Jumuiya ya Wanafunzi wa Vyuo Vikuu Tanzania (TAHLISO) limesema linaunga mkono juhudi kubwa zinazoonyeshwa na Rais wa Jamhuri ya Muung...
Jumuiya ya
Wanafunzi wa Vyuo Vikuu Tanzania (TAHLISO) limesema linaunga mkono juhudi kubwa
zinazoonyeshwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John
Magufuli kupigania
na kuzilinda rasilimali za nchi kwa maslahi ya Taifa jambo ambalo litasaidia
kuchangia kwa kasi harakati za kimaendeleo.
Hayo yalisemwa na
Mwenyekiti wa Tahliso, Stanslaus Kadugalize katika taarifa yake kwa vyombo vya
habari nchini ambapo alisema tokea Serikali ya awamu ya tano iingie madaraka
inakaribia kutimiza miaka miwili lakini ndani ya kipindi hicho watanzania
wameona mambo mengi makubwa yakifanywa kwa ajili ya kuipa nchi
maendeleo.
Alisema moja
kati ya mambo makubwa ni suala la kiongozi huyo kupamaba na vita dhidi ya dawa
za kulevya,kuondoa watumishi hewa serikalini pamoja na wenye vyeti feki, Vita
dhidi ya ufisadi na uhujumu uchumi,kufufua shirika letu la Ndege(ATC) kwa
kununua ndege ambazo hivi sasa watanzania wanajivunia kuwa ni mali
yao.
Mwenyekiti
huyo alisema pia mambo mengine ni Ujenzi wa Reli ya kisasa, Ujenzi wa Mabweni
ya wanafunzi katika Chuo kikuu cha Dar es salaam (UDSM), utoaji wa ajira zaidi
ya 50,000 kwa vijana wahitimu, Kuimarisha utumishi wenye nidhamu na uwajibikaji
serikalini, Kuinua kwa kasi uchumi wa nchi yetu kimataifa, Kuboresha sekta ya
afya pamoja na kupunguza bei za madawa ya binadamu nchini na mengine mengi
yaliyoleta maendeleo ya nchi yetu
Alisema
pamoja na hayo lakini Rais Magufuli alionyesha ujasiri mkubwa kwa kuzuia mchanga
wa madini ya dhahabu (Makinikia) na kuunda tume ili ichunguze namna nchi
ilivyokuwa inapoteza mapatoambayo ilionyesha jinsi watu walivyoibiwa mapato ya
Taifa kwa kipindi kirefu.
“Lakini
hakuishia hapo Juzi Rais Magufuli amekabidhiwa ripoti ya uchunguzi dhidi ya
Madini ya Almas na Tanzanite iliyochunguzwa na kamati mbili zilizoundwa na Mhe.
Spika Jobu Ndugai ripoti ambayo imeonyesha jinsi watanzania tulivyoibiwa kwa
kipindi kirefu, Mhe. Rais hakusita kuwachukulia hatua wale wote waliohusika
katika kupelekea Taifa kupoteza mapato”Alisema
Alisema
sambamba na hayo suala la ukamataji wa madini ya Almas kwenye uwanja wa Ndege
yaliyokua yameripotiwa kuwa na thamani ya 31.4bn tofauti na uhalisia wake
ambapo kitaalamu almas ile ina thamani ya 64bn hii ni hatua kubwa sana ya
kiukombozi wa nchi yetu ambayo iligeuka kuwa shamba la bibi kila mtu
anajifanyia anavyotaka wazungu wanatuibia wanapeleka mali zetu kwao huku
wakituachia mashimo makubwa bila kunufaika na rasilimali
zetu.
“Kutokana na
hayo tuna kila sababu ya kumpongeza Rais Magufuli kwa kuwa ameonyesha uzalendo
wa hali ya juu bila kumuonea mtu haya bila kujali cheo cha mtu ameonyesha namna
anavyokerwa na vitendo viovu dhidi ya rasilimali za Taifa na pia kaonyesha
uchungu mkubwa wa kuzijali rasilimali za Taifa letu kwa vitendo huku
akituonyesha mfano unaopaswa kuigwa na kila Mtanzania katika vita hii kubwa ya
kuzilinda”Alisema na kuongeza kila mtanzania anapaswa kuwa mlinzi wa rasilimali
hizo kwenye mahali alipo.
Alisema
watanzania wamefika hapa walipo kwa sababu ya baadhi ya watu waliopewa dhamana
na serikali katika nyadhifa mbalimbali kukosa maadili ya uongozi kwa makusudi
ama kwa bahati mbaya (uzembe) ambao umeligharimu Taifa lna
kulisababishia kupoteza
fedha nyingi ambazo zingeweza kuisaidia serikali yetu kutuboreshea maisha yetu,
upatikanaji wa Maji, ujenzi wa barabara, Utoaji elimu bure hadi Chuo Kikuu,
huduma za afya nk.
“Hata
hivyo sisi kama TAHLISO Tunawataka ndugu zetu waliopewa dhamana na serikali hii
ya awamu ya tano ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe. John
Pombe Joseph Magufuli kwa nyadhifa mbalimbali wafanye kazi kwa bidii
na kuzingatia
maadili na miiko ya kazi zao”Alisema
Lakini pia
wakitangulize uzalendo wa nchi yetu kwa maslahi ya Taifa letu bila kuangalia
maslahi yao binafsi huku wakitambua kuwa wamesomeshwa na kodi za wanachi wa
Tanzania ili kuwatumikia Watanzania kwa moyo safi na weredi
mkubwa.
Katika hatua
nyengine Mwenyekiti huyo wa Tahaliso aliwataka vijana kuacha kukata
tamaa tusikate
tamaa wala kukatishwa tamaa na mtu kwa haya yaliyofanyika huko nyuma badala
yake wajipe moyo na kumuunga mkono Rais wa nchi ambaye amejitolea kwa nia dhati
kurudishia Tanzania Mpya itakayokuwa na kasi kubwa ya
kiuchumi.
“Lakini
pamoja na hayo tusiache kumuombea kwa mungu ili aweze kumlinbda na kumpa afya
njema katika kipindi chake cha uongozi kutokana na dhamira ya kipekee aliyokuwa
nayo kulinda rasilimaliza za nchi “Alisema.
COMMENTS