqkebJJ3iw0wyskukLzsw6FHgEkgFUEZEqC1FU67jDIsOVQcDDt9g/s72-c/tmp_12255-Picha+na+1-1793538332.JPG
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2016/07/wakuu-wa-vyuo-vya-maendeleo-ya-jamii.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2016/07/wakuu-wa-vyuo-vya-maendeleo-ya-jamii.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy